WANANDOA
wawili wakazi katika kitongoji cha Makambo Kata ya Itenka wilayani Mlele
Mkoani Katavi wameuawa kikatili kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa
kichwa na kiwiliwili baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana wakati
wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao.
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari amewataja wanandoa hao wawili waliouawa kuwa ni Seth Mwakalimbwa (65) na Yakoba Kalulu(48) wakazi wa kitongoji hicho.
Kidavashari
amesema jana kuwa tukio hilo la mauaji ya kikatili lilitokea hapo juzi nyakati
za usiku wa manane nyumbani kwa wanandoa hao waliokuwa wakiishi pamoja
kama mke na mume
Amesema kwamba marehemu hao wakutwa na mauti hayo wakati wakiwa ndani ya nyumba wamelala ambapo kundi la watu wasiofahamika walivamia nyumba yao na kuwaua kwa kuwakata kata na mapanga mwilini kiasi cha kupoteza fahamu kisha kuwachinja kwa kuwatenganisha kichwa na kiwiliwili.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa, Balozi wa eneo hilo, Wilbroad Mahenge alisema kuwa yeye ndio alibaini kutokea kwa mauaji hayo baada ya kutowaona wanandoa hao kwa siku mbili pasipo kuwa na taarifa yoyote.
Mahenge alisema kuwa kutokana na kutokuwa na taarifa yoyote ukizingatia kwamba pia yeye ni jirani yao, alikwenda katika makazi yao na alipofika hapo, alikuta milango ya nyumba yao iko wazi hali ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Ameongeza kwamba alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika hivyo aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hali hiyo, Mahenge alitoka nje na kasha alikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitoa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda Kidavashari amesema chanzo cha tukio la mauaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo lakini polisi inaendelea kuwasaka watu hao.
Amesema kwamba marehemu hao wakutwa na mauti hayo wakati wakiwa ndani ya nyumba wamelala ambapo kundi la watu wasiofahamika walivamia nyumba yao na kuwaua kwa kuwakata kata na mapanga mwilini kiasi cha kupoteza fahamu kisha kuwachinja kwa kuwatenganisha kichwa na kiwiliwili.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa, Balozi wa eneo hilo, Wilbroad Mahenge alisema kuwa yeye ndio alibaini kutokea kwa mauaji hayo baada ya kutowaona wanandoa hao kwa siku mbili pasipo kuwa na taarifa yoyote.
Mahenge alisema kuwa kutokana na kutokuwa na taarifa yoyote ukizingatia kwamba pia yeye ni jirani yao, alikwenda katika makazi yao na alipofika hapo, alikuta milango ya nyumba yao iko wazi hali ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Ameongeza kwamba alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika hivyo aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hali hiyo, Mahenge alitoka nje na kasha alikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitoa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda Kidavashari amesema chanzo cha tukio la mauaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo lakini polisi inaendelea kuwasaka watu hao.
CHANZO-PEMBEZONI KABISA BLOG
No comments:
Post a Comment