Afisa Mradi wa shirika la watu wenye ulemavu wa
ngozi nchini (TAS) Severin Mallya akikabidhi kiasi cha shilingi milioni moja
kwa mtoto Baraka Cosmas(6) aliyekatwa kuiganja na watu wasiofahamika na kulazwa
katika hospitali ya rufaa kanda ya Mbeya.Katikati ni mama wa mtoto huyo Priscar
Shaban.Kulia ni mmoja wa viongozi wa TAS Mbeya mjini.
Afisa Mradi wa shirika la watu wenye ulemavu wa
ngozi nchini (TAS) Severin Mallya akikabidhi kiasi cha shilingi milioni moja
kwa mtoto Baraka Cosmas(6) aliyekatwa kuiganja na watu wasiofahamika na kulazwa
katika hospitali ya rufaa kanda ya Mbeya.Aliyesimama ni Afisa
ustawi wa jamii mkoa wa Rukwa Dionisia Njuuli akimsubiri mtoto Baraka ili waanze safari kuelekea Dar es salaam.
Muuguzi wa zamu akiwa pamoja na mtoto Baraka na mdogo wake Lucy kabla ya Baraka kuanza safari kuelekea Dar es salaam na hatimaye kupelekwa nchini Marekani na shirika la Under the same sun kwaajili ya matibabu ya kutengenezewa kiganja cha bandia.
Wauguzi wengine pia walijumuika kumuaga Baraka.
HABARI KAMILI
SHILINGI 1,000,000
zimetolewa na Chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi nchini(TAS) ikiwa ni msaada
kwa familia ya Mtoto Baraka Cosmas(6) aliyekatwa kiganja cha mkono wake na watu
wasiojulikana.
Afisa Mradi wa TAS
Severin Mallya amekabidhi msaada huo kwa familia ya mtoto huyo iliyopewa
hifadhi ya muda katika hospitali ya Rufaa kanda ya nyanda za juu kusini iliyopo
mkoani Mbeya.
Akikabidhi msaada
huo,Mallya amesema TAS bado inaamini kuwa mapambano dhidi ya vitendo vya
kikatili vinavyofanywa na watu dhidi ya jamii ya watu walio na ualbino
yatafanikiwa iwapo jamii yote itahusika.
Amesema ni jambo la
msingi kila mwanajamii akatambua kuwa anawajibu mkubwa wa kuwalinda watu walio
na ualbino sambamba na kushiriki katika utoaji wa elimu yenye kupinga imani
potofu kuwa viungo vya watu wa jamii hiyo vinaweza kumtajirisha mtu.
Wakati TAS wakitoa
msaada huo,Mtoto Baraka tayari amesafirishwa kutoka jijini Mbeya hadi Dar es
salaam tayari kwa matibabu zaidi ikiwemo kutengenezewa kiganja cha bandia.
Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa kabla ya kuanza safari kuelekea Dar es salaam,Afisa ustawi wa jamii mkoa
wa Rukwa Dionisia Njuuli alisema mtoto Baraka atakabidhiwa kwa kituo cha
shirika la Under the same sun ambao watampeleka Marekani kwaajili ya matibabu
zaidi.
Njuuli amesema mama wa
mtoto Baraka ataendelea kuishi hospitalini hapo sambamba na wanae wawili walio
na ualbino mpaka pale serikali ya mkoa wa Rukwa itakapokuwa imetoa kauli juu ya
mahali salama wanapoweza kuishi.
No comments:
Post a Comment