Mwenyekiti wa bodi hiyo kaimu mkuu wa mkoa wa Mbeya
dk.Norman Sigalla alitangaza uamuzi huo leo hii (Juni 28) katika kikao
kilichowakutanisha wajumbe wa bodi na waandishi wa habari.
Dk.Sigalla amesema bodi imefikia maamuzi hayo baada
ya madaktari kushindwa kutimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kutofika katika
kikao walichoitwa na pia kutojibu barua walizopewa na kutakiwa kujibu ni kwa
nini wasiwajibishwe.
Amesema kutofika kazini kwa madaktari hao kwa siku
tano mfululizo walivunja mkataba wao kwa mujibu wa kanuni za kudumu za utumishi
wa umma toleo la mwaka 2009 kifungu namba F16,F 17 na F 27.
Amesema kwakuwa bodi ndiyo huingia mkataba na
madaktari hao,imechukua uamuzi wa kuvunja mikataba nao na kuwarejesha kwa
muajiri wao yaani waziri wa Afya na Ustawi wa jamii ili naye achukue hatua za
juu zaidi.
Amefafanua kuwa wameshatoa agizo la kuwataka madaktari hao
waliokuwa katika mafunzo kuondoka katika hosteli waliyokuwa wakiishi kwa
gharama za hospitali ya rufaa.
Lyamba Lya Mfipa imefika katika hosteli ya madaktari hao
saa tisa alasiri na kukuta wakiendelea
na harakati za kuhamisha mali zao kutoka katika hosteli hiyo na kuelekea
mitaani.
Wakati huo huo mwenyekiti wa shirikisho la vyama
huru vya wafanyakazi (TUCTA) Nicholaus Mgaya akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Mbeya amelaani namna inayotumiwa na madaktari kutafuta suluhu ya
madai yao.
Alisema yawezekana madai yao ni ya msingi lakini
walipaswa kutumia njia ya mazungumzo na hasa kup[itia chama cha wafanyakazi cha
TUGHE walicho wanachama na si chama cha kitaaluma wanachokitumia.