Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, September 24, 2011

Urasimu,Rushwa changamoto kwa Stakabadhi yaa mazao ghalani

URASIMU na rushwa vimetajwa kuwa changamoto kubwa inayokwamisha mfumo wa stakabadhi ya mazao gharani licha ya serikali kulipa uzito suala hilo.

Katibu Tawala Msaidizi uchumi mkoa wa Mtwara Shangwe Twamala aliyasema hayo jana jijini Mbeya alipokuwa akitoa mada ya Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani kwa washiriki kutoka halmashauri zote za wilaya mkoa wa Mbeya.

Twamala alisema mkoa wa Mtwara uliokuwa wakwanza kutumia mfano huo katika zao la Korosho umekumbana na vikwazo vingi katika utekelezaji wa mfumo na kutaja moja ya vikwazo hivyo kuwa ni rushwa inayotolewa na wanunuzi waliokuwa wakiwanyonya wakulima wa zao hil

Alitolea mfano kuwa kuna wakati wafanyabiashara hao walichanga pesa na kuwahonga madereva wa malori yaliyopewa kazi ya kusafirisha gunia tupu kutoka Dar es salaam hadi mkoani hapo kwaajili ya kuhifadhia zao hilo na kuwataka wazicheleweshe kwa kulala njiani.

“Waliwahonga madereva wa malori wakiwataka wawe na vituo vingi vya kulala ili wakulima waone mfumo huu haufai na kuamua kuuza korosho kwa wafanmyabiashara vwa siku zote.Ilitubidi tukaongea na makamanda wa polisi wa mikoa yote ya njiani kuwaomba wasiruhusu gari hizo zilale njiani ndiyo tukafanikiwa” alisema.

Nao uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Kyela ulisema urasimu katika utoaji wa leseni za usajiri wa Maghala umesababisha kushindwa kwa mfumo huo msimu huu ambapo ilitarajiwa mfumo huo utumike kwa mazao ya mpunga na korosho lakini mpaka sasa maghala waliyonayo hayajasajiriwa.

No comments:

Post a Comment