Friday, May 29, 2015
Thursday, May 28, 2015
Wednesday, May 27, 2015
Tuesday, May 26, 2015
HAPA NDIPO TUNAPOANZIA KUPOROMOSHA MAADILI YA JAMII YETU
KATIKA kipindi cha miaka ya zamani Ualimu ulikuwa
wito.Ni kutokana na hali hiyo watu walioajiriwa kwenye tasnia hiyo walikuwa
wenye staha kulingana na walivyofundishwa chuoni.
Uwepo wao katika kundi lolote ndani ya jamii
uliwatofautisha na makundi mengine.Walionekana watu wenye kutegemewa na jamii
kwenye masuala ya ushauri na hakika jamii iliyowazunguka ilinufaika na uwepo
wao.
Walimu katika miaka hiyo hawakuishia kufundisha wanafunzi
darasani,walifundisha jamii yote.Palipotokea na jambo jamii ilikusanyika na
kuhimiza lazima mwalimu flani awepo kwenye kikao hicho.
Leo hii mambo ni tofauti!Walimu wamekuwa chanzo cha
jamii kupoteza mwelekeo.Mavazi yasiyoendana na wadhifa walio nao imekuwa jambo
la kawaida kwa walimu wetu.
Ni vema jamii ikatambua kuwa shuleni ni sehemu
muhimu kwenye makuzi ya mtoto.Ili kuepuka matokeo mabaya ya mtoto katika siku
za baadaye ni muhimu jamii ikaona umuhimu wa kuweka mazingira yenye kuwezesha
walimu wenye staha na wenye kutambua wajibu wao katika jamii inayowazunguka.
MAJIMBO YA MBEYA KUGAWANYWA.
MAJIMBO ya Mbeya mjini
na Mbeya vijijini huenda yakagawanywa na kuwa majimbo mawilimawili iwapo Tumea
ya taifa ya uchaguzi itaridhia maombi yaliyopendekezwa na wadau kwenye vikao
vya Ushauri vya wilaya vilivyofanyika jana.
Vikao vya kuyagawa
majimbo hayo vimefanyika kwa nyakati na tofauti kwenye ukumbi wa halmashauri ya
wilaya ya Mbeya ambapo kwa jimbo la Mbeya mjini wadau wamependekeza kuundwa kwa
majimbo mapya ya Iyunga na Sisimba huku Jimbo la Mbeya vijijini likipendekezwa
kuundwa kwa majimbo ya Mbeya na Isangati.
Akizungumza kwenye
kikao cha Ushauri cha wilaya,Mkurugenzi wa jiji la Mbeya Bwana Musa Zungiza amesema
mapendekezo ya mgawanyo wa jimbo la Mbeya mjini yanazingatia maeneo ambayo
awali yalikuwa ni tarafa.
Bw.Zungiza amesema
katika Tarafa ya Iyunga ambayo sasa inapendekezwa kuwa jimbo kuna kata 21 na
mitaa 116,iinakadiriwa kuwa na wakazi 327,122 hadi kufikia Julai 2015 idadi
aliyosema inakidhi vigezo vya tarafa hiyo kuwa jimbo.
Kwa upande wa tarafa ya
Sisimba inayopendekezwa kuwa jimbo la Sisimba amesema ina kata 15 inayokadiriwa
kuwa na wakazi 106,264 kufikia Julai mwaka huu.
Naye mkurugenzi
mtendaji wa halmashauri Bibi Upendo sanga amesema jimbo la Mbeya litakuwa na
kata 11 zinazokadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 107,349.
Bi.Sanga amesema jimbo
la Isangati lenye kata 15 zinazokadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 221.
Mwisho.
Saturday, May 23, 2015
WANANDOA WACHINJWA NA KUUAWA KWA KUTENGANISHWA VICHWA
WANANDOA
wawili wakazi katika kitongoji cha Makambo Kata ya Itenka wilayani Mlele
Mkoani Katavi wameuawa kikatili kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa
kichwa na kiwiliwili baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana wakati
wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao.
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari amewataja wanandoa hao wawili waliouawa kuwa ni Seth Mwakalimbwa (65) na Yakoba Kalulu(48) wakazi wa kitongoji hicho.
Kidavashari
amesema jana kuwa tukio hilo la mauaji ya kikatili lilitokea hapo juzi nyakati
za usiku wa manane nyumbani kwa wanandoa hao waliokuwa wakiishi pamoja
kama mke na mume
Amesema kwamba marehemu hao wakutwa na mauti hayo wakati wakiwa ndani ya nyumba wamelala ambapo kundi la watu wasiofahamika walivamia nyumba yao na kuwaua kwa kuwakata kata na mapanga mwilini kiasi cha kupoteza fahamu kisha kuwachinja kwa kuwatenganisha kichwa na kiwiliwili.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa, Balozi wa eneo hilo, Wilbroad Mahenge alisema kuwa yeye ndio alibaini kutokea kwa mauaji hayo baada ya kutowaona wanandoa hao kwa siku mbili pasipo kuwa na taarifa yoyote.
