Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, November 30, 2016

MRISHO NGASA ATUA RASMI MBEYA CITY


Picha inayo-trend kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii ni ya Mrisho Ngasa na afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ambayo inaashiria tayari nyota huyo wa zamani wa Yanga ameshakamilisha deal na ‘wagonga nyundo wa Mbeya’ Mbeya City.

Mwezi Septemba mwaka huu Ngasa alijiunga na Fanja FC inayoshiriki ligi kuu nchini Oman (Oman Professional League) ikiwa ni wiki tatu tu, baada ya kuvunja mkataba na klabu ya Free State Stars ya South Africa.

Nyota huyo wa zamani wa vilabu vya Kagera Sugar, Yanga, Azam FC na Simba vyote vya VPL hajadumu Oman na hatimaye amerejea tena nchini na kusajiliwa na klabu ya Mbeya City ambapo ataungana na kocha wake wa zamani Kinna Phiri aliyemsajili kutoka Yanga kwenda Free State Stars kabla ya kocha huyo kutimuliwa kufatia mfululizo wa matokeo mabovu.

Afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ame-post picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa pamoja na Mrisho Ngasa na kuandika maneno yanosomeka: “Mnapokamilisha jambo kutakiana heri ndio uungwana.





POLISI SONGWE WAPEWA MSAADA WA PIKIPIKI

Chifu wa Usafirishaji na Lojistiki,Naibu Kamishina wa Polisi Shabani Mrai Hiki na Meneja mkuu wa kampuni ya Bima ya Maisha ya Sanlam nchini Wilson Mnzava wakikata utepe kama ishara ya kukabidhiana pikipiki nne zilizotolewa na kampuni hiyo kwaajili ya Jeshi la polisi mkoani Songwe.

 Meneja mkuu wa kampuni ya Bima ya Maisha ya Sanlam nchini Wilson Mnzava akizungumza jambo kabla ya kukabidhi pikipiki nne zenye thamani ya shilingi milioni 10.
 Kamanda wa Polisi mkoani Songwe Mathias Nyange akie;lezea uhaba wa vitendea kazi unaolikabili jeshi la polisi mkoani Songwe.
 Chifu wa Usafirishaji na Lojistiki,Naibu Kamishina wa Polisi Shabani Mrai Hiki na Meneja mkuu wa kampuni ya Bima ya Maisha ya Sanlam nchini Wilson Mnzava wakikabidhiana pikipiki nne zilizotolewa na kampuni hiyo kwaajili ya Jeshi la polisi mkoani Songwe.








Tuesday, November 29, 2016

ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA NA VIONGOZI WA DINI KATIKA UWANJA WA SIA

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla (kulia) akiwa ameambatana na wajumbe wa Kamati ya ulinzi na Usalama mkoa na viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu mkoani Mbeya wakikagua Miundombinu ya Uwanja wa Ndegea wa Kimataifa wa Songwe(SIA).Lengo la ziara hii iliyofanyika jana ni kuwezesha wananchi kutambua jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuboresha Sekta ya Usafiri nchini

 Mkuu wa Usalama katika uwanja wa SIA Ole Laput akitoaa maelekezo juu ya masuala ya usalam uwanjani SIA
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla akifafanua jambo kwa wajumbe alioongozanaa nao kwenye ziara ya kukagua uwanja wa SIA


 Mhariri Mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw. Joachim Nyambo akikagua taa za kuongozea ndege wakati wa mchana kunapokuwa na ukungu.
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla na wajumbe wengine wakisikiliza maelezo ya Uongozaji ndege kutoka kwa mhandisi Samweli Murembe aliyekuwa zamu kwenye Chumba cha kuongozea ndege
Juu ni Viongozi wa dini na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Mbeya wakiangalia namna tukio la uzimaji moto linavyofanyika iwapo kutatokea ajali ya ndege kuwaka moto ikiwa uwanjani.Chini ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla akishirikiana na viongozi wa dini kuuombea uwanja wa SIA


                              HABARI KAMILI

WAKAZI mkoani Mbeya wamehamasishwa kujiandaa na ujio wa Ndege za Kampuni ya ATC zinazotarajiwa kuanza safari za Dar es salaam na Mbeya kuanzia DDesemba 2 mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla ametoa hamasa hiyo alipofanya ziara na viongozi wa dini mkoani hapa kutembelea Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe(SIA) lengo likiwa ni kujinea jitihada zinazofanywa na Serikali za kuukamilisha uwanja huo.

Makalla amesema taarifa zilizothibitishwa kuwa ndege za ATC zitakuwa zikifanya safari kwa siku tano kwa juma ambapo  siku hizo ni Jumatatu,jumatano,ijumaa,jumamosi na jumapili.

