Tuesday, October 11, 2011
Monday, October 10, 2011
Kandiro-Jiulizeni mpo kufanya nini
MKUU WA mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewataka
madiwani na watendaji katika halmashauri za wilaya kila mmoja kujiuliza yupo
katika nafasi yake kwaajili ipi.
Kandoro amesema kwa kufanya hivyo kila mmoja alipo
ataweza kutambua wajibu wake na kuhakikisha anautekeleza akilenga kuyabadili
maisha ya wananchi waliomwajiri.
Mkuu huyo wa mkoa,aliyasema hayo juzi(Oktoba 10)
katika kikao maalumu cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ileje
kilicholenga kujadili taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa serikali CAG.
Alisema wapo baadhi ya madiwani na watendaji ambao
wamekuwa wakiyasahau majukumu yao na kujikuta wanaendekeza siasa katika kila
wanalofanya pasipo kutambua kuwa kufanya hivyo kunawacheleweshea maendeleo wananchi
katika maeneo yao.
Aliwataka madiwani kuhakikisha wanakuwa na
mshikamano katika kutafuta sukluhu za changamoto zinazowakabili wananchi badala
ya kuendeleza makundi yaliyotokana na kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Kandoro alisema ushirikiano wa pamoja baina ya wadau
hao kwa kushirikiana na wananchi ndio unaoweza kuongeza kipato cha mwananchi
mmojammoja ambaye kwa mafanikio hayo ataweza kuuchangia uchumi wa wilaya hiyo
na kuiondoa katika hali ya utegemezi wa asilimia 98 ya bajeti yake kutoka
serikali kuu.
Alisema ni vema wadau hao wakaona aibu kwa
halmashauri yao kuwa na uwezo wa kujitegemea kwa asilimia mbili pekee wakati
ambao mkakati wa serikali ni kuona halmashauri zinajitegemea kwa asilimia 50.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri
hiyo Glads Dyamvunye alisema ukosefu wa vyanzo vya mapato ni changamoto kubwa
kwa halmashauri yake hali inayopelekea kuendelea kuwa tegemezi kwa serikali kuu.
Sunday, October 9, 2011
Kijiji kunufaika na uwekezaji
SERIKALI ya kijiji cha Luhanga wilaayani Mbarali
imesisitiza kuwa uwekezaji wa kilimo unaolengwa kufanywa na Umoja wa wakulima wa
Luhanga unalenga kuwanufaisha wakazi wa kijiji hicho na haupo kwa maslahi ya
watu binafsi.
Uongozi wa kijiji hicho umesema makubaliano ya
mkataba na umoja huo ni pamoja na umoja kutekeleza mambo makuu matatu ikiwemo
kujenga ofisi ya kisasa ya kijiji,kuleta maji kijijini hapo kwaajili ya
matumizi ya kilimo pamoja na kulipia ardhi waliyopewa kwaajili ya shughuli zao.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Muhamed Msonsa alisema
jana kuwa umoja huo utapaswa kulipa shilingi 5000 kwa kila hekari moja ya eneo
walilopewa na kijiji hivyo kijiji kila mwaka kitakuwa kikikusanya jumla ya
shilingi milioni 62 kwa hekari 5000 zilizotolewa.
Kwa upande wa afisa mtendaji wa kata ya Luhanga
Aloyce Joseph alisema wapo wanasiasa wanaoonekana kuingilia kati uwekezaji huo
na kuwalaghai wananchi kuwa kilichofanyika ni unyang’anyi wa ardhi hali ambayo
imeonekana kuwagawa wanakijiji katika makundi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya
ya Mbarali George Kagomba alisema uwekezaji wa Umoja huo utakinufaisha kijiji
kwani kabla hata ya kuanza kwa shughuli husuika tayari umoja huo umeonesha nia
kwa kuanza kuwasaidia wanakijiji kutatua changamoto mbalimbali.
Saturday, October 8, 2011
Mbunge Mbaroni
MBUNGE wa Mbarari Modestus Dickson Kilufi aliyekuwa
anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kutishia kuua atafikishwa mahakamani kesho
jumatatu(Oktoba 10) na kwa sasa yupo nje kwa dhamana.
Mbunge Kilufi alikamatwa juzi(Oktoba 7) saa 10 jioni
akiwa ofisini kwake ambapo kwa mujibu wa maelezo yake askari waliofika
kumkamata ofisini hapo walimweliza kuwa alitishia kumuua ofisa mtendaji wa kata
ya Ruiwa Jordan Masweve.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi
alithibitisha kuachiwa kwa dhamana mbunge Kirufi alipozungumza na waandishi wa
habari kwa njia ya simu.
