Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, September 25, 2011

14 wafa katika ajali ya fuso,zaidi ya 40 wajeruhiwa


Watu 14 wamekufa na wengine zaidi ya 40 kujeruhiwa  baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka mnadani katika kijiji cha Mbuyuni Wilayani  Chunya kupinduka katika eneo la Mlima Msangamwelu barabara ya Mbalizi-Chunya.

Ajali hiyo imetokea jana Septemba 24 mwaka huu majira ya saa 12:00 jioni katika eneo la Mlima Msangamwelu ambapo mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Eden Sanga amesema gali hilo aina ya fuso lililokuwa limebeba abiria pamoja na mizigo lilishindwa kupanda mlima na kupinduka kutokana na kufeli kwa breki.

Sanga amesema kulikuwa na magari mawili yameongozana ambapo wote walikuwa wanatokea mnadani na kwamba fuso walilokuwa wamepanda wao lilifanikiwa kupanda mlima huo bila matatizo lakini gari la wenzao lilishindwa kupanda mlima huo na kupinduka.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Anacret Malindisa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambapo alisema watu 11 walifariki papo hapo mara baada ya ajali hiyo kutokea na wengine watatu walifariki jana asubuhi wakati wakipatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mbalizi.

Amesema watu hao walikuwa wanasafiri katika lori aina ya fuso lenye namba za usajili T 532 AJF lililokuwa likitokea Mbuyuni Wilayani Chunya ambapo lilikuwa limebeba mizigo na watu ambao  walikuwa wakitoka mdani.

Amewataja watu waliokufa katika ajali hiyo ambao wametambulika kwa jina moja moja kuwa ni  Exzavery, Kaloli, Lembo, Masai, Kashinje,  Noa,mama Anna Ugalahenga, Mwakalasya, Meshack na Mwakilasa ambvao miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya,

Hata hivyo Malindisa amesema kuwa  watu wengine watatu waliofariki leo asubihi katika hospitali  teuleya ifisi  bado majina yao hayajatambuliwa.Aidha alisema uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hiyo bado unaendelea na kwamba taarifa kamili itatolewa baadae.

Saturday, September 24, 2011

Wanafunzi acheni siasa,zinashusha taaluna yenu


Hatua ya vijana walioko mashuleni na vyuoni kujiingiza katika siasa imetajwa kuwa ugonjwa mbaya unaohatarisha taaluma nchini pamoja na mustakabali wa maisha ya watanzania miaka michache ijayo.
Ili kuepuka na balaa linaloweza kuikumba nchi badae vijana hao wametahadharishwa kutojiuhusisha na siasa na badala yake waelekeze nguvu zao kwenye masomo ili kuinua kiwango chao cha Taaluma.
Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa (Saccos) cha Walimu wa shule za Sekondari wilayani Mbeya, Frank Phiri ameyasema hayo kwenye mahafari ya pili ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Itebwa ambapo jumla ya wanafunzi 86 wamehitimu.
Amesema wanafunzi wanapaswa kutambua kuwa viongozi wakisiasa wakongwe wanaowashabikia hivi sasa walijiingiza katika siasa hiyo baada ya kutoka masomoni na si wakiwa masomoni na ndiyo maana taaluma zao zinaonekana kuwa nzuri.
Awali Mwalimu Mkuu wa  shule, Mpege Mwamkota amesema shule hiyo inakusudia kuboresha  huduma za hosteli ili kukabiliana na changamoto ya wanafunzi wa kike kukatisha masomo kutokana na kupata mimba.

Urasimu,Rushwa changamoto kwa Stakabadhi yaa mazao ghalani

URASIMU na rushwa vimetajwa kuwa changamoto kubwa inayokwamisha mfumo wa stakabadhi ya mazao gharani licha ya serikali kulipa uzito suala hilo.

Katibu Tawala Msaidizi uchumi mkoa wa Mtwara Shangwe Twamala aliyasema hayo jana jijini Mbeya alipokuwa akitoa mada ya Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani kwa washiriki kutoka halmashauri zote za wilaya mkoa wa Mbeya.

