WANAUME
wanaofanyiwa unyanyasaji na wake zao ikiwemo kupigwa wamehimizwa kujiunga katika chama chao ili
kiweze kuwasaidia kupigania haki zao zilizo za nmsingi.
Afisa
kutoka kituo cha usimamizi wa sheria na haki za binadamu(LHRC) Reticia Petro
alitoa hamasa hiyo katika semina ya siku tatu ya mafunzo juu ya usimamizi wa
sheriaa na haki za binadamu iliyofanyika jijini Mbeya na kuhudhuriwa na
wasimamizi wa sheria katika mikoa mbalimbali nchini.
Reticia
amesema wapo wanaume wengi wanaofanyiwa unyanyasaji mkubwa na wa kutisha na
wake zao lakini kwa madai ya kuficha aibu hiyo wameendelea kutoeleza ukweli.
Amesema
miongoni mwa unyanyasaji wanaofanyiwa ni pamoja na kipigo cha mara kwa mara
ambacho wamekuwa wakikipata kutoka kwa wake zao na wao kulazimika kudanganya
hususani wanapoulizwa juu ya majeraha wanayoyapata.
No comments:
Post a Comment