Nyombi alisema mbunge huyo yupo nje kwa dhamana na
atafikishwa mahakamani siku ya jumatatu kusomewa shitaka la kutishia kuua kwa
maneno.
Hata hivyo kamanda huyo hakutaja mbunge atafikishwa
katika mahakama ipi bali alisema ofisi ya mwanasheria wa serikali mfawidhi mkoa
wa Mbeya ndiyo inayotambua mahakama hiyo kwani hata kukamatwa kwake kulilenga
kutekeleza agizo la ofisi hiyo.
“Baada ya askari wetu kumkamata jana,leo hii
tumemfikisha katika ofisi ya mwanasheria wa serikali na wao ndiyo watamfikisha
mahakamani.Lakini hivi sasa yupo nje kwa dhamana na shitaka linalomkabili ni
kutishia kuua kwa maneno” alisema Nyombi
Kwa upande wa Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi CCM
mkoa wa Mbeya umesema hauhusiki na mashitaka yanayomkabili mbunge huyo kwani ni
masuala yake binafsi na si ya chama.
Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Verena Shumbusho alisema
jana kuwa shitaka la kutishia kuua linalomkabili mbunge kirufi chama hakiwezi
kulitolea tamko lolote.
“Kama chama hatuwezi kutoa tamko lolote juu ya
kukamatwa kwake wala shitaka linalomkabili.Hilo ni suala lake binafsi na chama
hatulitambui kabisa” alisema Shumbusho.
Sunday, October 2, 2011
MATOKEO IGUNGA
Kwa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari ikiwemo mtandao wa JF zinatanabaisha kuwa
Matokeo Igunga.(Jumla kuu ni CCM 26266. CHADEMA 22443)
Na haya ni kata kwa kata...
Mboto CCM 730- CHADEMA 302
Nguvu moja CCM 694 CHADEMA 284
Nkinga CCM1479. CHADEMA 1085
Itumba CCM1079 CHADEMA 590
Nanga. CCM 897. CHADEMA 645
Igurubi CCM 925 CHADEMA 592
Mwisi CCM 926. CHADEMA 992
Mbutu. CCM 1186. CHADEMA 1426
Kinungu. CCM 505 CHADEMA 268
Ngulu CCM 622 CHADEMA 412
Igunga CCM 3181 CHADEMA 3358
Choma CCM 1227 CHADEMA 918
Kining. CCM 700 CHADEMA 451
Mwashiku. CCM 798 CHADEMA 484
Nsimbo CCM 738 CHADEMA 1016
Itunduru CCM 738 CHADEMA 784
Mwamashimba CCM 1224 CHADEMA 1421
Mbutu CCM 1335 CHADEMA 1427
Bukoko CCM 1136 Chadema 931
Nyandekwa CCM 691 Chadema 631
Ndembezi CCM 866 Chadema 806
Chabutwa CCM 545 Chadema 581
Ziba CCM 1053 Chadema 860
Igoweko CCM 1051 Chadema 880
Sungwizi CCM 1225 Chadema 718
Isakamaliwa CCM 525 Chadema 593
Matokeo Igunga.(Jumla kuu ni CCM 26266. CHADEMA 22443)
Na haya ni kata kwa kata...
Mboto CCM 730- CHADEMA 302
Nguvu moja CCM 694 CHADEMA 284
Nkinga CCM1479. CHADEMA 1085
Itumba CCM1079 CHADEMA 590
Nanga. CCM 897. CHADEMA 645
Igurubi CCM 925 CHADEMA 592
Mwisi CCM 926. CHADEMA 992
Mbutu. CCM 1186. CHADEMA 1426
Kinungu. CCM 505 CHADEMA 268
Ngulu CCM 622 CHADEMA 412
Igunga CCM 3181 CHADEMA 3358
Choma CCM 1227 CHADEMA 918
Kining. CCM 700 CHADEMA 451
Mwashiku. CCM 798 CHADEMA 484
Nsimbo CCM 738 CHADEMA 1016
Itunduru CCM 738 CHADEMA 784
Mwamashimba CCM 1224 CHADEMA 1421
Mbutu CCM 1335 CHADEMA 1427
Bukoko CCM 1136 Chadema 931
Nyandekwa CCM 691 Chadema 631
Ndembezi CCM 866 Chadema 806
Chabutwa CCM 545 Chadema 581
Ziba CCM 1053 Chadema 860
Igoweko CCM 1051 Chadema 880
Sungwizi CCM 1225 Chadema 718
Isakamaliwa CCM 525 Chadema 593
Sunday, September 25, 2011
14 wafa katika ajali ya fuso,zaidi ya 40 wajeruhiwa
Watu 14 wamekufa na wengine zaidi ya
40 kujeruhiwa baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka mnadani katika
kijiji cha Mbuyuni Wilayani Chunya kupinduka katika eneo la Mlima Msangamwelu
barabara ya Mbalizi-Chunya.
