Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, June 28, 2023

 https://www.facebook.com/100001526491541/videos/163778579924492/

Wednesday, June 14, 2023

SINGIDA BIG STARS YAPIGWA MNADA

Na Lyamba Lya Mfipa
Uongozi wa klabu ya Singida Big Stars umefikia makubaliano ya kuiuza timu hiyo kwa wamiliki wa Fountain Gate.

Mtendaji Mkuu wa Singida Big Stars John Kadutu amesema hayo mkoani Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Amesema wameridhia kuiuza timu hiyo kwa fountain Gate, lakini kwa sharti la timu hiyo kubakia mkoani Singida.
Kwa upande wake Mmiliki mpya wa Timu hiyo Japhet Makau amesema, fursa hiyo imekuja katika wakati muafaka ndio maana wamemua kuichangamkia.
Kwa sasa jina la Singida Big Stars limebadilishwa na kuitwa Singida Fountain Gate Football Club.

MICHUANO TULIA TRUST BODABODA CUP 2023 YAZINDULIWA RASMI.

 
Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa akisalimiana na wachezaji wa timu za Madereva Bodaboda za Uyole na Stendi kuu kwenye uzinduzi wa Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge.

Na Joachim Nyambo, Mbeya.

 

MEYA wa jiji la Mbeya Dormohamed Issa amezindua rasmi michuano ya Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 yatakayoshirikisha timu nane kutoka kanda za madereva bodaboda zilizogawanywa kwenye makundi mawili ya A na B.

 

Michuano hiyo imerejea tena baada ya kusitishwa kwa misimu miwili mfululizo ambapo kwa mara ya kwanza yalifanyika 2019 lakini kwa miaka iliyofuata haikufanyika kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo mlipuko wa Covid-19

 

Kwa upande wa kundi A timu zinazoshiriki michuano hiyo ni za madereva bodaboda kutoka kanda za Iyunga, Stendi Kuu, Soweto na Kabwe wakati kundi B zipo timu za kanda za Mafiati, Sae, Uyole na Kadege.

 

Akizindua michuano hiyo katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge, Meya wa jiji la Mbeya Meya Issa ameipongeza Taasisi ya Tulia Trust inayoyaandaa akisema yana mchango mkubwa katika kuibua na kukuza vipaji vya vijana.

 

Amewasihi madereva bodaboda kutumia michuano hiyo situ kwa kuibua vipaji vyao bali pia kuimarisha afya zao hivyo kuwataka kuwa na nidhamu ya hali ya juu wakati wote yatakapokuwa yanaendelea.

 

“Mpira unaanza kucheza chini lakini haujui huko mbele utafika wapi…naamini kabisa kuna wachezaji miongoni mwenu mkionyesha nidhamu mkazingatia yale mnayofundishwa na walimu kuyafuata ipo siku mtafika mbali.”  

 

“Mpira ni nidhamu..na ukitaka kufanikisha katika jambo lolote weka nidhamu mbele..ukiamua kuwa padre weka nidhamu mbele, ukitaka kuwa shekh weka nidhamu mbele na hata ukitaka kuwa kiongozi wajali watu wako.” Amesisitiza Issa.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano ya Chama cha soka Mbeya mjini(Mufa), Ramadhan Nyambala amesema kutokana na ari ya mpira wa miguu katika mkoa wa Mbeya ni muhimu wadau wengi kuzidi kujitokeza kuandaa mashindano mbalimbali.

 

Amesema kuandaliwa kwa mashindano kama ya Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 ni sehemu ya mikakati muhimu na inayotarajiwa kwenye kuibua na kukuza vipaji vya vijana.

 

Afisa Habari na Mawasiliano wa Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema baada ya michuano hiyo kufanyika kwa mara ya kwanza 2019 iaka miwili mfululizo ilisimama kutokana na changamoto mbalimbali zilizoibuka ikiwemo cha mlipuko wa ugojwa wa corona.

 

Mwakanolo amesema michuano hiyo itakayokuwa ikifanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge na Magereza Mbeya yanatarajia kufikia tamati mwezi ujao huku akisema zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu zitatangazwa hivi karibuni.

Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa akisalimiana na waamuzi wa mchezo kati ya timu za Madereva Bodaboda za Uyole na Stendi kuu kwenye uzinduzi wa Tulia Trust Bodaboda Cup 2023 kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge.

Sunday, June 11, 2023

Tulia Trust Bodaboda Cup hatua ya makundi

Tunakutana jumatatu hii Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge Jijini Mbeya tukizindua msimu wa Pili ligi ya TULIA TRUST BODABODA CUP 2023.