Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, July 1, 2024

NDIYOOO!! MWAMBA WA LUSAKA KATUA JANGWANI!

 


MIAKA 33 iliyopita ndipo alizaliwa katika familia iliyosheheni Vipaji vya soka. Akakulia Zambia, Akahitimu elimu ya Sekondari 2009.

 

Kisha akajikita rasmi kwenye Soka akiwa na Zesco United. Akaisaidia Zesco kufika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa  Afrika

Kipaji kikampeleka kucheza katika nchi mbalimbali zikiwemo Misri, Morocco na Tanzania yenyewe ambako amekuwa Mchezaji bora wa muda wote wa Tanzania.

 

Ni Mchezaji mwenye mguu wa dhahabu, huchoki kumtazama, anakupa matokeo wakati wowote. Anafunga na ana-assit na kuburudisha kwa Pamoja.

 

Si mwingine, huyu ni Fundi Clatous Chama, naam! Ndiye yeye  "Mwamba wa Lusaka" hii leo amejiunga na Klabu ya Yanga SC, Mabingwa wa Soka la Tanzania.

 

Matarajio ya wapenda soka ni kuwa baada ya kutua Jangwani rasmi sasa ataendelea kutamba  kwenye Uwanja wake aliouzoea, Uwanja anaoutumia siku zote kuandika na kuvunja rekodi zake na kuweka mpya, Uwanja wa Benjamin Mkapa... Ndiyo! Lupaso!

 

Je Mwamba wa Lusaka bado yupo yupo sana kuwatesa Mabeki akiwa katika soka la Tanzania? Au mambo yatakuwa tofauti!, Acha Inyeshe Tuone Panapovuja!!!

No comments:

Post a Comment