Mratibu wa mpango wa mafunzo ya ufundi ya muda mfupi katika
chuo cha VETA Mkoa wa Mbeya, Benedict Chuwa (kulia) akitoa maelezo juu
ya ugawaji wa vifaa kwa vijana walishiriki mafunzo hayo kwa msaada wa
shirika la vijana la Marekani kushoto ni Mkurugenzi wa Veta nyanda
Justin Rutha amabaye alikuwa mgeni rasmi katika zoezi hilo.
Mkurugenzi wa VETA nyanda za juu kusini Justin Rutha akizungumza na viijana washio katika mazingira magumu kutoka jiji la Mbeya kabla ya kuwakabidhi vifaa vya ufundi katika fani mbalimbali vilivyo tolewea na shirika la vijana kutoka Marekani.
JUMLA ya vijana 69
wanaoishi katika mazingia magumu na hatarishi jijini Mbeya wamehitimu mafunzo
ya muda mfupi ya ufundi stadi katika fani mbalimbali zinatolewa na chuo cha
Ufundi Veta Mkoani Mbeya.
Akizungumza mbele ya mgeni
Rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Veta Nyanda za juu kusini Justin Rutha,mratibu wa
wa mufunzo hayo,Benedict Chuwa alisema kuwa Mafunzo hayo yalifanyika kwa muda
miezi mitano ambapo miezi mitatu ilikuwa kwa nadharia ni miezi miwili ilikuwa
kwa vitendo na yalilenga kuwasaidia vijana waishio mazingira magumu.
Mafunzo hayo yanayo
fadhiliwa na sahirika na vijana la Marekani (Internation Youth Foundation) ‘IYF’
kwa kulipia ada ya masomo kiasi cha
shilingi 400,000/ kwa kila mwanafunzi sanjali na kuwapa vifaa kila kijana kutokana na fani aliyo
somea ili kwenda kuanza maisha ya kujitegemea.
Chuwa alisema kuwa mafunzo
hayo yalianza kutolewa Oktoba 2 mwaka jana na kufikia mwisho April mosi mwaka
huu walianza vijana zaidi ya 70 lakini ni vijana 69 ndiyo waliohitimu katika
fani saba tofauti ambazo ni,Ushonaji,Ujenzi,Mapambo na Saloon,Fundi
bomba,Upishi,Uchomeleaji wa Vyuma na fundi magari pamoja na Udereva na kwamba
vifaa vilivyo nunuliwa vimegharimu jumla ya shilingi milioni tatu chini ya
ufadhili huo.
Akizungumza juu ya
zoezi lilivyo endeshwa jinsi ya kuwapata vijana hao Chuwa alisema
Chuo cha Veta kiliwasiliana na Halmashuri ya jiji la Mbeya ili kuweza kuwabaini
vijana wanoishi katika mazingira magumu kutoka baadhi ya kata jiji hapa na baada
ya hapo mafunzo yalianza rasmi.
Kwa upande wake Mkurugenzi
wa Veta nyanda za juu kusini,inayojumisha mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi,
Rutha alisema kuwa ni vema vijana hao wakatambua lengo la mafunzo ni kumfanya
fundi awe mairi katika fani husika badala ya kuwa wababaishaji.
Rutha aliongeza mafunzo
waliopata ni muhimu na yanahitaji katika
jamii na kwamba ni vema ujuzi waliopata ukawa chachu ya kuleta mabadiliko ya
kiuchumi na katika familia zao, kwani kufanya hivyo kutawasukuma wafadhili kuendeleo
kutoa misaada kwa vijana wengine ambao waliokosa fursa hiyo.
‘Kwanza niwapongeza kwa
udhubu wenu kukubali na kujitokeza kushiriki mafunzo hayo lakini pia kwa
uvumilivu wenu katika miezi yote mitano ya mafunzo ya vitendo na nadharia
lakini ni vema mkatambua kuwa fani mlizosomea ni mhunimu na zinahitaji kila
kukicha hivyo niwa sii mnapaswa kujituma ili kuchochea maendeloa ya familia
zenu na taifa kwa ujumla’alisema Rutha.
‘Na mjua wazi mkifanya
vizuri wafadhili wataendelea kuisadia jamii yetu lakini mkifanya vibaya
mtakatisha tamaa,pia elimu mliopata hapa haitoshi bali iwe kichocheo cha
kujifua zaidi katika masuala ya ufundi’alisema Rutha.
Akitoa ushuhuda mmoja wawa
washiriki wa mafunzo hayo Irene Josphat ambaye amesomea katika fani ya Saloon na
Mapambo alisema kuwa awali kabla hajashiriki mafunzo hayo alikuwa hana ujuzi
lakini sasa amekuwa na utaalamu mkubwa katika masula ya nywele na upambaji.
No comments:
Post a Comment