Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, April 18, 2015

SIMBA ACHINJWA NA MBEYA CITY 2-0



MCHEZO wa ligi kuu ya Tanzania bara kati ya Mbeya City ya jijini Mbeya na Simba Sc ya Dar es salaam umemalizika kwa timu ya samba kukubali kipigo cha goli mbili 2-0.

Ilikuwa dakika ya 45 yaaani sekunde chache kabla ya mapumziko,Paul Nonga alipowanyanyua mashabiki wa Mbeya City baada ya kufunga goli la kwanza akiunganisha pasi kutoka kwa Deus Kaseke.

Goli hilo likadumu hadi timu hizo zinakwenda mapumziko huku katika kipindi hicho cha kwanza timu zote zikionesha uwezo sawa kwa kufanya mashambulizi kwa zamu lakini kama ilivyokuwa kabla ya mchezo,kipindi hicho cha mapumziko pia wachezaji wa timu ya Simba hawakwenda katika vyumba vya kubadilishia nguo na badala yake wakabakia katika benchi lao wakisubiri kuanza kwa kipindi cha pili cha mchezo.

Kipindi cha pili kikaanza kwa timu zote kuonesha kuonesha kuwa zilikitumia vyema kipindi cha mapumziko japo katika kipindi hiki Simba wakaonekana kupwaya kwa Mbeya City kiasi cha kuruhusu mashambulizi mengi langoni kwao huku safu ya kiungo ikionekana kushindwa kustahimili kasi ya mchezo.

Dakika ya 69 ya mchezo,Peter Mwalyanzi maarufu kama afisa mipango,akawanyenyua tena mashabiki wa Mbeya City waliofurika ndani ya dimba la Sokoine baada ya kupachika goli safi na la kiufundi kutokana na uwezo wake binafsi uliosababisha walinzi wa Simba kubakia wakimsindikiza wakati akienda kutekeleza adhma aliyotumwa na timu yake.

Katika kipindi hicho cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ambapo wenyeji Mbeya City waliwatoa Peter Mapunda,Cosmas Fredy na Deus Kaseke na nafasi zao zikachukuliwa na Hamad Kibopile,Peter Mwalyanzi na Seleman Hassan.

Kwa upande wao Simba waliwatoa Abdi Banda na Elius Maguli na kuwaingiza uwanjani Awadh Juma na Issa Abdalah.

Hadi kipenga cha mwisho cha mwamuzi Zacharia Jackob kutoka mkoani Pwani Mbeya City 2,Simba SC maarufu kama mnyama bila.

No comments:

Post a Comment