Amesema ndege ndege itakuwa ikitoka Dar es salaam saa sita mchana na kufika Mbeya saa nane na kisha saa nane na nusu kuanza safari ya kurudi Dar es salaam.

Amesema kutokana na fursa hiyo wakazi wa mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani wanapaswa kujipanga kuhakikisha wanakuwa wanufaika wa kwanza kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi wanazoweza kuzifanya kupitia fursa hiyo

Aidha mkuu huyo wa mkoa pia amesisitiza adhma ya mkoa wa Mbeya kunufaika na uwanja wa SIA kwa wawekezaji kuzalisha na kusafirisha maua,matunda na mbogamboga kwenda nje ya nchi mara ndege za kimataifa zitakapoanza kutua kwenye uwanja huo.

Amewataja  viongozi wa dini kuwa moja ya kundi muhimu linaloweza kuwahamasisha wananchi kuutumia uwanja huo kwa manufaa huku akiwasisitiza pia kutumia nafasi walizonazo kuhubiri amani ili uwanja huo uweze kuwa katika hali ya usalama wakati wote.

Kwa upande wao viongozi wa Dini walioshiriki ziara hiyo,wameipongeza serikali kwa jitihada zake za ujenzi wa uwanja wa SIA hususani hatua ya kufunga Taa za kuongozea ndege wakati wa Ukungu wakisema zitasaidia kwa kiasi kikubwa safari za ndege kuwa za uhakika.


Wameisihi serikali kuendelea kushughulikia changamoto ya kufunga taa za kuongozea ndege wakati wa usiku ili kuwezesha ndege kuanza kufanya safari zake wakati wote wakisema itawezesha uwanja huo kutumika kwa tija zaidi.

ZIARA YA WAZIRI WA ELIMU.SAYANSI NA TEKNOLOJIA BUSOKELO

 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Joyce Ndalichako akikagua daftari za wanafunzi wa darasa la Pili katika shule ya Msingi Malema iliyopo katika Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe.Nyuma yake ni Mwalimu mkuu wa shule hiyo Francisca Kalewa
 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Joyce Ndalichako akishiriki kucheza na wanafunzi wa shule ya msingi Malema iliyopo katika halmashauri ya Busokeo wilayani Rungwe.
 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Joyce Ndalichako akisalimiana na viongozi na wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Busokelo
 Wakazi wa kijiji cha Malema kilichopo katika Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe wakimsikiliza Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Joyce Ndalichako(hayupo pichani) allipofanya mkutano wa hadhara kijijini hapo baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya elimu wilayani hapo

Tuesday, November 8, 2016

MWANAHABARI GORDON KALULUNGA ALIVYOHOJIWA NA POLISI KWA SAA TANO

Na Joachim Nyambo,Mbeya.

MWANDISHI wa habari wa gazeti la Mtanzania,Gordon Kalulunga Oktoba 24 mwaka huu aliwekwa kizuizini na kuhojiwa kwa muda wa masaa manne katika kituo cha Polisi cha Mbalizi yalipo makao makuu ya Wilaya maalumu ya kipolisi Mbeya vijijini.

Mwandishi wa habari hizi aliyeambatana na Kalulunga walifika kituoni hapo majira ya Saa nane na Nusu mchana ambapo awali majira ya saa tano asubuhi,afisa mmoja wa jeshi la polisi alimpigia simu mwanahabari huyo akimtaka afike kituoni hapo kwaajili ya kuhojiwa.

Kwa mujibu wa Kalulunga wakati akipigiwa simu licha ya kuhoji kulikuwa na tatizo gani hata aitwe kituoni,afisa aliyempigia simu hakumweleza kuna nini na badala yake akamweleza ni masuala ya kiofisi yasiyoweza kuzungumzwa kupitia simu.

“Baada ya kupigiwa simu niliona kabla ya kwenda ni vema niwajulishe ndugu,jamaa na rafiki zangu wakiwemo wanahabari.Ndiyo sababu nimewaiteni ili ikiwezekana kwa walio na nafasi niongozane nao wakajue kuna nini”alisema Kalulunga baada ya kukutana na mwandishi wa habari hizi kabla ya kuelekea kituoni.

Zipo tetesi kutoka ndani ya jeshi hilo kuwa awali maafisa wawili waliagizwa kumtafuta Kalulunga popote alipo ili akamatwe na kufikishwa kituoni hapo lakini mmoja wa askari walioagizwa alishauri mwanahabari huyo aitwe kwani hawezi kukaidi kufika.

