Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 26, 2015

HAPA NDIPO TUNAPOANZIA KUPOROMOSHA MAADILI YA JAMII YETU



KATIKA kipindi cha miaka ya zamani Ualimu ulikuwa wito.Ni kutokana na hali hiyo watu walioajiriwa kwenye tasnia hiyo walikuwa wenye staha kulingana na walivyofundishwa chuoni.

Uwepo wao katika kundi lolote ndani ya jamii uliwatofautisha na makundi mengine.Walionekana watu wenye kutegemewa na jamii kwenye masuala ya ushauri na hakika jamii iliyowazunguka ilinufaika na uwepo wao.

Walimu katika miaka hiyo hawakuishia kufundisha wanafunzi darasani,walifundisha jamii yote.Palipotokea na jambo jamii ilikusanyika na kuhimiza lazima mwalimu flani awepo kwenye kikao hicho.

Leo hii mambo ni tofauti!Walimu wamekuwa chanzo cha jamii kupoteza mwelekeo.Mavazi yasiyoendana na wadhifa walio nao imekuwa jambo la kawaida kwa walimu wetu.

Ni vema jamii ikatambua kuwa shuleni ni sehemu muhimu kwenye makuzi ya mtoto.Ili kuepuka matokeo mabaya ya mtoto katika siku za baadaye ni muhimu jamii ikaona umuhimu wa kuweka mazingira yenye kuwezesha walimu wenye staha na wenye kutambua wajibu wao katika jamii inayowazunguka.

No comments:

Post a Comment