Twamala alisema mkoa wa Mtwara uliokuwa wakwanza kutumia mfano huo katika zao la Korosho umekumbana na vikwazo vingi katika utekelezaji wa mfumo na kutaja moja ya vikwazo hivyo kuwa ni rushwa inayotolewa na wanunuzi waliokuwa wakiwanyonya wakulima wa zao hil

Alitolea mfano kuwa kuna wakati wafanyabiashara hao walichanga pesa na kuwahonga madereva wa malori yaliyopewa kazi ya kusafirisha gunia tupu kutoka Dar es salaam hadi mkoani hapo kwaajili ya kuhifadhia zao hilo na kuwataka wazicheleweshe kwa kulala njiani.

“Waliwahonga madereva wa malori wakiwataka wawe na vituo vingi vya kulala ili wakulima waone mfumo huu haufai na kuamua kuuza korosho kwa wafanmyabiashara vwa siku zote.Ilitubidi tukaongea na makamanda wa polisi wa mikoa yote ya njiani kuwaomba wasiruhusu gari hizo zilale njiani ndiyo tukafanikiwa” alisema.

Nao uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Kyela ulisema urasimu katika utoaji wa leseni za usajiri wa Maghala umesababisha kushindwa kwa mfumo huo msimu huu ambapo ilitarajiwa mfumo huo utumike kwa mazao ya mpunga na korosho lakini mpaka sasa maghala waliyonayo hayajasajiriwa.

Friday, September 23, 2011

TUCTA Mbeya wapongeza uchaguzi wao taifa,Waonya


SHIRIKISHO la vyama huru vya wafanyakazi TUCTA mkoani Mbeya limetoa saalamu za pongezi kwa viongozi wapya washirikisho waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika septemba 15 mwaka huu mjini Arusha.

Kaibu katibu wa TUCTA mkoani Mbeya Thomas Kasombwe akizungumza na gazeti hili amesema kuchaguliwa kwa mara nyingine kwa mwenyekiti shirikisho hilo Omary Ayoub na katibu Nicholaus Mgaya kunadhihirisha jinsi wanashirikisho walivyo bado na matumaini na uonmgozi wao.

Kasombwe alisema tawi la Mbeya linatambua mchango wa viongozi hao katika kupigania maslahi ya wafanyakazi kwa waajiri wao hivyo wanaamini kuwa mikakati waliyoianzisha kwenye kipindi kilichopita wataiendeleza katika uongozi huu.

Hata hivyo alisema nguvu zaidi ya ushirikiano katika utendaji inahitajika ili kufikia malengo ya utatuzi wa changamoto zinazowakabili wanachama wa vyama vya wafanyakazi hivyo ni vema wakafanya kazi kwa bidii.

Kaimu katibu huyo aliyataja mabo ambayo uongozi huo mpya ni vema wakaanza naayo kwakuwa yapo mezani kwao kuwa ni pamoja na kuendelea kuihimiza serikali kuongeza kima cha chini cha mishahara kutoka 150,000 cha sasa na kufikia 315,000.

Changamoto nyingine ni serikali kupunguza kiasi cha kodi kwa wafanyakazi kwa asilimia 9 au 10 kabisa badaala ya punguzo la asilimia moja lililotangazwa na serikali hivi karibuni.

Alisema ni vema pia uongozi wa shirikisho ukakaa pamoja na serikali na kujadili ni jinsi gani itaweza kutatua tatizo la mgawo wa umeme kwa haraaka pamoja na kushusha bei ya nishati hiyo muhimu katika maendeleo ya jamii.

“Tunatambua sote kuwa kukosekana kwa umeme wa uhakika kwa kiasi kikubwa kunayumbisha uchumi wan chi yetu.Waananchi wanashindwa kuzalisha,viwanda havifanyi kazi ipasavyo na hiyo inasababisha hata serikali kukosa kodi.Lakini hata utakapopatikana umeme wa uhakika tungependa bei yake ishuke ili isiwaumize watanzania” alisema

Alisema suala jingine ni kutokuwepo na utaratibu maalumu unaoongoza kupanda na kushuka kwa mafuta hali inayozusha mgongano wa mara kwa mara baina ya wadau husika hali inayopaswa kuisimamiwa na uongozi wa shirikisho kusaiduiana na serikali kupata ufumbuzi wake.

