Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, August 20, 2014

WATOTO 9700 WAKABILIWA NA UTAPIAMLO KALAMBO

WATOTO 9700 waliopo katika vijiji vya Kisumba, Kasote na Chisenga kwenye kata ya Kisumba vilivyoko wilayani Kalambo mkoani Rukwa wanakabiliwa na tatizo kubwa la utapiamlo mkali kufuatia kuwepo kwa malezi duni kutoka kwa wazazi na walezi wao.

Hali hiyo imesababisha mkoa wa Rukwa kuwa miongoni mwa mikoa mitano ambayo inakabiliwa na tatizo la udumavu licha kuzalisha kwa wingi mazao ya chakula hususani ni mahindi.


Baadhi ya wanawake wa kijiji hicho walisema hayo wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi jana wakati wa sherehe za siku ya afya kijiji iliyoandaliwa katika kijiji cha Kisumba iliyoandaliwa na shirika la Africare linalotekeleza mradi wa wazazi na mwana wenye lengo la kupunguza vifo vya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano mkoani humo.

Mmoja wa wanawake hao, Yusta Sangu alisema kuwa hali hiyo imejitokeza kutokana na kukosekana kwa elimu sahihi ya afya uzazi kwa muda mrefu kiasi cha kufanya wanawake wengi  wajifungulie majumbani bila kufuata uzazi wa mpango hivyo kuwa na idadi kubwa mno ya watoto

KWA HISANI YA BLOG YA PEMBEZONI KABISA

No comments:

Post a Comment