Kama kweli laana
ipo,naomba eeh Mwenyezi Mungu walaani watu wanaofanya ukatili huu.Huyu ni
mwanamke Suzana Mgasa Mungu (34),aliye na ulemavu wa ngozi(Albino).
Mwanamke huyu
alifanyiwa ukatili wa kujeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili wake na watu
wasiojulikana na hatimaye watu hao kuondoka na sehemu ya mkono wake baada ya
kumuua mumewe wakati akijaribu kupambana kumwokoa mkewe.
Tukio hili lilitokea
Agosti 15 mwaka huu majira ya saa tano usiku huko Igunga Tabora.Vitendo hivi
vya kikatili vimekuwa vikifanyika nchini na kulipa sifa mbaya taifa la
watanzania wajiitao kisiwa cha amani.
Ewe mwenyezi Mungu
mjaalie afya njema Suzana,na nakuomba andika majina ya waliofanya ukatili huu
katika kitabu chenye orodha ya watu wasiopaswa kusamehewa kamwe.
PICHA KWA HISANI YA TANZANIA ALBINISM SOCIETY
No comments:
Post a Comment