Tuesday, April 28, 2015
Sunday, April 26, 2015
Thursday, April 23, 2015
Wednesday, April 22, 2015
Tuesday, April 21, 2015
RATIBA ZA MICHEZO TANZANIA
2015-04-21
VPL
|
18:00
|
YANGA
|
Vs
|
STAND UNITED
|
U/Taifa
|
2015-04-22
VPL
|
16:00
|
SIMBA SC
|
Vs
|
MGAMBO JKT
|
U/Taifa
|
2015-04-24
VPL
|
16:00
|
RUVU SHOOTING
|
Vs
|
YANGA
|
U/Taifa
|
2015-04-25
VPL
|
16:00
|
MBEYA CITY
|
Vs
|
KAGERA SUGAR
|
Sokoine
|
VPL
|
16:00
|
SIMBA SC
|
Vs
|
NDANDA FC
|
U/Taifa
|
VPL
|
16:00
|
POLISI MORO
|
Vs
|
COASTAL UNION
|
Jamhuri
|
VPL
|
19:00
|
AZAM FC
|
Vs
|
STAND UNITED
|
Azam comp
|
2015-04-26
VPL
|
16:00
|
MTIBWA SUGAR
|
Vs
|
JKT RUVU
|
Manungu
|
VPL
|
16:00
|
T.PRISONS
|
Vs
|
MGAMBO JKT
|
Sokoine
|
2015-04-27
VPL
|
16:00
|
YANGA
|
Vs
|
POLISI MORO
|
U/Taifa
|
2015-05-02
VPL
|
16:00
|
NDANDA FC
|
Vs
|
KAGERA SUGAR
|
Nangwanda
|
VPL
|
16:00
|
T.PRISONS
|
Vs
|
MBEYA CITY
|
Sokoine
|
VPL
|
16:00
|
MGAMBO JKT
|
Vs
|
JKT RUVU
|
Mkwakwani
|
CAF conf
|
16:00
|
Etoile Du Sahel
|
Vs
|
YANGA
|
TUNISIA
|
2015-05-03
VPL
|
16:00
|
COASTAL UNION
|
Vs
|
STAND UNITED
|
Mkwakwani
|
VPL
|
16:00
|
SIMBA SC
|
Vs
|
AZAM FC
|
U/Taifa
|
VPL
|
16:00
|
MTIBWA SUGAR
|
Vs
|
RUVU SHOOTING
|
Manungu
|
2015-05-07
VPL
|
16:00
|
AZAM FC
|
Vs
|
YANGA
|
U/Taifa
|
2015-05-10
VPL
|
16:00
|
JKT RUVU
|
Vs
|
SIMBA SC
|
U/Taifa
|
VPL
|
16:00
|
MTIBWA SUGAR
|
Vs
|
COASTAL UNION
|
Manungu
|
VPL
|
16:00
|
STAND UNITED
|
Vs
|
RUVU SHOOTING
|
Kambarage
|
VPL
|
16:00
|
MBEYA CITY
|
Vs
|
POLISI MORO
|
Sokoine
|
VPL
|
16:00
|
KAGERA SUGAR
|
Vs
|
T.PRISONS
|
Kaitaba
|
VPL
|
16:00
|
NDANDA FC
|
Vs
|
YANGA
|
Nangwanda
|
VPL
|
16:00
|
AZAM FC
|
Vs
|
MGAMBO JKT
|
Azam comp
|
2015-05-17
COSAFA
|
16:00
|
LESOTHO
|
Vs
|
TANZANIA
|
South Africa
|
2015-05-19
COSAFA
|
16:00
|
TANZANIA
|
Vs
|
NAMIBIA
|
South Africa
|
2015-05-21
COSAFA
|
16:00
|
ZIMBABWE
|
Vs
|
TANZANIA
|
South Africa
|
2015-06-18
CHAN qulf
|
16:00
|
TANZANIA
|
Vs
|
UGANDA
|
U/Taifa
|
2015-09-11
Kirafiki
|
16:00
|
TANZANIA
|
Vs
|
BATA BULLETS
|
U/Azam comp
|
MBUNGE,MWENYEKITI CCM NUSURA WAZICHAPE KAVU KAVU MBELE YA WAZIRI
Waziri wa
Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(Kushoto) na Mbunge wa Mbarali Dickson Kilufi wakisaini vitabu vya wageni baada ya kuwasili Ubaruku kuwasikiliza wananchi juu ya mgogoro wa mpaka kati ya vijiji 21 na Tanapa.
