Miili 10 kati ya 13 ya marehemu
katika ajali iliyotokea jana(Juni 5) mlima wa Mzalendo nje kidogo ya jiji la
Mbeya ikihusisha lori lenye namba T 658 ASJ aina ya FAW lililokuwa na tela
lenye namba T 150 ASN lililoigonga Toyota coasta T886 BDZ imetambuliwa.
Taarifa kutoka jeshi la polisi mkoani Mbeya
kupitia ofisi za kikosi cha usalama barabarani leo zimeeleza kuwa marehemu
watatu bado hawajatambuliwa na kuendelea kutoa wito kwa wakazi mkoani humo
kuzidi kujitokeza katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya rufaa
kuitambua miili hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa
hiyo,waliotambuliwa ni wanawake Lucia Livingstone(51) mkazi wa katumba wilayani
Rungwe,Mwalumu mstaafu Ernesta Kikanga(62) mkazi wa Ifunda mkoani Iringa,Lena
Uzuri Ngomano(49) mkazi wa Isongole Rungwe na Bahati Japhari(33) mkazi wa
Kyela.
Upande wa wanaume wametambuliwa sita na
wote wakiwa wanatokea katika vitongoji vya jijini Mbeya ambao ni pamoja na
dereva wa coaster Mwasa Dimond(32) wa CCM Ilomba,Yerusalemu
Mwakyusa(35),Emanuel Mwanjanja wa Ilomba,Pius Mbeye wa Uyole,Mwase Piusi wa
Iganjo na Mwarine Focus wa Uyole.
Wakati huo huo muuguzi mkuu katika
hospitali ya Rufaa dokta Thomas Isdori amesema 13 kati ya majeruhi 20
waliofikishwa wameruhusiwa na kubaki majeruhi saba wanaoendelea vizuri kati yao
akiwemo mwanaume mmoja Fodi Mwakabunga(35) mkazi wa Kyela.
No comments:
Post a Comment