Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, January 18, 2012

Wafanyabiashara wakubwa wanawadanganya wadogo suala la ushuru

Na Joachim Nyambo,Mbeya.

MKURUGENZI wa halmashauri ya jiji la Mbeya Juma Iddy ametoa ufafanuzi juu ya mambo yanayochochea migogoro ya wafanyabiashara wanaogomea ongezeko la ushuru katika masoko ya jijini humo.

Mgogo huo ulianza tangu Januari 16 mwaka huu baada ya wafanyabiashara katika soko la Soweto kugoma wakipinga ongezeko la ushuru walilotangazia na kusababisha soko hilo kufungwa kwa muda na umejkuwa ukizuka katika masoko mengine licha ya kuwepo kwa vikao vya mara kwa mara vinavyoukutanisha uongozi wa halmashauri na wafanyabiashara ili kufikia muafaka.

Akizungumza na waandishi wa habari leo(Januar18) ofisini kwake,Iddy amesema  mvutano huo unasababishwa na mitazamo binafsi walionao wafanyabiashara wanaomiliki vibanda ama maduka madogo wanaotaka waendelee kulipa shilingi 200 sawa na wale wanaouza nyanya na mchicha.

Alisema wafanyabiashara hao wanawashinikiza wale wadogo kwa kuwafukuza ndani ya masoko ili ionekane msimamo wa kupinga ongezeko la ushuru ni la wafanyabiashara wote jambo ambalo  halilengi kuwasaidia wanaozalisha faida ndogo ikilinganisha na wao.

Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo,ongezeko la ushuru na bei za pango la vibanda na maduka linatokana na sheria ndogo mpya iliyopitishwa mwaka jana ikiwa imeridhiwa na wadau wote wakiwemo wafanyabiashara kupitia njia mbalimbali zinazostahili kufuatwa kabla ya sheria kupitishwa.

Amesema sheria hiyo inawataka wafanyabiashara wa bidhaa kama mbogamboga kuendelea kulipa shilingi 200 iliyokuwa ikitozwa kwa wafanyabiashara wote kwenye masoko tangu mwaka 2008,shilingi 300 kwa wanaomiliki vizimba na shilingi 500 kwa walio na vibanda ama maduka madogo ambao huza pia bidha aza viwandani.

Kwa upande wa miuondombinu inayolalamikiwa katika soko la Sido,mkurugenzi huyo amesema halmashauri haiwezi kuwekeza miundombinu ya muda mrefu kwakuwa eneo hilo si mali yake na mkataba wa wafanyabiashara kufanyia shughuli zao hapo utamalizima baada ya ujenzi wa soko la Mwanjelwa kumalizika na wafanyabiashara waliokuwepo awali kurejeshwa hapo.

No comments:

Post a Comment