Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, April 30, 2017

MAAGIZO YA JPM AKIWA DODOMA

Kabla ya kuondoka Dodoma kwenda Kilimanjaro Mhe. Rais Magufuli ameagiza mambo manne.

1. Chuo Kikuu cha Dodoma kifutiwe deni la kodi ya ardhi la zaidi ya Shilingi Bilioni 2 kama ilivyoombwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma Prof. Kikula.


2. Hati za viwanja za Dodoma zilizokuwa zinatoa umiliki wa miaka 33 tu ziongezwe hadi kufikia miaka 99 ili kuvutia uwekezaji.


3. Uwanja wa mpira ambao Mfalme wa Morocco Mohammed VI ametoa msaada wa kuujenga Dodoma, ujengwe jirani na Mjini.


4. Wizara ya Ardhi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na vyombo vingine vinavyohusika wakae na kufanya tathimini kama bado tunahitaji kuendelea kuwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA).

Saturday, April 29, 2017

MPAMBANO WA SOKA VIONGOZI WA SERIKALI NA DINI KUNOGESHA MEI MOSI MBEYA

TIMU ya Soka ya Viongozi na watumishi wa Serikali mkoani Mbeya inatarajia kumenyana vikali na timu ya Viongozi wa dini mkoani hapa,katika mchezo utakaopigwa ndani ya iwanja wa Sokoine jijini Mbeya siku ya Mei mosi.

Mchezo huo utakaopigwa jioni mara baada ya kumalizika kwa shughuli za Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya wafanyakazi duniani unatarajiwa kuwa na msisimko mkubwa kutokana na watu watakaoingia uwanjani hapo kuushuhudia wakianzia na matukio ya sherehe.

Akizungumzia mchezo huo,mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla ambaye pia ni Kocha mchezaji ndani ya kikosi cha viongozi wa Serikali leo ametamba kuhakikisha wanaibuka na ushindi mnono dhidi ya viongozi wa dini.

Amesema ushindi huo utakuwa kulipiza kisasi kwani miaka kadhaa iliyopita,timu hizo ziliwahi kumenyana ndani ya dimba la Sokoine na viongozi wa serikali wakaambulia kichapo.

Amewasihi wakazi mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kushuhudia mpambano huo akisema itakuwa sehemu pia ya wao kujifunza kuwa viongozi nao wako tayari kuonesha mfano wa ushirikiano bora kwa vitendo.


Akizungumzia kambi ya Viongozi wa dini,Meya wa jiji la Mbeya,Mchungaji David Mwashilindi amesema kwakuwa yeye atacheza upande wa viongozi wa kidini ana uhakika historia itaendelea kujirudia kwa viongozi wa Kiserikali kufungwa.