Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, May 28, 2016

KUMEKUCHA KIPYE CUP 2016,TIMU 14 KUTEULIWA KUSHIRIKI

MAANDALIZI ya Mashindano ya kuibua vipaji katika soka Wilayani Mbarali mkoani Mbeya ya Kipye Cup 2016 yamezidi kushika kasi ambapo kesho(Mei 29) timu 14 zinatarajiwa kupitishwa ili kushirili mashindano hayo.

Kwa mujibu wa mratibu wa Kipye Cup,Frank Kipye,mashindano hayo ambayo ni msimu wa tatu sasa tangu kuasisiwa kwake yatashirikisha timu 14 ambapo tati ya hizo 10 zitakuwa zikitokea katika kata ya Mapogoro wilayani Mbarali na nne ni kutoka nje ya kata hiyo ili kuleta ushindani.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa,Kipye amesema kamati ya ligi hiyo kesho itakuwa na kazi ya kupitisha timu 14 kati ya zile zilizochukua fomu kuomba usajiri wa kushiriki mashindano hayo.

Amesema mara baada ya timu shiriki kuteuliwa,kazi itakayokuwa imesalia ni kutangaza tarehe rasmi ya kuanza kwa michuano huku akisisitiza kuwa zawadi kwa msimu huu ni mshindi wa kwanza Ngombe mwenye thamani isiyopungua shilingi milioni 1.5,mshindi wa pili lakini tano,wa tatu laki tatu.

“Lengo la mashindano hayo ni kuibua vipaji vya soka sambamba na kutoa hamasa kwa jamii kupenda michezo kutokana na faida zake nyingi ikiwemo vijana kuepuka matumizi ya dawa za kulevya,ulevi na pia ngono zembe.”

Kipye amesema msimu huu mashindano yanatarajiwa kuwa na mvuto zaidi kutokana na kamati ya maandalizi kuamua kuongeza idadi ya timu kutoka nje ya kata ya Mapogoro.

“Ligi itaendeshwa katika uwanja uliopo Mabadaga kata ya Mapogoro.Tumeona tuongeze timu kutoka nje ya kata ili kuleta mvuto zaidi.Mwaka jana tulishirikisha timu mbili tu kutoka nje ya kata.”anasema Kipye.

Kwa msimu wa mwaka jana bingwa wa ligi hiyo ilikuwa timu ya Kapunga FC ambao mwaka huu wanatarajiwa kuwa mabingwa watetezi.

No comments:

Post a Comment