Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, January 18, 2012

Mbeya City kukipiga na Yanga,Simba na Azam

 
TIMU ya soka ya Mbeya City ya jijini Mbeya iliyopo katika ligi daraja la kwanza inaondoka alhamisi hii kuelekea jijini Dar es salaam kwaajili ya michezo ya kirafiki ikiwa ni katika kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi hiyo utakaoanza februari 5 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo(Januari 18) mkurugenzi wa halmashauri ya jiji Juma Iddy amesema ziara hiyo itaiwezesha timu kucheza jumla ya michezo sita ambapo kwa Dar es salaam pekee itacheza michezo mine.

Iddy amesema ikiwa Dar es salaam itacheza na timu tatu za ligi kuu ya Tanzania bara alizozitaja kuwa ni pamoja na mabingwa watetezi timu ya Yanga,Simba pamoja na Azam FC na timu moja iliyopo daraja la kwanza ambayo hakuwa tayari kuitaja.

Amesema baada ya michezo mine timu hiyo itaanza safari ya kurejea jijini Mbeya lakini ikiwa njiani itacheza na timu ya JKT Ruvu ya Pwani na Moro United na iwapo mazungumzo yatafanikiwa itacheza pia na Polisi Tanzania ya mkoani Dodoma.

Amesema timu hiyo kwa kukaa muda mrefu kambini anaamini itafanya vyema katika mzunguko ujao kama ilivyokuwa kwa ule wa awali ambapo hadi unamalizika Mbeya City ilikuwa na jumla ya pointi 13 ikiwa haijapoteza hata mchez o mmoja zaidi ya kutoa sare moja.

No comments:

Post a Comment