Mahenge alisema kuwa kutokana na kutokuwa na taarifa yoyote ukizingatia kwamba pia yeye ni jirani yao, alikwenda katika makazi yao na alipofika hapo, alikuta milango ya nyumba yao iko wazi hali ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Ameongeza kwamba alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika hivyo aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hali hiyo, Mahenge alitoka nje na kasha alikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitoa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda Kidavashari amesema chanzo cha tukio la mauaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo lakini polisi inaendelea kuwasaka watu hao.
Amesema kwamba marehemu hao wakutwa na mauti hayo wakati wakiwa ndani ya nyumba wamelala ambapo kundi la watu wasiofahamika walivamia nyumba yao na kuwaua kwa kuwakata kata na mapanga mwilini kiasi cha kupoteza fahamu kisha kuwachinja kwa kuwatenganisha kichwa na kiwiliwili.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa, Balozi wa eneo hilo, Wilbroad Mahenge alisema kuwa yeye ndio alibaini kutokea kwa mauaji hayo baada ya kutowaona wanandoa hao kwa siku mbili pasipo kuwa na taarifa yoyote.
Mahenge alisema kuwa kutokana na kutokuwa na taarifa yoyote ukizingatia kwamba pia yeye ni jirani yao, alikwenda katika makazi yao na alipofika hapo, alikuta milango ya nyumba yao iko wazi hali ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Ameongeza kwamba alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika hivyo aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hali hiyo, Mahenge alitoka nje na kasha alikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitoa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda Kidavashari amesema chanzo cha tukio la mauaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo lakini polisi inaendelea kuwasaka watu hao.
CHANZO-PEMBEZONI KABISA BLOG
Friday, May 22, 2015
TMA YAPELEKA HUDUMA ZIWA NYASA
Mkuu wa wilaya ya Kyela Thea Ntara(wa tatu kutoka kulia) akiwa na maafisa wa TMA na wadau wengine wa shughuli za kimaendeleo katika ziwa Nyasa.Wadau hawa walikutana mjini Kyela kupashana habari za ujio wa TMA katika ziwa Nyasa sambamba na kupeana uzoefu juu ya majanga ya ziwa hilo.
Kaimu mkurugenzi wa
huduma za ufundi za TMA Dk.Pascal Waniha akielezea namna TMA ilivyoona umuhimu wa kufikisha huduma zake kwa watumiaji wa ziwa Nyasa.
Wadau mbalimbali wa ziwa Nyasa wakiwemo wavuvi wakishiriki semina ya kupeana uzoefu juu ya majanga ya ziwa hilo.
Wanahabari kama anavyoonekana mwandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo Solomon Mwansele ni miongoni mwa wadau ambao wametajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwenye usambazaji wa taarifa zitakazotolewa na TMA juu ya utabiri wa hali ya hewa ndani ya ziwa Nyasa.
Mkuu wa wilaya ya Kyela
Thea Ntara akibainisha namna ujio wa TMA katika ziwa Nyasa ulivyoleta neema kwa watumiaji wa ziwa hilo
Mkurugenzi wa huduma za Utabiri za TMA Dk.Hamza Kabelwa akibainisha mikakati ya TMA katika utoaji taarifa za hali ya hewa.
HABARI KAMILI.
MAMLAKA ya Hali ya Hewa
Tanzania(TMA) imepeleka huduma zake katika wilayani Kyela lengo ni kusogeza
huduma ya upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa kwa watumiaji wa ziwa Nyasa.
Kwa mujibu wa watumiaji
wa ziwa Nyasa wakiwemo wavuvi na wasafirishaji,kwa muda mrefu wamekuwa
wakilazimika kutumia njia za asili kubaini majanga yanayoweza kutokea ndani ya
ziwa hilo na wakati mwingine walilazimika kutumia taarifa zilizotolewa na
mamlaka ya hali ya hewa ya nchi jirani ya Malawi.
Wakazi wilayani Kyela
wanasema kutokana na changamoto hiyo madhara makubwa yamekuwa yakitokea ikiwemo
vifo vya wavuvi kutokana na vimbunga vilivyowakumba wakati wakiendelea na
shughuli zao ndani ya ziwa Nyasa.
Kaimu mkurugenzi wa
huduma za ufundi za TMA Dk.Pascal Waniha anasema mamlaka hiyo imeamua kuwafikia
watumiaji wa ziwa Nyasa kutokana na mahitaji yaliyopo.
Mkuu wa wilaya ya Kyela
Thea Ntara anasema sasa watumiaji wa ziwa hilo wako katika mazingira salama kwakuwa
kabla ya kufanya shughuli zao watapataa taarifa za uhakika juu ya utabiri wa
hali ya hewa.
Subscribe to:
Posts (Atom)