MKAZI
wa kijiji cha Ikukwa wilayani Chunya Wahama Wajoga anayekadiriwa kuwa na umri
wa kati ya miaka 85-90 amekutwa amefariki dunia porini alipokuwa akichimba
mizizi kwaajili ya dawa za kienyeji.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa kijiji cha Ikukwa, Josta Jiwili mwili wa Wajoga
anayedaiwa kuwa alikuwa mganga wa jadi ulikutwa kichakani juzi na pembeni
kukiwa na kipande cha nondo alichokuwa akitumia kuchimbia mizizi.
Mwenyekiti
huyo alisema inaonekana mpaka anakutwa na mauti tayari alikuwa amekwishachimba
baadhi ya m,izizi kwani ilikutwa katika begi dogo alilokuwa nalo.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema siku moja kabla ya kifo chake walikuwa pamoja na Wajoga wakinywa pombe za kienyeji,na kucheza
muziki katika kilabu cha wazenga,akiwa mzima wa afya njema hivyo kushangazwa na kifo chake.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema siku moja kabla ya kifo chake walikuwa pamoja na Wajoga wakinywa pombe za kienyeji,na kucheza
muziki katika kilabu cha wazenga,akiwa mzima wa afya njema hivyo kushangazwa na kifo chake.
Kwa upande wake ndugu wa marehemu walisema kifo hicho kimewashangaza sana kwani marehemu hakuwahi kusumbuliwa na tatizo lolote hadi mauti yanamkumba.
Nao Machifu wa kijiji cha Ikukwa walisema kuwa kifo hicho kinadhaniwa
kuhusishwa na imani za kishirikina kutokana na marehemu kujihusisha na kuagua wagonjwa wanaodhaniwa kulogwa.
Mmoja
wa machifu hao,Chifu Mwavamba alisema imekuwa ni
kawaida kwa waganga wa kienyeji kupimwa nguvu na watu wanaodhaniwa ni wachawi kwa kuwa inasadikika hawapendezwi na uwepo wa watu wanaotoa tiba kwa wanaologwa na wachawi.
kawaida kwa waganga wa kienyeji kupimwa nguvu na watu wanaodhaniwa ni wachawi kwa kuwa inasadikika hawapendezwi na uwepo wa watu wanaotoa tiba kwa wanaologwa na wachawi.
No comments:
Post a Comment