Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, February 20, 2024

Taifa Stars kuanza na Bulgaria "FIFA Series"


 Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” inatarajia kwenda nchini Azerbaijan Kwaajili ya mashindano madogo ya FIFA Series yatakayo husisha timu nne kutoka mabara tofauti.

Stars itacheza mchezo wake wa kwanza March 22 dhidi ya Bulgaria na mchezo wa pili utapigwa March 25 dhidi ya Mongolia.
FIFA Series ni mashindano madogo mbadala wa mechi za kirafiki za kimataifa timu shiriki zitakuwa ni Tanzania, Bulgaria, Mongolia pamoja na mwenyeji Azerbaijan.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Tanzania kushirikishwa kwenye mashindano hayo yanayoandaliwa na FIFA kwa mara ya kwanza pia katika kutimiza kalenda ya michezo ya kimataifa.
Mbali na Azerbaijan, FIFA pia wameandaa michezo hii kwenye mataifa ya Saudi Arabia, Algeria, Sir Lanka,
Baadhi ya nchi za kiafrika zitakazoshiriki ni pamoja na Tanzania, Zambia, Ghana , Afrika Kusini , Algeria na Ethiopia.
Bado haijawekwa wazi kama mashindano haya yatakuwa

Saturday, January 13, 2024

SBL YAZIDI KUGAWA MAOKOTO

 

Meneja mauzo wa Kampuni ya SBL mkoani Mbeya, Karolina Mwamaso( kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi 500,000 kwa mshindi wa promosheni ya Maokoto inayoemndeshwa hiyo, Patrick Mrema wa jijini Mbeya katika hafla iliyofanyika New City Pub jijini Mbeya(Na Mpigapicha Wetu)








Thursday, January 11, 2024

DK. TULIA ASHIRIKI BONANZA LA PAMOJA ZANZIBAR



 Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson,  ameshiriki Bonanza la pamoja lililohusisha michezo mbalimbali kati ya Baraza la Wawakilishi Sport club,  Bunge Sport club na NMB Sport Club lililofanyika Visiwani Zanzibar leo tarehe 11 Januari, 2024

Thursday, December 21, 2023

FAINALI LIGI YA MKOA STELLA FIYAO CUP SONGWE FURAHA NYINGINE YA X-MASS

 


FINAL LIGI YA MKOA STELLA FIYAO CUP SONGWE. kupigwa tarehe 24/12/2023 katika viwanja vya Tunduma day Sekondari iliyopo tunduma Kati ya MKWAJUNI FC kutoka Wilaya ya SONGWE na LAMBYA FC kutoka wilaya ya ILEJE kuanzia majira ya saa kumi jioni shamlashamla za fainal zitaanza mapema sana mwambie rafiki ni bonge Moja la fainal.LIGI YA MKOA STELLA FIYAO CUP 2023/2024 IMEDHAMINIWA NA MBUNGE VITI MAALUMU MKOA SONGWE MH.STELLA FIYAO

Thursday, October 26, 2023

KenGold wataka kujiimarisha zaidi kileleni Championship



 

NA MWANDISHI WETU


VINARA wa NBC Championship League KenGold FC wamewasili salama mkoani Kagera kwa ajili ya mchezo wao wa mzunguko wa nane dhidi ya Biashara United uliopangwa kuchezwa katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba Jumamosi ya Oktoba 28,2023.

Vinara hao wamesema matarajio yao ni kuendeleza ushindi kwenye michezo yake ili kujiweka mahali salama zaidi hivyo wamejipanga kupata matokeo ya ushindi katika mchezo huo wa kesho.

Akizungumza kwa njia ya simu mara baada ya kuwasili Kagera mshambuliaji wa kikosi hicho, Emanuel Mpuka alisema licha ya kusafiri umbali mrefu wachezaji wote wapo na afya njema na morali kubwa kuelekea kwenye mchezo huo.

