Mkuu
wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewataka viongozi na wananchi wa wilaya Mpya ya
Momba kuhakikisha wanakuwa na mshikamano ili kuiwezesha wilaya yao kupata
maendeleo kwa haraka.MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO AKIPEWA SILAYA ZA JADI ZA WANYAMWANGA KABILA LA WAKAZI WA WILAYA MPYA YA MOMBA
Kandoro
ameyasema hayo katika sherehe za kuipongeza serikali kwa kukubali ombi la
kuanzishwa kwa wilaya ya Momba zilizoandaliwa na wananchi na kufanyika katika
kijiji cha Chitete yalipo makao makuu ya
wilaya hiyo.
Amesema
migongano na vitendo vya uvunjifu wa amani vinaweza kusababisha wilaya yao
kuchelewa kuyafikia maendeleo hatua ambayo itakuwa inatofautiana na malengo ya
serikali ya kuchukua maamuzi kuanzisha wilaya mpya.
Amewataka
maofisa na watendaji wa serikali wilayani hapo kuhakikisha wanazingatia
uadirifu katika utendaji kazi wao wakiogopa uonevu lakini pia wakizingatia
kutokuwa waoga.
Kwa
upande wake mkuu wa wilaya hiyo Abiud Saidea ameahidi kushirikiana kwa karibu
na watendaji pamoja na wananchi huku pia akiiomba serikali ya mkoa kuhakikisha
inakuwa karibu na kuipa upendeleo wilaya yake katika mipango mbalimbali ya
kimaendeleo iliyopo.
No comments:
Post a Comment