WATENDAJI wa idara ya Biashara na Masoko katika
halmashauri ya jiji la Mbeya wamepewa muda wa wiki moja kuhakikisha ujenzi wa
vyoo katika soko la Sokoine jijini hapo lunakamilika.
MEYA KAPUNGA (KUSHOTO)AKIFINGIANA NA MWEKA HAZINA WA JIJI
Agizo hilo limetolewa na Meya wa jiji hilo Athanas Kapunga wakati akikabidhi vifaa
kwaajili ya ujenzi wa vyoo 12 vyenye thamani ya shilingi 500,776 vilivyotolewa
na kampuni ya Marumaru ya jijini hapa.
Kapunga alisema alilazimika
kutafuta msaada huo kufuatia wafanyabiashara katika soko hilo kulalamikia hali ya ukosefu wa vyoo na
kutishia kutoendelea kulipa ushuru iwapo hawatojengewa vyoo.
“Mnamo Juni 11
mwaka huu wafanyabiashara hawa ambao awali walikuwa katika soko la Uhindini
lililoungua waliiandikia halmashauri kuwa tangu wahamie Sokoine hakuna
vyoo.Wakasema hatuwezi kuendelea kulipa ushuru wakati hakuna vyoo.Tukaona madai
yao ni ya kweli”.
Alisema baada ya
kupokea barua hiyo alifanya ziara kutembelea soko hilo akiwa ameambatana na watendaji wa
halmashauri na ndipo walipofikia uamuzi wa kuchukua baadhi ya vibanda vya
maduka vilivyokuwa havijakamilika ili kuvitumia kwa ujenzi wa vyoo.
Alisema vibanda
vitatu vilivyokuwa vinajengwa kwaajili ya maduka vimechukuliwa na halmashauri
na wamiliki watalipwa fidia kwaajili ya ujenzi wa vyoo hivyo.
Hata hivyo alisema
kwakuwa ilikuwa mwishoni mwa mwaka wa fedha ilikuwa vigumu kwa halmashauri
kupata fedha mara moja na ndipo ikalmazimu kutembeza bakuli kwa wadau
mbalimbali na ndipo kampuni ya Marumaru ikatoa msaada huo.
Alisema tayari
amezungumza na mkurugenzi akamuhakikishia kuwa ametenga shilingi milioni kumi
kwaajili ya ujenzi wa vyoo hivyo hivyo kinachotakiwa ni kuwalipa wahusika fidia
na kuanza ujenzi mara moja.
Alisema mpaka
ijumaa ya wiki ijayo ujenzi wa vyoo hivyo unapaswa uwe umekamilika na kuanza
kutumika kwakuwa afya ni jambo la msingi kwanza kuliko hata kukusanya ushuru.
No comments:
Post a Comment