Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, June 17, 2012

WATOTO WALEMAVU WAIOMBA SERIKALI

SERIKALI mkoani Mbeya imeombwa kulijengea uwezo Baraza la watoto walio na Ulemavu ili liweze kufanya kazi zake za kuwatetea watoto hao kama ilivyotarajiwa wakati wa kuanzishwa kwake.WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI CHITETE WILAYANI MOMBA MKOANI MBEYA WAKIIMBA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KIMKOA

Ombi hilo limetolewa katika risala ya baraza hilo iliyosomwa na mtoto Daria Njovu mwanafunzi wa shule ya msingi Mwenge ya wilayani Mbozi kwenye maadhimisho ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Chitete wilayani Momba.BAADHI YA WAKAZI WA WILAYA YA MOMBA WALIOFIKA KATIKA MAADHIMISHO YA MTOTO WA AFRIKA
Daria amesema baraza hilo linakabiliwa na changamoto nyingi hali inayolazimu kuomba msaada wa serikali na wadau wengine katika kulijengea uwezo ili litimize kazi zake.

Amezitaja changamoto zinazoendelea kuwakabili watoto walio na ulemavu kuwa ni pamoja na ukosefu wa matibabu,elimu duni kwa jamii juu ya walemavu na pia walemavu kusoma katika shule za mchanganyiko na watoto wa kawaida.

Wameiomba pia serikali ya mkoa kuanzisha shule za sekondari maalumu kwaajili ya walemavu ili kuwawezesha watoto wanaohitimu elimu ya msingi na kufaulu waweze kujiunga na shule hizo na kuendelea na masomo ya elimu ya juu kama ilivyo kwa enzao wasio na ulemavu.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amesema kuwaweka watoto walio na walemau katika shule za mchanganyiko na wasio na ulemavu kunalenga kuondoa dhana ya kuwatenga walemavu.

No comments:

Post a Comment