Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, September 20, 2014

WALIMU 26 WAHITIMU MAFUNZO YA WAVU MBEYA



 Wahitimu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuhitimu mafunzo yao ya siku tano







 Mkufunzi Somo Ahmed Kimwaga ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ufundi ya TAVA akifundisha washiriki namna ya kucheza mchezo wa wavu




WALIMU 26 kutoka shule za msingi na sekondari za wilaya mbalimbali mkoani Mbeya wamehitimu mafunzo ya awali ya mchezo wa wavu mkoani Mbeya yaliyoandaliwa na chama cha mchezo huo nchini(TAVA).

Mafunzo hayo yaliyoanza Septemba 15 mwaka huu yamemalizika leo chini ya mkufunzi kutoka TAVA Somo Ahmed Kimwaga ambapo lengo ni kuhamasisha mchezo huo mashuleni.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa Kimwaga amesema sambamba na mafunzo hayo washiriki watapata fursa ya kuanzisha chama cha wavu mkoa ili kiwezo kuwa sehemu ya hamasa ya mchezo huo.

Aliwataka washiriki kuhakikisha wanakwenda kuyafanyia kazi yale waliyojifunza badala ya kujijengea sifa kwa kupata chetio na kwenda kukitundika ukutani.

Hata hivyo Kimwaga alisema kukosekana kwa vyama vya wavu katika ngazi za mikoa ni changamoto inayokwamisha utekelezaji wa Tava katika kuhamasisha mchezo huo.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Mwalimu Davis Mwakalinga alisema iwapo mchezo wa wavu utapata wadau wa kuuwezesha ni mchezo mzuri na wenye heshima yake katika jamii.

Amesema ni mchezo unaoweza kuiwezesha nchi kujipatia umaarufu mkubwa kimichezo iwapo mikakati ya dhati itawekwa kuuwezesha.

Mshiriki mwingine Mwalimu Yasinta Mafuru amesema ushiriki mdogo wa wanawake katika mafunzo hayo ambao wako wawili pekee kati ya washiriki 26 inatokana na hamasa ndogo katika jamii juu ya ushiriki wa mwanamke katika michezo.


No comments:

Post a Comment