Mara baada ya kuwasili kituoni hapo,Kalulunga aliitwa katika chumba cha Ofisi za Upelelezi wa makosa ya jinai huku akiruhusiwa kuingia na mtu mwingine mmoja ambaye ni mtu wake wa karibu ili asikilize mahojiano hayo.

Kikao cha mahojiano kianza saa nane mchana na kumalizika saa 12 jioni,ambapo mara baada ya kutoka Kalulunga alisema amekumbana na tuhuma za kesi tatu miongoni mwa kesi hizo ikiwa ni kwa nini hivi karibuni aliandika habari iliyoonesha mapungufu ya jeshi la polisi.

“Wamenihoji kuhusua habari ya tukio la mtoto aliyesadikika kuzikwa ndani ya nyumba.Baadhi ya maswali ni pamoja na kwa nini niliandika kuwa polisi waliogopa kuingia ndani ya nyumba hiyo”

“Suala la pili wamehoji ni kwa nini kupitia mtandao wa kijamii wa Mbalizi Forum tuliweka mjadala wa risiti bandia za faini zinazotolewa na baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani wanapowakamata madereva wenye makosa”

Alisema kadhalika kesi ya tatu ilihusu Mbalizi Forum kuruhusu mjadala wa uwepo wa baadhi ya askari wanaoendekeza kupokea rushwa hususani wa kitengo cha usalama barabarani huku pia wakimlaumu ni kwa nini kupitia mtandao huo yanayojadiliwa ni mabaya tu yanayofanywa na jeshi la polisi lakini mazuri hayatajwi.

Alisema mara baada ya mahojiano alichoambiwa na afisa aliyekuwa akimhoji ni kuwa jalada hilo litafikishwa juu hivyo binafsi hakujua ni kupelekwa mahakamani au ala.


POLISI WAWILI WATIMULIWA KAZI MBEYA

JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limewafukuza kazi askari wake wawili kutokana na askari hao kuwafanyia Vitendo vinavyokwenda kinyume cha maadili wanafunzi wa kike wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Sekondari Isuto iliyopo Kijiji na Kata ya Isuto, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi Dhahiri Kidavashari amewataja askari waliofukuzwa kazi kuwa ni H.4925 PC Petro Oscar Magana wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Mbeya na J.1422 PC Lucas Joseph Ng’weina wa Wilaya ya Kipolisi Mbalizi.

Kamanda Kidavashali amesema leo kuwa mnamo Novemba 4 mwaka huu majira ya saa 5:30 Usiku huko katika Shule ya Sekondari Isuto iliyopo Kijiji na Kata ya Isuto, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya, askari hao wawili wawili wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya walituhumiwa kuwafanyia vitendo vibaya kinyume na maadili wanafunzi wa kike wa kidato cha nne wa Shule hiyo wanaoendelea na mtihani wa Taifa.

Amesema kuwa, askari hao kwa pamoja wakiwa kwenye ulinzi wa mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne 2016 waliwatoa kwenye Hostel wanafunzi wa kike kwa kile walichodai kupiga kelele.

Amesema baada ya kuwatoa wanafunzi hao, waliwapeleka eneo la kufoleni na kuanza kuwapa adhabu mbalimbali ambazo ni kupiga push up, kuruka kichura, kushika masikio na kuwachapa viboko sehemu za makalio vitendo vilivyowasababishia maumivu makali na kupelekea baadhi ya wanafunzi hao wa kike kuondoka na kurudi majumbani kwao”.

Amesema Kufuatia vitendo hivyo, Mkuu wa Shule hiyo,Rose Dihembe alitoa taarifa kwa uongozi wa Wilaya ambapo taarifa zilifika kwa uongozi wa Mkoa ambao mara moja walifika eneo la tukio na kuchukua hatua za awali ikiwemo kusikiliza malalamikio hayo ya tukio na kuwaondoa askari waliolalamikiwa na mwisho kuchukua hatua za kinidhamu zilizopelekea kufukuzwa kazi askari hao.

Hata hivyo kamanda Kidavashari amesema kutokana na vitendo walivyovifanya askari hao jeshi la polisi linatarajia kuwafikisha mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Kamanda huyo, ametoa wito kwa wananchi mkoani hapa kuendelea kuliamini Jeshi la Polisi na kwamba halitafumbia macho vitendo vya askari vinavyokwenda kinyume na maadili ya kazi yao na pia kinyume na sheria za nchi.

Aidha Kamanda Kidavashari ameomba wananchi kuendelea kutoa taarifa ya vitendo vyote vya uhalifu vinavyotendwa bila kujali vinatendwa na askari au wananchi wa kawaida ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa.