Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, January 12, 2012

KKKT wataka Jamboleo iwalipe milioni 800


Na Joachim Nyambo,Mbeya.

KANISA la Kiinjili la Kilutheri KKKT dayosisi ya Konde limetoa siku saba kwa gazeti la Jamboleo kukanusha habari iliyochapishwa na gazeti hilo ikihusu kanisa kuwatimua wachungaji wawili kwa tuhuma za kujihusisha na uingizaji wa dawa za kulevya nchini kupitia msamaha wa kodi kwenye uingizaji wa mizigo ya kanisa.

Siku hizo saba zimetolewa na kanila likitaka  gazeti likanushe habari hizo kupitia ukurasa wake wa kwanza na kulipa fidia ya shilingi milioni 800 kwa kuishushia hadhi yake mbele ya jamii na wadau wengine ambao wamepoteza uimani na kanisa hilo.

Kiongozi mkuu wa KKKT dayosisi ya Konde Askofu Israel Mwakyolire ametoa tamko hilo leo (Januari 12) alipokuwa akitoa msimamo wa kanisa kwa waandishi wa habari juu ya habari hiyo iliyochapishwa Januari mosi 2012 katika gazeti hilo.

Askofu Mwakyolire amesema kutotekelezwa kwa maagizo hayo katika muda uliopangwa kutoka siku ya tamko kutapelekea kanisa kufungua shitaka mahakamani ili kuiwajibisha kampuni.

Amesema pia kanisa linamtaka mwandishi wa habari hiyo (Dotto Mwaibale) kujieleza kusudio lake katika kutoa taarifa ya uongo yenye nia na kusudia la kulidharirisha kanisa ama sivyo pia atafikishwa mahakamani kwani hakuna mchungaji yeyote aliyefukuzwa wala kusimamishwa na kanisa.

Mwisho.

Na Joachim

No comments:

Post a Comment