Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, June 5, 2012

AJALI YAUA KUMI,19 WAJERUHIWA VIBAYA

WATU kumi wamefariki dunia na wengine 19 kujeruhiwa vibaya kufuatia ajali mbaya iliyotokea jijini Mbeya ikihusisha gari ya abiria aina ya Coasta na Lori zilizogongana uso kwa uso.
Ajali hiyo imetokea leo(Juni 5) majira ya saa 6:30 eneo la mlima Mzalendo Igawilo nje kidogo ya jiji la Mbeya ambapo Coasta yenye namba  T 188 AWE iliyokuwa imejaza abiria ikitokea jijini kuelekea wilayani Kyela liligongana na Lori lenye namba T 658 ASJ Scania lililokuwa na tela lenye namba T 150 ASN likitokea Malawi.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema chanzo cha ajali hiyo ni kufeli kwa breki za Scania iliyokuwa ikishuka mlima mkali na maarufu kwa ajali kutokana na kuwa na kona nyingi na ndipo likaivaa coasta na kusababisha majonzo hayo.

Kwa mujibu wa maafisa wa jeshi la polisi waliozungumzia tukio hilo baada ya kuteremsha miili ya watu waliokufa katika ajali hiyo na kuiingiza katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya rufaa Mbeya watu waliokufa ni 10 na 19 walijeruhiwa.

Maofisa hao wameoomba kutotajwa majina kutokana na kutokuwa wasemaji wa jeshi la polisi walisema waliokufa eneo la tukio ni tisa na mmoja alifia katika hospitali ya rufaa wakati akiendelea kupata matibabu pamoja na majeruhi wengine.

Wamesema kati ya waliokufa wapo wanaume saba akiwemo dereva aliyefahamika kwa jina la Mwasa Diamond(32) mkazi wa eneo la CCM Ilomba jijini Mbeya huku aliyefia hospitali akifahamika kwa jina la Titus Mbeye pamoja nao wanawake watatu akiwemo mmoja aliyetajwa kuwa mjamzito lakini wote hawakufahamika majina wala makazi yao.

Harakati za kumtafuta kamanda wa polisi mkoani hapa Athuman Diwani zimegonga mwamba baada kutopatikana ofisini na hata alipopigiwa simu yake ya kiganjani yenye namba 0787323444 haikupokelewa. 

No comments:

Post a Comment