Aamesema matarajio ya matokeo bora yanatokana na maandalizi waliyoyafanya hata kabla ya kuanza kwa safari huku akisema mabadiliko ya hali ya hewa hayatarajiwi kuwa kikwazo kwao.

"Tunaamini kwenye maandalizi tuliyojiandaa, tumekuja kupambana kusaka alama tatu,hali ya hewa ya huku inautofauti mkubwa sana na Mbeya...kuna muda joto,kuna muda baridi na wakati mwingine mvua inanyesha kabisa. Lakini hiyo haituondoei kwenye nia yetu" Amesema Mpuka

Mshambuliaji huyo mpaka sasa amefunga magoli 3 na Assist 2 kwenye kikosi cha KenGold FC ambacho kinaongoza msimamo wa NBC Championship League kikiwa na alama 16.

CHUNYA YAENDELEA KUWABURUZA WAPINZANI SHIMISEMITA DODOMA

 

Timu ya wanawake ya kuvuta Kamba ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ikiongozwa na Kiongozi mwanamama mwenye misuli Bi Devotha Mwasaga ikiendeleza ubabe wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Jijini Dodoma

NA MWANDISHI WETU, DODOMA


Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bingwa mtetezi wa mchezo wa kuvuta Kamba  SHIMISEMITA msimu uliopita msimu huu bado inaendelea kuwabuluza wapinzani wake katika michezo ya watumishi inayoendela jijini Dodoma baada ya Timu ya wanawake kuvuta Kamba kuingia nusu fainali wakati Timu ya wanaume kuvuta kamba iko Robo Fainali

                          Chunya DC Vs Moshi DC (ME) mshindi CHUNYA DC

                         Chunya DC Vs Tunduma TC (KE) mshindi CHUNYA DC

Kwa matokeo hayo  Chunya Dc wanaume wametinga hatua ya robo fainali (Mtoano) ambapo watakutana uso kwa uso timu ya watumishi kutoka Arusha jiji  huku timu ya Chunya DC wanawake wao wametinga hatua ya nusu fainali ambapo watavaa na timu Kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam (DAR CC) ambayo ni kesho asubuhi.


Kuelekea Mchezo wa Nusu Fainali kepten wa timu ya wanawakeChunya DC Kuvuta kamba Bi Devotha Mwasaga amesema kilichobaki kutoka kwa wanachunya ni dua, Sara na Maombi ili kufanikisha azma ya kuleta ushindi Chunya na hatimaye kuiheshimisha wilaya ya Chunya kwani upande wa Maandalizi hakuna changamoto yoyote timu iko salama.


“Tunachokihitaji kutoka kwa wananchunya ni maombi kila mmoja kwa Imani yake ili timu iweze kufanikiwa kutwaa ubingwa kwani upande wa maandalizi kila kitu kiko vizuri, wachezaji wana ari na morali wa kuhakikisha ubingwa unakuja Chunya hivyo tuiheshimishe Chunya yetu”.


Kwa upande wa timu wanaume kuvuta kamba kepteni wa Timu hiyo Ridhiwani Mshigati amesema bado timu iko Imara na iki tayari kwa michezo yote iliyo mbele yetu huku lengo ni lile lile kuchukua tena ubingwa katika mashindano hayo hasa kwa upande wa Mchezo wa Kuvuta Kamba.


“Kwenye mchezo wa kuvuta kamba tumeendelea na kutetea ubingwa wetu na ndo maana tumeshinda 2 bila kwa maana ya kwamba tuliocheza nao tumefunga awamu zote mbili, na kamba ina mbinu za kupata ushindi, sisi tumehatika kupata mtaalamu anatuongoza vizuri na kwasasa tuko kambini tunaendelea kupeana mbinu na kutunza nidhamu. kurudi mikono mitupu kwa Mwajiri ni aibu kubwa ambayo sisi hatutaki itokee kwetu kulingana na huduma tulizopewa na mwajili wetu.


