Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, August 21, 2014

UKATILI HUU MPAKA LINI?



Kama kweli laana ipo,naomba eeh Mwenyezi Mungu walaani watu wanaofanya ukatili huu.Huyu ni mwanamke Suzana Mgasa Mungu (34),aliye na ulemavu wa ngozi(Albino).

Mwanamke huyu alifanyiwa ukatili wa kujeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili wake na watu wasiojulikana na hatimaye watu hao kuondoka na sehemu ya mkono wake baada ya kumuua mumewe wakati akijaribu kupambana kumwokoa mkewe.

Tukio hili lilitokea Agosti 15 mwaka huu majira ya saa tano usiku huko Igunga Tabora.Vitendo hivi vya kikatili vimekuwa vikifanyika nchini na kulipa sifa mbaya taifa la watanzania wajiitao kisiwa cha amani.

Ewe mwenyezi Mungu mjaalie afya njema Suzana,na nakuomba andika majina ya waliofanya ukatili huu katika kitabu chenye orodha ya watu wasiopaswa kusamehewa kamwe.

PICHA KWA HISANI YA TANZANIA ALBINISM SOCIETY

Wednesday, August 20, 2014

WATOTO 9700 WAKABILIWA NA UTAPIAMLO KALAMBO

WATOTO 9700 waliopo katika vijiji vya Kisumba, Kasote na Chisenga kwenye kata ya Kisumba vilivyoko wilayani Kalambo mkoani Rukwa wanakabiliwa na tatizo kubwa la utapiamlo mkali kufuatia kuwepo kwa malezi duni kutoka kwa wazazi na walezi wao.

Hali hiyo imesababisha mkoa wa Rukwa kuwa miongoni mwa mikoa mitano ambayo inakabiliwa na tatizo la udumavu licha kuzalisha kwa wingi mazao ya chakula hususani ni mahindi.


Baadhi ya wanawake wa kijiji hicho walisema hayo wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi jana wakati wa sherehe za siku ya afya kijiji iliyoandaliwa katika kijiji cha Kisumba iliyoandaliwa na shirika la Africare linalotekeleza mradi wa wazazi na mwana wenye lengo la kupunguza vifo vya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano mkoani humo.

Mmoja wa wanawake hao, Yusta Sangu alisema kuwa hali hiyo imejitokeza kutokana na kukosekana kwa elimu sahihi ya afya uzazi kwa muda mrefu kiasi cha kufanya wanawake wengi  wajifungulie majumbani bila kufuata uzazi wa mpango hivyo kuwa na idadi kubwa mno ya watoto

KWA HISANI YA BLOG YA PEMBEZONI KABISA

CHADEMA MBEYA YAPATA VIONGOZI WAPYA


CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Mkoani, kimepata viongozi wapya kupitia uchaguzi uliofanyika jana jijini Mbeya.

Katika uchaguzi wa jana, Msimamizi wa uchaguzi huo Mratibu wa chama hicho kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Franky Mwaisumbe,  amemtaja Joseph China kuwa mwenyekiti mpya.


China ameibuka mshindi baada ya kupata kura 36 dhidi ya kura 19 alizopata Zabron Nzunda na nne alizoambulia Meshack Kapange aliyejiunga na chama hicho hivi karibuni akitokea CCM.

Kwa nafasi ya Katibu msimamizi amesema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho wagombea wa nafasi hiyo huomba na majina yaliyopendekezwa katika ngazi husika hupelekwa katika kamati ya utendaji taifa ambayo huthibitisha jina moja kati ya walioomba.

Mwaisumbe amesema kwa mkoa wa Mbeya walioomba nafasi hiyo ni aliyekuwa Mwenyekiti wa mpito wa chama hicho mkoa, Boyd Mwabulanga,Mwenyekiti wa Wilaya ya Mbarali, Kazamoyo Jidawaya  na   Fanul Mkisi.

Akifafanua zaid imatokeo ya uchaguzi,msimamizi huyo amesema nafasi ya Mwenyekiti wa Baraza la vijana (Bavicha)Mkoa wa Mbeya, imechukuliwa na Tito George, wakati  nafasi ya Baraza la wanawake (Bawacha) ikishikwa na Happynes Kulabya, huku  nafasi ya Mwenyekiti Baraza la wazee ikienda kwa Martin Mpwani.

Monday, August 18, 2014

NI SHIDA!!!!!!!TUKO KIKAZI ZAIDI.

Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Joachim Nyambo(kulia) akifuatiwa na mwandishi wa magazeti ya Mwananchi,The Citizen na Mwanaspoti mkoani Mbeya Brand Nelson na mwandishi wa Chanel Ten Rose Chapewa.Katikati wapo Solomoni Mwansele wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo,Rashidi Mkwinda wa Majira na Charles Mwaipopo wa Baraka FM.Mwenye suti kushoto ni mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro

Saturday, August 16, 2014

Lyamba Lya Mfipa yatembelea ofisi za Tushiriki

Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa  Bw.Joachim Nyambo(wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la TUSHIRIKI alipotembelea ofisi za shirika hilo zilizopo Soweto jijini Mbeya.

