Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, April 19, 2018

TEMBO WAMVAMIA KIKONGWE,WAMJERUHI HADI KIFO


WANYAMA Tembo watatu wamemvamia na kumjeruhi na kimsababishia kifo Kikongwe aliyefahamika kwa jina la Sixbertha Mtundu(88) mkazi wa kitongoji cha Mbuyuni mtaa wa Ihanga kata ya Rujewa wilayani Mbarali

Afisa Mtendaji wa Kata ya Rujewa wilayani Mbarali,John Mpangala amesema tukio limetokea juzi saa 11 za jioni maeneo yaliyopo jirani na Ikulu ndogo ya wilaya ya Mbarali.

Mpangala amesema kikongwe huyo amevamiwa na tembo hao wakati akitokea shambani kwake na inasadikika kutokana na umri wake mkubwa huenda hakuwaona wanyama hao mapema na pia alishindwa kukimbia baada ya kuvamiwa.

Hata hivyo Afisa mtendaji huyo amesema tukio hilo liligunduliwa na msamaria mwema mmoja aliyepita eneo hilo na kukuta kikongwe huyo akiwa amelala njiani huku amejeruhiwa vibaya kwa kukanyagwa na tembo na ndipo mkazi huyo alikwenda kwa mwenyekiti wa kitongoji na kumjulisha na ndipo wakaenda eneo husika ikiwa ni majira ya saa moja na nusu usiku lakini wakakuta amekufa.

Afisa mtendaji huyo amesema walichokifanya baada ya tukio hilo ni kuwapa taarifa wenyeviti wa vitongoji vya maeneo ya jirani ili waweze kuwapa tahadhali wananchi kuwa bado tembo hawajulikani walipo japo njia waliopikuwa wakielekea inakwenda eneo la Hifadhi ya Mpanga Kipengele hivyo huenda wapo au wamekwenda hifadhini.

Amesema eneo la tukio kwa miaka ya nyuma ilikuwa njia(Shoroba) ya wanyama lakini baada ya shughuli mbalimbali za kibinadamu hususani kilimo na makazi kukithiri wanyama hawakuendelea kupita tena.





No comments:

Post a Comment