MWANAFUNZI wa sekondali ya Iramba mkoani hapa,Christina Nyingi(20) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa kwa kosa la wizi wa mali yenye thamani ya shilingi milioni 2.
Awali, akisomewa mashitaka na wakili wa serikali Adolf Maganda Mbele ya hakimu mkazi Francis Kishenyi alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa novemba 28mwaka jana katika maeneo ya uhindini jijini hapa.
Maganda alieleza mahakamani hapo kuwa mshitakiwa novemba 28 mwaka jana maeneo ya uhindini aliiba camera ya digital moja,simu moja aina ya nokia,magauni mawili,chupa sita za pafyumu na mabegi mawili vyote vikiwa na thamani ya milioni 2 mali ya Mili Maboko.
Mshitakiwa alikana shitaka na kurudishwa rumande katika gereza la Ruanda jijini hapa,baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana na kwamba kesi hiyo itatajwa tena febuari 8 mwaka huu.
Wakati huohuo Mkazi wa Manzese Darajani jijini Dar es salaamu amefikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na shtaka la kujifanya polisi.
Akisomewa shitaka na wakili wa serikali Adolf Maganda mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa Kussaga Majinge alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa januari 4 mwaka huu katika maeneo ya iyunga mkoani hapa.
Mshitakiwa alikana shtaka na kurudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza Masharti ya dhama, kesi hiyo itatajwa tena febuari 8 mwaka huu.
Joachim Nyambo, Mbeya Januari 26 2012