Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, March 20, 2015

JAPAN YAITABIRIA MAKUBWA TANZANIA



                      HABARI KAMILI

BALOZI wa Japan nchini Kazuyoshi Matsunaga ameitabiria makubwa Tanzania iwapo wasomi wa  nchi hii watachukua hatua mathubuti za kitaaluma na kizalendo katika kulitoa taifa  kwenye umaskini na kulipeleka mbele kimaendeleo.


Matsunaga ameyasema hayo wilayani Ileje wakati wa hafla ya kusaini hati ya makubaliano ya  mkataba wa ujenzi wa chuo  cha ufundi(VETA) kati ya balozi huyo na na viongozi wa serikali wilayani hapa ambapo Japan itachangia  kiasi cha shilingi milioni 160.

Amesema kuwa Tanzania ina rasilimali nyingi ambazo wasomi wakizitumia vizuri fani zao nchi yao itakwenda mbele na kuwa taifa lenye uwezo mkubwa wa kiuchumi .

Akitumia picha za mji mkuu wa Japan Tokyo alionyesha mwonekano ulivyokuwa mara baada ya vita  kuu ya pili ya Dunia ukionekana kuharibiwa vibaya huku kukiwa hakuna miundombinu yoyote kama vile majengo na umeme.

                          
Aliongeza kuwa walioifikisha Japan ilipo sasa kimaendeleo ni wasomi ambao walitanguliza uzalendo kwa taifa lao huku nchi hiyo ikiwa haina rasilimali kama ilivyo kwa Tanzania ambayo ina utajiri mkubwa wa madini kama vile dhahabu na almasi lakini iko nyuma kimaendeleo.

Matsunaga alisisitiza kuwa wahitimu wa vyuo vyote vinavyoanzishwa nchini wanapaswa wawe chachu ya maendeleo katika maeneo yao na taifa kwa ujumla.

Naye Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene alitoa wito kwa wasomi waishio nje  ya Ileje kuwekeza wilayani  kwao hatua aliyosema itaongeza kasi ya maendeleo hususani kwa wilaya zilizopo pembezoni.

No comments:

Post a Comment