Thursday, July 4, 2024
Tuesday, July 2, 2024
BONANZA BAAAB KUBWA KUFANYIKA WEEKEND HII
Timu ya watumishi ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya inataraji kwenda Jijini Mbeya Mwishoni mwa wiki hii July 6, 2024 Kushiriki katika Bonanza la Watumishi Lililoandaliwa na Afisa Michezo Mkoa wa Mbeya, litakalofanyika katika Uwanja wa Sokoine
Monday, July 1, 2024
NDIYOOO!! MWAMBA WA LUSAKA KATUA JANGWANI!
MIAKA 33 iliyopita
ndipo alizaliwa katika familia iliyosheheni Vipaji vya soka. Akakulia Zambia, Akahitimu
elimu ya Sekondari 2009.
Kisha akajikita rasmi
kwenye Soka akiwa na Zesco United. Akaisaidia Zesco kufika Nusu Fainali ya
Klabu Bingwa Afrika
Kipaji kikampeleka
kucheza katika nchi mbalimbali zikiwemo Misri, Morocco na Tanzania yenyewe
ambako amekuwa Mchezaji bora wa muda wote wa Tanzania.
Ni Mchezaji mwenye mguu
wa dhahabu, huchoki kumtazama, anakupa matokeo wakati wowote. Anafunga na
ana-assit na kuburudisha kwa Pamoja.
Si mwingine, huyu ni Fundi
Clatous Chama, naam! Ndiye yeye
"Mwamba wa Lusaka" hii leo amejiunga na Klabu ya Yanga SC, Mabingwa
wa Soka la Tanzania.
Matarajio ya wapenda
soka ni kuwa baada ya kutua Jangwani rasmi sasa ataendelea kutamba kwenye Uwanja wake aliouzoea, Uwanja
anaoutumia siku zote kuandika na kuvunja rekodi zake na kuweka mpya, Uwanja wa
Benjamin Mkapa... Ndiyo! Lupaso!
Je Mwamba wa Lusaka
bado yupo yupo sana kuwatesa Mabeki akiwa katika soka la Tanzania? Au mambo
yatakuwa tofauti!, Acha Inyeshe Tuone Panapovuja!!!