Na tunashukuru Halmashauri jirani za Rungwe na Tunduma wanatusapo, ingawa Tunduma Tc walifungwa na timu ya wanawake kuvuta kamba tuliwaomba radhi na kuwambia kwa hili hatuna ujirani tukawatoa, Tunaomba  watu wa Chunya waendelee kutuombea ili kutetee ubingwa wetu na lengo ni siku ya kufungwa kwa Mashindano haya Halmashauri yetu ya Chunya Itajwe na Mgeni rasmi na Bendera yetu iweze kupepea mbela ya Halmashauri zaiidi ya Mia moja zilizoshiriki Mashindano hayo” amesema Mshigati.


Utofauti wa hatua yaani Timu ya wanaume kuwa hatua ya Robo Fainali (Mtoano) huku timu ya wanawake kuwa hatua ya Nusu Fainali umetokana na Idadi ya timu zilizoshiriki mchezo huo kwani Timu za wanawake zilikuwa chache kulinganisha na timu za wanaume hivyo kupelekea  kupelekea baadhi ya hatua za mashindano kuwa na mzunguko mfupi kulingana na timu za wanaume.


Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndiye Bingwa Mtetezi wa Mchezo wa Kuvuta Kamba Taifa kwa msimu wa mwaka 2022 na sasa timu zote ziko hatua nzuri kutetea ubingwa mwaka huu 2023, Maombi, bahati pamoja na kujituma vitaendelea kuhitajika ili timu zetu ziendelee kufanya vizuri

Friday, August 11, 2023

USHIRIKI WA MASHUJAA FC LIGI KUU TANZANIA KUONGEZA CHACHU YA MAENDELEO KIGOMA


 Na Mwandishi Wetu, Kigoma.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema ushiriki wa Timu ya Mashujaa FC katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara utaongeza chachu ya Maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Kigoma.

Andengenye ametoa kauli hiyo alipotembelea na kukagua Maendeleo ya Ukarabati wa Uwanja wa CCM Lake Tanganyika Stadium utakaotumiwa na Timu ya Mashujaa kwa ajili ya michezo ya nyumbani katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara Msimu wa 2023/2024.

Ameeleza kuwa, kutokana na ushiriki wa timu hiyo, Mkoa utapokea wageni kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kushuhudia michezo ya ligi kuu ambapo kuanzia wafanyabiashara wakubwa  hadi wajasiriamali wadogo watapata fursa ya kunufaika kiuchumi kutokana na kuwahudumia wageni hao.

"Pamoja na kupata burudani, michezo inatoa fursa  mbalimbali za kujiimarisha kiuchumi kupitia biashara, nitoe wito kwa wafanyabiashara na wakazi kwa ujumla tuchangamkie fursa za kiuchumi zitakazojitokeza ambazo zitatokana na wageni watakaokuja kwa ajili ya kushuhudia michezo mbalimbali ya ligi kuu" amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Upande wake Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mha. Francisco Magoti amesema ukarabati huo unahusu maeneo ya majukwaa, vyumba vya kubadilishia nguo kwa wachezaji, ukumbi wa mikutano, vyoo pamoja na eneo la kuchezea mpira.

" Mafundi wapo kazini na tutahakikisha  maboresho muhimu yanakamilika kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi kuu Tanzania Bara ili kuruhusu michezo ifanyike kama ilivyopangwa huku uwanja ukiwa katika ubora unaotakiwa" amefafanua Magoti.

Upande wake Afisa Vijana Mkoa wa Kigoma, Edward Manase amesema  wameridhishwa na maendeleo ya kazi mbalimbali zinazofanyika za marekebisho ya uwanja huo huku akiwahimiza watendaji kutanguliza uzalendo na kuzingatia ubora.

Hisia zote:
6

MAMBO YOTE NI KESHO,TUKUTANE UYOLE

 


 


Wednesday, June 28, 2023

 https://www.facebook.com/100001526491541/videos/163778579924492/

Wednesday, June 14, 2023

SINGIDA BIG STARS YAPIGWA MNADA

Na Lyamba Lya Mfipa
Uongozi wa klabu ya Singida Big Stars umefikia makubaliano ya kuiuza timu hiyo kwa wamiliki wa Fountain Gate.

