JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.
Ofisi ya Kamanda wa Polisi,
Mkoa
wa Mbeya,
Namba ya simu 2502572
S. L. P. 260,
Fax - +255252503734
MBEYA.
E-mail:- rpc.mbeya@tpf.go.tz
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 15.08.2016.
Jeshi la Polisi mkoa
wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika
maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana
na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na
wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio
makubwa ya uhalifu na kumakata mali mbalimbali kama ifuatavyo :-
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mbeya mnamo tarehe 07.08.2016 hadi tarehe 13.08.2016
lilifanya misako mbalimbali katika maeneo ya Jiji la Mbeya. Misako hiyo
ilifanyika maeneo ya Uyole, Isyesye, Ituha, Iyela, Airport, Kalobe, Nzovwe,
Simike, Forest Mpya na Mwanjelwa. Katika Misako hiyo iliyolenga kukomesha
vitendo vya wizi na uvunjaji nyumba wakati wa usiku na mchana, mali na vitu mbalimbali vya wizi
vilipatikana pamoja na watuhumiwa 10 kukamatwa kuhusika katika matukio hayo.
Mafanikio yaliyopatikana katika misako:
KUPATIKANA NA RISASI 10 ZA SMG
Mnamo
tarehe 14.08.2016 majira ya saa 14:00 mchana huko maeneo ya Sae Jijini Mbeya,
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JOHAN
MWASUMBWI (32) Mfanyabiashara na Mkazi wa Sae alikamatwa akiwa na risasi 10
za silaha aina ya SMG kinyume cha sheria.
KUPATIKANA NA SARE ZA JESHI [JWTZ]
Mnamo
tarehe 14.08.2016 majira ya saa 14:00 mchana huko maeneo ya Sae Jijini Mbeya,
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JOHAN
MWASUMBWI (32) Mfanyabiashara na Mkazi wa Sae alikamatwa akiwa amevaa sare
za JWTZ aina ya Kombati [Shati na Suruali].
Mtuhumiwa
atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.
Kupatikana kwa Gari moja na Bajaji: Katika misako hiyo Bajaji nne zilipatikana zenye namba
za usajili MC 999 AKQ, MC 250 ARG, MC 274 AAK na moja iliyokuwa na namba 28 ubavuni pamoja na gari moja yenye namba ya usajili
T.501 CAB aina ya Toyota Noah rangi nyeupe.
Kupatikana kwa Mali za Wizi: Katika misako hiyo, mali na vitu mbalimbali vya wizi
vilipatikana ambavyo ni:-
1.
Vyerehani vitatu
moja aina ya Butterfly,
2.
Amplifier moja,
3.
Spika tatu kubwa,
4.
Laptop aina ya
Samsung,
5.
Laptop aina ya HP
G.56,
6.
Laptop aina ya HP
693,
7.
Redio aina ya
Panasonic,
8.
Television Flat
Screen aina ya Boss inchi 32,
9.
Monitor aina ya
HP,
10. Mashine ya Kudarizi ya Umeme,
11. Viti vitatu vya Plastic,
12. Keyboard aina ya ACER na Mouse,
13. Deki aina ya Samsung,
14. Subwoofer moja aina ya Piano,
15. Computer isiyokuwa na jina,
Vitu
vingine vilivyopatikana ni pamoja na Simu 10 za aina mbalimbali ikiwemo Tecno,
Samsung na Itel, Chaja ya simu ya Smartphone, Earphone 08, Betri za simu 07,
Makava ya simu, Flash Disk 03, Katoni za Soda 10, Kreti za bia tupu 06, Kreti
za soda 08 na bidhaa mbalimbali za dukani ambazo ni mafuta ya kula, mafuta ya
kujipaka mwilini, biskuti, juice, sabuni za unga.
Kukamatwa Watuhumiwa 10 wa Uhalifu: Aidha katika misako hiyo watuhumiwa 10 walikamatwa
kuhusika katika matukio ya kupatikana na mali za wizi na kuvunja nyumba usiku
na kuiba ambapo majalada ya uchunguzi yalifunguliwa. Watuhumiwa hao ni pamoja
na
1. STEPHANO NAZMA (24) Mkulima na Mkazi wa Ituha
2. REGINA BENEDICT (16) Mkulima na Mkazi wa Kalobe
3. SHABANI DAFA (21) Dereva na Mkazi wa Airport
4. GODFREY NDUKWA (22) Mfanyabiashara na Mkazi wa Airport
5. JAMES ENOCK (20) Mkulima na Mkazi wa Airport.
Watuhumiwa
wengine waliokamatwa ni
6. FIDELIS NGOVANO (32) Mkulima na Mkazi wa Wilaya ya Mbarali
7. ISRAEL LIYAUMI (33) Mkulima na Mkazi wa Madibila Wilayani Mbarali 8. ZEBEDAYO KADUMA (35) Mkulima na
Mkazi wa Uyole
9. RIZIKI ALFEO (17) Mkulima na Mkazi wa Ubaruku Wilayani Mbarali na 10. JOSHUA DAUDI (26) Mkulima na Mkazi
wa Ubaruku Wilayani Mbarali.
Aidha
katika zoezi hilo la Misako lilienda sambamba na ukaguzi wa nyumba za kulala
wageni zilizopo katika maeneo ya Uyole, Isyesye, Ituha, Iyela, Airport ya
Zamani, Kalobe, Nzovwe, Simike, Forest Mpya na Mwanjelwa. Hali kadhalika
wamiliki na wahudumu katika Nyumba hizo za kulala wageni walipewa elimu ikiwa
ni pamoja na kuandika majina ya wageni wote katika kitabu cha wageni pamoja na
kuweka namba za wahudumu, wamiliki na viongozi wa Jeshi la Polisi kwenye
milango kwa ajili ya dharura zitakazojitokeza kwa hatua zaidi.
WITO:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishna wa
Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa
wito kwa jamii hasa vijana kuacha tabia ya kutaka kupata mali au utajiri kwa
njia ya mkato na badala yake wafanye kazi halali ili wapate kipato halali. Pia
anasisitiza kuwa maendeleo hayapatikani kwa kufanya kazi hama biashara haramu,
watumie fursa zilizopo Mkoa wa Mbeya kujitafutia ajira.
Imesainiwa na
[DHAHIRI A.
KIDAVASHARI - DCP]
KAMANDA
WA POLISI MKOA WA MBEYA.