CHAMA Cha Demokrasia na
Maendeleo(CHADEMA), Mkoani, kimepata viongozi wapya kupitia uchaguzi
uliofanyika jana jijini Mbeya.
Katika uchaguzi wa jana,
Msimamizi wa uchaguzi huo Mratibu wa chama hicho kanda ya Nyanda za Juu Kusini,
Franky Mwaisumbe, amemtaja Joseph China kuwa mwenyekiti mpya.
China ameibuka mshindi
baada ya kupata kura 36 dhidi ya kura 19 alizopata Zabron Nzunda na nne
alizoambulia Meshack Kapange aliyejiunga na chama hicho hivi karibuni akitokea
CCM.
Kwa nafasi ya Katibu
msimamizi amesema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho wagombea wa nafasi hiyo
huomba na majina yaliyopendekezwa katika ngazi husika hupelekwa katika kamati
ya utendaji taifa ambayo huthibitisha jina moja kati ya walioomba.
Mwaisumbe amesema kwa
mkoa wa Mbeya walioomba nafasi hiyo ni aliyekuwa Mwenyekiti wa mpito wa chama
hicho mkoa, Boyd Mwabulanga,Mwenyekiti wa Wilaya ya Mbarali, Kazamoyo
Jidawaya na Fanul Mkisi.
Akifafanua zaid imatokeo
ya uchaguzi,msimamizi huyo amesema nafasi ya Mwenyekiti wa Baraza la vijana
(Bavicha)Mkoa wa Mbeya, imechukuliwa na Tito George, wakati nafasi ya
Baraza la wanawake (Bawacha) ikishikwa na Happynes Kulabya, huku nafasi
ya Mwenyekiti Baraza la wazee ikienda kwa Martin Mpwani.
No comments:
Post a Comment