Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, July 25, 2014

SIKU YA MASHUJAA YAFANA MBEYA

BAADHI YA MAOFISA WA JESHI LA WAANANCHI(JWTZ) WAKIWA WAMESHIKA NEMBO MBALIMBALI ZA MASHUJAA KWAAJILI YA VIONGOZI WA NGAZI MBALIMBALI KIMKOA KUWEKA KATIKA MNARA WA MWENGE WA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA. MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO AKITOA HESHIMA MARA BAADA YA KUWEKA NGAO NA MKUKI KATIKA MNARA WA MASHUJAA JAMII mkoani Mbeya imetakiwa kujiuliza ni kwa namna gani itaweza kukumbukwa na vizazi vijavyo kulingana na historia ya kulitumiakia taifa la Tanzania. Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na wakazi jijini Mbeya waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya Siku ya mashujaa zilizofanyika katika maeneo ya Mnara wa Mwenge jijini humo. Bw.Kandoro amesema uwepo wa siku ya kuwakumbuka mashujaa kunaikumbusha jamii kutambua kuwa kuna watu waliojitolea kumwaga damu yao ili kwaajili ya kulinda taifa lao. Amesema huenda bila uwepo wa watu waliomwaga damu zao kulilita taifa,wanaoitwa mashujaa hivi sasa taifa la Tanzania lisingekuwa katika muonekano wa hali ya amani na utulivu. Amesema ni wakati sasa kwa wanajamii kujiuliza kizazi kijacho kitawakumbuka kwa mazuri yapi waliyoyatenda kwa taifa lao. Amesema kumbukumbu nzuri pekee na itakayoenziwa kwa heshima ni kuidumisha amani na utulivu uliopo kwa kila mmoja kuhakikisha anatekeleza wajibu wake wa kushirikiana na mwenzake kwa moyo wa upendo na mshikamano.

No comments:

Post a Comment