Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, May 21, 2016

ZIARA YA WANACHAMA WA TAJATI,SUPRISE BEACH MJINI MAKAMBAKO

 Wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) wakipiga picha ya pamoja na mkurugenzi wa kampuni ya Star Entergrated inayomiliki Suprise Beach Bw.Patrick Kyando (aliyeshika kitabu)kabla ya kuanza kutembelea vivutio mbalimbali ndani ya eneo lake.
 Baadhi ya wanachama wa TAJATI wakiwa wamepanda mkokoteni unaokokotwa na Punda kuelekea Suprise Beach.

Mwenyekiti wa TAJATI,Bw.Ulimboka Mwakilili akiwa amepanda Farasi njiani kuelekea Suprise Beach.


 Hapa ni langoni pa Suprise Beach.Ukifika hapa lazima utavutiwa kupiga picha kwaajili ya ukumbusho kama ilivyotokea kwa wanatajati hawa.
 Mwenyeji akitoa maelezo katika eneo ambalo hutumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo sherehe za Harusi.
 Kwa mbaali kulia ni mfano wa Mlima Kilimanjaro na kushoto ni mfano wa boti.Hapa unaweza kujifunza kupanda mlima na pia kupanda boti.


 Wanatajati wakiwa wamepozi katika eneo lililopewa jina la Mwanza.Kimsingi linavutia na unaweza kujihisi kweli umefika jijini Mwanza kutokana na mandari yanayofanana.








 Mwanahabari kutoka TV 1 Laudence Simkonda akipiga kasia alipoamua kucheza na Mtumbwi kabla ya kupata ajali kama inavyoonekana hapo chini.

 Wanatajati wakivuka kutoka eneo la Kigamboni kwenda kisiwani Zanzibar(Haya ni majina tu yaliyowekwa hapa)

 Mwanahabari Felix Mwakyembe(aliyekaa) alikuwa mmoja kati ya wanatajati ambao hawakutaka kuondoka ndani ya eneo hili la kuvutia na la starehe za kipekee.
 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany)akionesha umahiri wa kusafiri ndani ya maji kwa kutumia Mtumbwi.

 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany)akicheza na nyani mdogo aina ya ngedere aliyepewa jina la King.


 Mwanahabari Laudence Simkonda akiwa ametumbukia kwenye maji baada ya mtumbwi wake kupinduka.Hata hivyo kutokana na uzoefu wake aliweza kujiokoa mwenyewe pasipo hata kuhitaji msaada wa mtu mwingine.

 Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Daniel Nyambo(Jodany) akiendelea na kazi ya kupiga picha za matukio mbalimbali wakati wa ziara hiyo.

No comments:

Post a Comment