Moja ya mabango yaliyoandikwa ujumbe na wananchi wahanga wa uhamisho
Waziri wa
Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu wakiwa na
Mwenyekiti wa CCM wilaya Mathayo Mwangomo baada ya kuhutubia wananchi.
Mwenyekiti wa CCM wilaya Mathayo Mwangomo baada ya kuhutubia wananchi.
HABARI KAMILI
KATIKA kuonesha hali si shwari ndani ya Chama Cha
Mapinduzi(CCM) wilayani Mbarali,mbunge wa jimbo hilo Mbarali Dickson Kilufi na Mwenyekiti
wa CCM wilaya Mathayo Mwangomo,hivi karibuni nusura wapigane Mbelea ya waziri wa
Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu.
Nyalandu aliwasili wilayani humo majira ya jioni
kwajili ya kufuatilia mgogoro wa kimpaka wa ardhi kati ya Tanapa na wakazi wa vijiji
vilivyopo jirani na hifadhi ya taifa ya Ruaha katika eneo la Ihefu.
Baada ya kufika wilayani hapa ilikiwa Nyalandu
akutane kwanza na wajumbe wa kamati ya Siasa ya wilaya ya Chama Cha Mapinduzi ili
kupata maoni yao kabla ya kukutana na uongozi wa serikali wilaya na kisha
wananchi katika kata ya Ubaruku.
Lakini kutokana na waziri kufika kwa kuchelewa
alilazimika kushauriana na viongozi wa chama kuahirisha vikao hivyo na badala
yake vifanyike kesho yake ili kutoa fursa kwa makundi yote kushirika katika
utatuzi wa mgogoro uliodumu kwa takribani miaka saba sasa.
Hata hivyo mbele ya kiongozi huyo,Mbunge Kirufi na
mwenyekiti wake wa Chama walishindwa kuficha utofauti walionao na badala yake
walianza kurushiana maneno makali(matusi) mbele yake huku kila mmoja akionesha
kuwa mbabe zaidi ya mwenzie.
Chanzo cha habari cha uhakika kilichokuwepo eneo la
tukio kilieleza kuwa viongozi hao waliendelea kurushiana matusi hadi pale
Nyalandu alipoamua kuingilia kati kuwasuluhisha na baadaye yeye kuamua kwenda
jijini Mbeya kupumzika kabla ya kurejea wilayani hapa kesho yake.
Uthibitisho wa tukio hilo ulibainika katika ukumbi
wa CCM wilaya,wakati Nyarando alipowataka wawili hao wapeane mkono kuashiria
hali ya jana yake imekwisha mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya huku
pia akiwasisitiza viongozi hao kuwa na umoja katika kupigania maslahi ya chama
na wananchi wanaowaongoza.
Hata hivyo Mbunge Kilufi katika kuonesha kuwa bifu
halijakwisha licha ya kukubali kupeana mikono ukumbini,alipopanda jukwaani
mbele ya wananchi wa kata ya Ubaruku alionesha kuendelea kuwa na kinyongo mbelea
ya baadhi ya viongozi wa CCM wilaya japok hakuwataja majina.
“Hata kama unamchukia Kilufi,endelea
kumchukia,lakini katika suala la mpaka kati ya Tanapa na wananchi naomba
tuungane kuwatetea watu wetu” yalikuwa maneno ya Kilufi jukwaani.
Baadhi ya wakazi wilayani hapa wanasema ugomvi baina
ya wawili hao unatokana na kuwa ufuasi katika makundi mawili tofauti ya watu
wanaowania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu ujao ambao mbunge anatajwa kuwa
katika kundi la waziri wa zamani Edward Lowasa.
Lakini wapo pia wanaosema mwenyekiti wa chama wilaya
amekuwa akipingana na mbunge huyo katika suala la mpaka kati ya Tanapa na
vijiji vya jirani kwa kile wanachoeleza kuwa amekula rushwa kutoka Tanapa
tuhuma alizozitaja pia mwenyekiti huyo alipozungumzia suala la mpaka akiwa
ukumbini.
“Mh.waziri suala hili la mpaka wengine hata
limetupaka matope,wapo wanaosema tumeingizwa mifukoni mwa Tanapa.Wanasema
Tanapa wametununua kwa kutupa fedha ili tusiwatetee wananchi.Tunaomba tulipatie
ufumbuzi ili mambo haya yasiendelee” alisema Mwangomo alipokuwa ukumbini.
Monday, April 20, 2015
MOTO WATEKETEZA MADUKA TUNDUMA
Wananchi wakijaribu kuokoa mali zilizopo katika maduka hayo.Picha na Saimen Mgalula |
Kikosi cha Zimamoto kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo kuuzima moto huo ambao umetekteza maduka zaidi ya Manne katika eneo hilo Mtaa wa Unyamwanga Kisimani mjini Tunduma. |
MOTO mkubwa umeteketeza
maduka zaidi ya Manne katika mtaa wa Unyamwanga Kisimani Mjini Tunduma
mkoani Mbeya April 19 mwaka huu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Mbeya Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa moto huo
ulitokea saa 2 usiku mtaa wa unyamwanga ambapo maduka hayo
yaliyoteketea yalikuwa katika jengo moja
linalomilikiwa Albart Ndembwike mkazi wa Tunduma .
Kamanda Msangi amesema moto huo ulitokea katika moja ya duka kati ya
hayo Manne yaliteketea kwa moto ambapo chanzo chake bado hakijafahamika mara
moja ambapo uchunguzi wa tukio bado unaendelea .
Amesema changamoto kubwa
iliyopo katika eneo hilo LA Mji wa Tunduma ni ukosefu wa gari la zima moto hivyo katika tukio la
jana walilazimika kuomba msaada kwa majirani zao Zambia ambao walifika mara
moja na kuuzima moto huo kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo.
Amesema changamoto hiyo
inatokana na wananchi wenyewe kufanya uhalibifu katika gari la zima moto
lililokuwepo katika mjini huo ambalo lilihalibiwa vibaya kwa kutupiwa mawe
kipindi nyuma ambalo kwa sasa lipo katika matengenezo.
Aidha jeshi la polisi
limelaani mtindo unaoota mizizi hivi sasa wa wananchi kujichukulia sheria
mkononi kwani kwa kufanya shambulio kwa kikosi cha zima moto mara kinapo wasili
katika eneo la tukio.
Amesema mashambulio ya aina
hiyo yamekuwa yakisababisha hasara ikiwa ni pamoja na kuvunjwa vioo vya gari,
kupotea kwa vitendea kazi pamoja na baadhi ya askari wa zimamoto kujeruhiwa
kitendo ambacho kinavunja moyo kwa askari hao.
Aidha mashuhuda wa tukio
hilo wanaeleza kuwa moto huo ulishika kasi kwa haraka kutokana na hali ya hewa
kuwa ya upepo mkali licha ya juhudi za wananchi kuuzima lakini uliwashinda
nguvui hadi pale kikosi cha zima moto kutoka nchini Zambia kilipo fika na
kuuzima moto huo.
Subscribe to:
Posts (Atom)