Kikao kuwapika viongozi wa halmashauri Mbeya


MAZUNGUMZO YA KATIBU TAWALA MKOA BIBI BEATHA O. SWAI KATIKA KUELEZA MADHUMUNI YA MAFUNZO YA KILIMO TAREHE 22 -23 SEPTEMBA, 2011 MKOANI MBEYA.
*      Wazo la kuendesha mafunzo ya uvuvi, nyuki, samaki, Stakabadhi ya Mazao Ghalani na Huduma za Ugani kwa viongozi na watalaamu  yametokana na mawazo yafuatayo:-

i.                    Mkoa haujafikia lengo la kuzalisha tani 4,459,995
ii.                 Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani haujaeleweka vema kwa wadau.
iii.               Sekta za uvuvi, nyuki na samaki hazijaendelezwa ipasavyo licha ya Mkoa kuwa na fursa kubwa ya kuendeleza Sekta hizi.
iv.               Mfumo wa uwajibikaji katika kusimamia kilimo unapashwa kuboresha ili kufikia malengo yaliyowekwa.
v.                  Pia kutekeleza maazimio yaliyofikiwa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika “Retreat” ya Homboro Julai 2011 pamoja na .”Retreat” ya Viongozi wa ngazi ya Mkoa na Wilaya iliyofanyika tarehe 18 Agosti, 2011 Mkoani Mbeya.

*      Mafunzo haya ya siku mbili (22-23 Septemba, 2011) yatatolewa na wawezeshaji ifuatavyo:-
i.                    Bw. Shangwe Twamala – Katibu Tawala Msaidizi – Uchumi kutoka RS Mtwara ambaye atatoa mada za:
a.      Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani
b.      Mfumo wa usimamizi wa Huduma za Ugani
ii.                 Bw. Edwin Meela – Afisa Nyuki – HW Manyoni ambaye atatoa mada ya ufugaji bora wa nyuki
iii.               Bw. Walece Z. Masha – Afisa Uvuvi – RS Ruvuma ambaye atatoa mada kuhusu ufugaji bora wa samaki, na
iv.               Bw. Jaliwa A. Ntibiyoboka -(Afisa Ushirika  HW Mpanda ambaye atatoa mada za:-
a.      Matumizi ya Daftari la Kilimo na
b.      Dhana ya Waganikazi kutika Huduma za Ugani

*      Washiriki wa mafunzo haya wamechaguliwa kwa makini kwa sababu aidha ni Wasimamizi na wafuatiliaji (DC, DED, M/kiti HW, M/Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira ya HW) au ni watekelezaji (wataalamu na wakulima). Hivyo mafunzo haya yatawafaa.

*      Matarajio kutokana na mafunzo haya ni kwamba:-
        i.            Washiriki wote kupata uelewa wa pamoja kuhusu masuala ya ufugaji bora na wa kibiashara wa nyuki na samaki, matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani na mfumo bora wa Huduma za Ugani kwa wakulima na wafugaji.
     ii.            Kupata uzoefu wa utekelezaji wa maeneo hayo kutoka kwa wawezeshaji.
   iii.            Kupata mawazo mbalimbali kutoka kwa washiriki kuhusu namna ya kuwa na mikakati ya kuendeleza sekta za kilimo, mifugo, uvuvi, nyuki pamoja Mfumo wa Stakabadhi ya Mazap Ghalani na Huduma za Ugani kwa wakulima na kufikia makubaliano ya utekelezaji katika Mkoa wetu.

*      Mhe. Mwenyekiti baada ya maelezo haya ya utangulizi naomba nikukaribishe rasmi ufungue mafunzo haya.