Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, October 19, 2016


WATU SITA WAFA KWA AJALI MBEYA




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.



 
                                                                                                  Ofisi ya Kamanda wa Polisi,                                                                                                                                                                                                                                                                                       Mkoa  wa  Mbeya,                                                                                    
Namba ya simu 2502572                                                                                   S. L. P. 260,
Fax - +255252503734                                                                                             MBEYA.
               tanpol.mbeya@gmail.com                                                       

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 19.10.2016.

Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu. Mafanikio yaliyopatikana katika Misako ni kama ifuatavyo:-

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO]

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja mkazi wa Kitongoji cha Masanza Wilaya ya Chunya aliyefahamika kwa jina la CHRISTINA PHILIPO [44] akiwa na Pombe haramu ya moshi [gongo] yenye ujazo wa lita 05.

Mtuhumiwa alikamatwa mnamo tarehe 18.10.2016 majira ya saa 11:00 asubuhi katika msako uliofanyika huko Kitongoji cha Masanza, kijiji na kata ya Bwawani, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya.

Aidha mtuhumiwa alikamatwa akiwa na Mtambo mmoja wa kutengenezea Pombe hiyo haramu. Taratibu za kumfikisha mahakamani zinaendelea.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya pia linaongeza jitihada za kuzuia na kupunguza ajali za barabarani kwa kuhakikisha madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatii sheria za usalama barabarani. Aidha kumekuwa na tukio 01 la ajali ya kifo kama ifuatavyo:-

AJALI YA VIFO.

Mnamo tarehe 18.10.2016 majira ya saa 15:50 jioni huko katika Kijiji cha Majimazuri, Wilaya ya Mbeya Vijijini katika Barabara ya Mbeya/Chunya Gari lenye namba za usajili T.841 BRW aina ya Isuzu basi likitokea Wilaya ya Chunya kwenda Mbeya likiendeshwa na dereva aitwaye ELIA ISACK [37] Mkazi wa Chunya liliacha njia, kupinduka na kusababisha vifo kwa abiria wanne ambao ni



1. HAWA MOHAMED [30] mkazi wa Chunya  2.  Mtoto mdogo miaka 2 wa kiume ambaye bado kufahamika jina lake 3. Mwanaume    asiyefahamika jina na 4. Mwanaume asiyefahamika.

Aidha katika ajali abiria 22 walijeruhiwa kati yao wanawake 14 na wanaume 08.  Majeruhi walitambulika kwa majina ya 1. HAPPY       BAKARI [28] Mkazi wa Mabatini 2. FAIDA MBUYI [47] mkazi wa        Igodima 3. AGNESS LUSUPA [45] Mkazi wa Ileje 4. EMMY           MWASIMBIHABI [35] Mkazi wa Mwakaleli 5. LONGI    MWALUVANDA [45] Mkazi wa Chunya 6. SIWANGU PAUL [28]       Mkazi wa Simike 7. RODA GUNZA [38] Mkazi wa Chunya 8.       ANITHA FRANK [18] Mkazi wa Igodima 9. MAGDALENA ALMASI          [19] Mkazi wa Iganzo 10. AGNESS NDOKILE [38] Mkazi wa Iganzo     11. ELIZA GIDION [21] Mkazi wa Chunya 12. JULIANA MWAMPASHI [36] Mkazi wa Chunya 13. SARAH ENOCK umri wa mwaka mmoja na nusu Mkazi wa Chunya na 14. EMMA ANGETILE           [35] Mkazi wa Chunya.

Majeruhi wengine ni 1. MOSES JACKSON [29] Mkazi wa Itaka 2. JOHNPHANCE SAMSON [35] Mkazi wa Mbozi 3. PETRO LYANGA          [24] Mkazi wa Tunduma 4. ISSA KALINGA [18] Mkazi wa Chunya 5. RICHARD KIHAMI mkazi wa Chunya 6. STARD MWASHITETE [34]           Mkazi wa Mbozi 7. MWANDALIMA JOSEPH miaka kati ya 35 – 40 na        8. CHEYO NDELE [32] Mkazi wa Mbeya.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Majeruhi wote wamelazwa Hospitali         ya Rufaa Mbeya. Dereva amekamatwa, Upelelezi unaendelea.


Mnamo tarehe 18.10.2016 majira saa 21:41 usiku huko eneo la Mlima Nyoka, Kata ya Itewe, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Gari lenye namba za usajili T.660 APR aina ya Toyota Pick up ikiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la JACOB SANGA iliacha njia na kupinduka kisha kusababisha kifo cha RAHEL SASITA [55] Mkazi wa Itewe.

Aidha katika ajali hiyo watu wawili walijeruhiwa ambao ni 1. ANNA SANGA [45] Mkazi wa Chemchem na 2. VENANCE OSIA [50] Mkazi wa Mwanyanje. Chanzo cha ajli ni mwendo kasi. Majeruhi wamelazwa Hospitali ya Igawilo. Dereva alikimbia mara baada ya tukio. Upeleleziunaendelea ikiwa ni pamoja na kumtafuta mtuhumiwa.

Mnamo tarehe 18.10.2016 majira ya saa 20:50 usiku huko katika Kijiji na kata ya Itope, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya, Gari lenye namba za usajili T.574 BNQ aina ya Toyota Coaster mali ya Kanisa la Uinjilisti Kiwira ikiendeshwa na dereva JAFARI SIMON [27] mkazi wa Tukuyu ilimgonga mpanda baiskeli aliyefahamika kwa jina la WEMA EDWIN [10] mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mbogola na kusababisha kifo chake papo hapo. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Dereva amekamatwa. Upelelezi unaendelea.


Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada zinaendelea kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha Mkoa wetu unakuwa mahala salama. Kumekuwa na tukio 01 la mauaji kama ifuatavyo:-

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JAMSON SANGA [42] fundi ujenzi, mkazi wa Nsalaga – Uyole alifariki dunia akiwa anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Awali mnamo tarehe 17.10.2016 majira ya saa 13:00 mchana marehemu akiwa njiani akirudi nyumbani kutoka shambani eneo la Mlimanyoka, kata ya Itewe, tarafa ya Tembela alivamiwa na watu wasiofahamika na kisha kumjeruhi kwa kumkatwa kwa kitu chenye ncha kali.

Marehemu alifariki tarehe 18.10.2016 majira ya saa 12:45 mchana.  Upelelezi unaendelea ili kuwabaini na kuwakamata waliohusika katika tukio hili.


WITO:

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa wito kwa madereva kuwa makini kwa kuzingatia na kufuata sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoepukika. Pia Kamanda KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za mtu/watu au kikundi cha watu wanaojihusisha na uuzaji na upikaji wa pombe haramu ya Moshi @ gongo ili wakamtwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.


                                                 Imesainiwa na:
[DHAHIRI A. KIDAVASHARI - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.