Ajali hiyo imetokea jana Septemba 24
mwaka huu majira ya saa 12:00 jioni katika eneo la Mlima Msangamwelu ambapo mmoja
wa mashuhuda wa ajali hiyo, Eden Sanga amesema gali hilo aina ya fuso
lililokuwa limebeba abiria pamoja na mizigo lilishindwa kupanda mlima na
kupinduka kutokana na kufeli kwa breki.
Sanga amesema kulikuwa na magari
mawili yameongozana ambapo wote walikuwa wanatokea mnadani na kwamba fuso
walilokuwa wamepanda wao lilifanikiwa kupanda mlima huo bila matatizo lakini
gari la wenzao lilishindwa kupanda mlima huo na kupinduka.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Anacret Malindisa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambapo alisema watu 11 walifariki papo hapo mara baada ya ajali hiyo kutokea na wengine watatu walifariki jana asubuhi wakati wakipatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mbalizi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Anacret Malindisa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambapo alisema watu 11 walifariki papo hapo mara baada ya ajali hiyo kutokea na wengine watatu walifariki jana asubuhi wakati wakipatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mbalizi.
Amesema
watu hao walikuwa wanasafiri katika lori aina ya fuso lenye namba za usajili T
532 AJF lililokuwa likitokea Mbuyuni Wilayani Chunya ambapo lilikuwa limebeba
mizigo na watu ambao walikuwa wakitoka mdani.
Amewataja watu waliokufa katika ajali hiyo ambao wametambulika kwa jina moja moja kuwa ni Exzavery, Kaloli, Lembo, Masai, Kashinje, Noa,mama Anna Ugalahenga, Mwakalasya, Meshack na Mwakilasa ambvao miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya,
Hata hivyo Malindisa amesema kuwa watu wengine watatu waliofariki leo asubihi katika hospitali teuleya ifisi bado majina yao hayajatambuliwa.Aidha alisema uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hiyo bado unaendelea na kwamba taarifa kamili itatolewa baadae.
Amewataja watu waliokufa katika ajali hiyo ambao wametambulika kwa jina moja moja kuwa ni Exzavery, Kaloli, Lembo, Masai, Kashinje, Noa,mama Anna Ugalahenga, Mwakalasya, Meshack na Mwakilasa ambvao miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya,
Hata hivyo Malindisa amesema kuwa watu wengine watatu waliofariki leo asubihi katika hospitali teuleya ifisi bado majina yao hayajatambuliwa.Aidha alisema uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hiyo bado unaendelea na kwamba taarifa kamili itatolewa baadae.
Saturday, September 24, 2011
Wanafunzi acheni siasa,zinashusha taaluna yenu
Hatua ya vijana walioko mashuleni na vyuoni kujiingiza
katika siasa imetajwa kuwa ugonjwa mbaya unaohatarisha taaluma nchini pamoja na
mustakabali wa maisha ya watanzania miaka michache ijayo.
Ili kuepuka na balaa linaloweza kuikumba nchi badae
vijana hao wametahadharishwa kutojiuhusisha na siasa na badala yake waelekeze
nguvu zao kwenye masomo ili kuinua kiwango chao cha Taaluma.
Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa (Saccos) cha
Walimu wa shule za Sekondari wilayani Mbeya, Frank Phiri ameyasema hayo kwenye
mahafari ya pili ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Itebwa ambapo
jumla ya wanafunzi 86 wamehitimu.
Amesema wanafunzi wanapaswa kutambua kuwa viongozi
wakisiasa wakongwe wanaowashabikia hivi sasa walijiingiza katika siasa hiyo
baada ya kutoka masomoni na si wakiwa masomoni na ndiyo maana taaluma zao
zinaonekana kuwa nzuri.
Awali Mwalimu Mkuu wa shule, Mpege Mwamkota amesema shule hiyo
inakusudia kuboresha huduma za hosteli ili
kukabiliana na changamoto ya wanafunzi wa kike kukatisha masomo kutokana na kupata
mimba.
Subscribe to:
Posts (Atom)