Shirika la Tushiriki linaendesha mradi wa kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira ya misitu iliyopo pembezoni mwa mlima Rungwe.

Friday, August 15, 2014

MBEYA CITY,TANZANIA PRISONS WAZUIWA KUTUMIA UWANJA WA SOKOINE

KIKOSI CHA MBEYA CITY
KIKOSI CHA TANZANIA PRISONS

 
WAMILIKI wa Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wameendelea na jitihada za kuukarabati uwanja huo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya ligi kuu ya Tanzania bara itakayoanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.

Ukarabati unaoendelea hivi sasa katika uwanja huo utakaotumiwa na Timu za Mbeya City na Tanzania Prison kama uwanja wa nyumbani ni pamoja na kuondoa magugu yasiyohitajika katika eneo la kuchezea maarufu kama Pichi.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa,Meneja wa Uwanja huo Modestus Mwaluka amebainisha namna shughuli nzima ya kuondoa magugu hayo inavyoendeshwa,shughuli ambayo pia imesababisha Timu za Mbeya City na Tanzania Prison kuzuiwa kuendelea kuutumia uwanja huo kwa mazoezi.

Mwaluka amesema wanalazimika kuyaondoa magugu hayo kutokana na asili yake mbaya ambapo huweka nundu nundu uwanjani na kusababisha mpira kukosa mwelekeo unaopaswa wakati ukichezwa katika uwanja husika.


Amezitaka timu za Mbeya City na Tanzania Prisons kutojawa na hasira baada ya kuzuiwa kutumia uwanja huo kwa mazoezi badala yake watambue kuwa  uongozi wa uwanja una nia ya dhati ya kuboresha miundombinu itakayosaidia timu hizo kucheza mpira mzuri na wenye kuvutia.

Mbunge wa zamani asimikwa kuwa kamanda wa UVCCM kata ya Kapele


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Mkoa wa Mbeya Aman Kajuna akimvisha Joho Aliyewahi kuwa mbunge wa Mbozi Magharibi(Sasa Momba) Eliakim Simpasa baada ya kumsimika rasmi kuwa Kamanda wa UVCCM kata ya Kapele wilayani Momba.

Simpasa ambaye hivi sasa ni Mjumbe wa halmashauri kuu CCM mkoa akitafakari jambo







Thursday, August 14, 2014

TUTARAJIE NINI MSIMU HUU?





JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.



 
RPC.                                                                                               Ofisi ya Kamanda wa Polisi,                                                                                                                                                                                                                                                                                               Mkoa wa Mbeya,                                                                                    
Namba ya simu 2502572                                                                                         S. L. P. 260,
Fax - +255252503734                                                                                                 MBEYA.
E-mail:-  rpc.mbeya@tpf.go.tz                                                                      



TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 14.08.2014.




·         MTOTO MDOGO MWENYE UMRI WA KATI YA MIAKA 03-04 AFARIKI DUNIA PAPO HAPO KATIKA AJALI YA GARI WILAYANI MBOZI.






·         MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA MIWILI AFARIKI DUNIA BAADA YA KUZAMA KATIKA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI.







·         MTU MMOJA MKAZI WA KIJIJI CHA MAMBA WILAYA YA CHUNYA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUNIKWA NA KIFUSI CHA UDONGO.







·         WATU WAWILI WAKAZI WA KIWIRA ROAD WILAYA YA RUNGWE WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA WAKIWA BHANGI.








KATIKA TUKIO LA KWANZA:


MTOTO MDOGO MWENYE UMRI KATI YA MIAKA 03 – 04 ALIYETAMBULIKA KWA JINA MOJA LA JACK AMEFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T. 140 BCU AINA YA SUZUKI LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA ELIUD KALINGA (54) MCHUNGAJI WA KANISA LA KKKT – TUNDUMA.

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 13.08.2014 MAJIRA YA SAA 17:00 JIONI HUKO MAENEO YA VWAWA SEKONDARI, KATA YA NDALAMBO, TARAFA YA VWAWA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA SERIKALI YA VWAWA. DEREVA AMEKAMATWA NA GARI LIPO KITUONI.

KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI MKOA WA MBEYA BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA MADEREVA NA WATUMIAJI WENGINE WA VYOMBO VYA MOTO KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO HIVYO IKIWA NI PAMOJA NA KUFUATA/KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.




KATIKA TUKIO LA PILI:


MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA MIWILI (02) ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FROLA MLINGO ALIKUTWA AMEKUFA MAJI KWENYE BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 13.08.2014 MAJIRA YA SAA 12:00 MCHANA MAHANGO, WILAYA YA MBARALI, MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA CHANZO CHA KIFO CHAKE NI KUZIDIWA NA MAJI YA BWAWA HILO WAKATI AKICHEZA NA WATOTO WENZAKE.

KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI MKOA WA MBEYA BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA WAZAZI/WALEZI KUWA MAKINI NA WATOTO WADOGO KWA KUWEKA UANGALIZI WA KUTOSHA ILI KUEPUKA MADHARA/MATATIZO YANAYOWEZA KUJITOKEZA.











KATIKA TUKIO LA TATU:


MTU MMOJA MKAZI WA KIJIJI CHA MAMBA WILAYA YA CHNUYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ASANGILWISYE MWAISANILA (21) ALIFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUNIKWA NA KIFUSI CHA UDONGO WA KUFYATULIA TOFALI.

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 12.08.2014 MAJIRA YA SAA 15:45 ALASIRI HUKO KATIKA KIJIJI NA KATA YA MAMBA, TARAFA YA KIPEMBAWE, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA, MAREHEMU ALIANGUKIWA NA KUFUNIKWA NA KIFUSI HICHO WAKATI AKICHIMBA UDONGO KATIKA ENEO HILO.

KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI MKOA WA MBEYA BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA JAMII KUWA MAKINI KATIKA SHUGHULI ZAO HASA KWA KUCHUKUA TAHADHARI ILI KUEPUKA MATATIZO.


TAARIFA ZA MISAKO:


JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. JAMSE MBILINYI (27) NA 2. AMBWENE SANGA (25) WOTE WAKAZI WA KIWIRA ROAD WAKIWA NA BHANGI UZITO WA KILO MOJA KWENYE MFUKO WA RAMBO.

WATUHUMIWA WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 12.08.2014 MAJIRA YA SAA 19:40 JIONI HUKO KATIKA ENEO LA KIWIRA ROAD, KATA YA KAWETERE, TARAFA YA TUKUYU MJINI, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. WATUHUMIWA NI WAUZAJI NA WATUMIAJI WA BHANGI HIYO, TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.

KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI MKOA WA MBEYA BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI HATARI KWA AFYA ZAO NA NI KINYUME CHA SHERIA.

Imesainiwa na kutolewa na:
[BARAKAEL N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Wednesday, August 13, 2014

MILA NA TAMADUNI ZA MTANZANIA


Tanuri linalosadikiwa kuwa lilikuwa likitumiwa na wahunzi zaidi ya miaka 100 iliyopita kuyeyushia udongo wenye madini ya chuma na kisha kutuyatumia kwaajili ya kutengenezea zana mbalimbali ikiwemo silaha za jadi kwaaji ya vita vya miaka ya zamani.Mabaki ya tanuri hili la asili yapo katika moja ya mapori yaliyopo kwenye kata ya Kapele wilayani Momba mkoani Mbeya. 

Mabaki ya matanuri haya yameendelea kupotea siku hadi siku.Huenda miaka kadhaa ijayo yasionedkane kabisa na watanzania wasiweze kujifunza kwa vitendo juu ya mambo ya kihistoria yaliyoachwa na mababu wa kabila la kinyamwanga hapa wilayani Momba.

Saturday, August 2, 2014

MBEYA CEMENT YACHANGIA MIFUKO 1000 YA SARUJI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA UNAOJENGWA CHUNYA

. Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro akipokea msaada wa Mifuko ya Saruji kutoka kwa Mkurugenzi mkuu wa kiwanda cha Mbeya Ciment Catherine Langreney. Mwandishi wa habari za michezo mkongwe George Chanda akielezea namna wilaya ya Chunya ilivyowahi kupeperusha bendera ya Tanzania kimataifa ilipotoa wanamichezo waliokwenda kushiriki mashindano ya kimataifa miaka ya nyuma MIFUKO 1000 ya saruji sawa na Tani 50 zimetolewa na kampuni ya Lafarge kupitia kiwanda chake cha Saruji cha Mbeya kwaajili ya ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo wilayani Chunya. 

 Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha Saruji Mbeya Catherine Langreney amekabidhi msaada huo kwa mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro mbele ya wadau mbalimbali waliofika kushuhudia tukio hilo katika eneo la Mbugani unapojengwa uwanja. 

 Akikabidhi msaada huo.Langreney ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano katika ujenzi wa uwanja huo huku akisisitiza kua kutoa mifuko 1000 ya saruji ni mwanzo tu wa mahusiano mazuri baina ya kiwanda na halmashauri ya wilaya ya Chunya.

 Amesema lengo la kiwanda ni kuendelea kuisaidia jamii inayoishi jirani kujenga miji ya kisasa yenye muonekano mzuri na kwa bei nafuu na kutaja ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo sawa kuwa miongoni mwa vitu vinavyohitajika katika miji bora. 

 Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro ameishukuru kampuni hiyo kwa kuungana na wadau wengine walioamua kujitoa kuchangia michango ya hali na mali ili kuwezesha kujengwa kwa uwanja huo. 

Amesema hadi kukamilika kwa ujenzi huo utakaokuwa na viwanja vya michezo mbalimbali ndani yake zinahitajika zaidi ya shilingi bilioni nane na hadi hivi sasa wadau wameweza kuchangi kiasi cha shilingi milioni 107 zikiwa ni fedha taslimu na nguvu kazi.