Mtendaji Mkuu wa Singida Big Stars John Kadutu amesema hayo mkoani Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Amesema wameridhia kuiuza timu hiyo kwa fountain Gate, lakini kwa sharti la timu hiyo kubakia mkoani Singida.
Kwa upande wake Mmiliki mpya wa Timu hiyo Japhet Makau amesema, fursa hiyo imekuja katika wakati muafaka ndio maana wamemua kuichangamkia.
Kwa sasa jina la Singida Big Stars limebadilishwa na kuitwa Singida Fountain Gate Football Club.

MICHUANO TULIA TRUST BODABODA CUP 2023 YAZINDULIWA RASMI.

 
Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa akisalimiana na wachezaji wa timu za Madereva Bodaboda za Uyole na Stendi kuu kwenye uzinduzi wa Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge.

Na Joachim Nyambo, Mbeya.

 

MEYA wa jiji la Mbeya Dormohamed Issa amezindua rasmi michuano ya Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 yatakayoshirikisha timu nane kutoka kanda za madereva bodaboda zilizogawanywa kwenye makundi mawili ya A na B.

 

Michuano hiyo imerejea tena baada ya kusitishwa kwa misimu miwili mfululizo ambapo kwa mara ya kwanza yalifanyika 2019 lakini kwa miaka iliyofuata haikufanyika kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo mlipuko wa Covid-19

 

Kwa upande wa kundi A timu zinazoshiriki michuano hiyo ni za madereva bodaboda kutoka kanda za Iyunga, Stendi Kuu, Soweto na Kabwe wakati kundi B zipo timu za kanda za Mafiati, Sae, Uyole na Kadege.

 

Akizindua michuano hiyo katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge, Meya wa jiji la Mbeya Meya Issa ameipongeza Taasisi ya Tulia Trust inayoyaandaa akisema yana mchango mkubwa katika kuibua na kukuza vipaji vya vijana.

 

Amewasihi madereva bodaboda kutumia michuano hiyo situ kwa kuibua vipaji vyao bali pia kuimarisha afya zao hivyo kuwataka kuwa na nidhamu ya hali ya juu wakati wote yatakapokuwa yanaendelea.

 

“Mpira unaanza kucheza chini lakini haujui huko mbele utafika wapi…naamini kabisa kuna wachezaji miongoni mwenu mkionyesha nidhamu mkazingatia yale mnayofundishwa na walimu kuyafuata ipo siku mtafika mbali.”  

 

“Mpira ni nidhamu..na ukitaka kufanikisha katika jambo lolote weka nidhamu mbele..ukiamua kuwa padre weka nidhamu mbele, ukitaka kuwa shekh weka nidhamu mbele na hata ukitaka kuwa kiongozi wajali watu wako.” Amesisitiza Issa.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano ya Chama cha soka Mbeya mjini(Mufa), Ramadhan Nyambala amesema kutokana na ari ya mpira wa miguu katika mkoa wa Mbeya ni muhimu wadau wengi kuzidi kujitokeza kuandaa mashindano mbalimbali.

 

Amesema kuandaliwa kwa mashindano kama ya Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 ni sehemu ya mikakati muhimu na inayotarajiwa kwenye kuibua na kukuza vipaji vya vijana.

 

Afisa Habari na Mawasiliano wa Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema baada ya michuano hiyo kufanyika kwa mara ya kwanza 2019 iaka miwili mfululizo ilisimama kutokana na changamoto mbalimbali zilizoibuka ikiwemo cha mlipuko wa ugojwa wa corona.

 

Mwakanolo amesema michuano hiyo itakayokuwa ikifanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge na Magereza Mbeya yanatarajia kufikia tamati mwezi ujao huku akisema zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu zitatangazwa hivi karibuni.

Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa akisalimiana na waamuzi wa mchezo kati ya timu za Madereva Bodaboda za Uyole na Stendi kuu kwenye uzinduzi wa Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge.