Wednesday, November 26, 2014
Sunday, November 23, 2014
WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 120,YUMO ASKARI POLISI PC JAMES
MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbeya imewahukumu kifungo cha miaka 120 watu wanne akiwemo aliyekuwa askari wa jeshi la Polisi baada ya kukutwa na hatia ya unyang’anyi wa kutumia silaha.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, James Mhanusi,ambapo mbali na kuwatia hatiani washitakiwa hao Mahakama hiyo pia imemuachia huru mshtakiwa mmoja kwa kile kilichoelezwa kuwa hakuna ushahidi unaomhusisha na tukio moja kwa moja.
Mwendesha mashtaka wa Serikali,Catherine Paul, aliwataja washtakiwa kuwa ni aliyekuwa Askari wa Jeshi la Polisi,8303 Pc James, Elinazi Mshana,Lusajo Jeremia na Abdalah Mohamed ambao kwa pamoja walitenda kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha Oktoba 7, 2013.
Mwendesha mashtaka huyo alisema watuhumiwa hao wenye kesi namba 23/2014 walitenda kosa hilo kinyume cha kifungu cha 287 (a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 ambapo walifanikiwa kupora Kahawa yenye thamani ya shilingi Milioni 119.2 yenye uzito wa kilogramu 30091.
Akisoma Hukumu kwa watuhumiwa hao, Hakimu Mhanusi amesema kutokana na ushahidi wa upande wa mashtaka na upande wa utetezi mahakama imeona mshtakiwa namba tatu katika kesi hiyo ambaye ni Gwantwa Malakasuka hakukuwa na ushahidi unaomtia hatiani pasipo shaka hivyo akaamuru kuachiwa huru.
Kwa upande wa Washtakiwa wengine, amesema ushahidi wa mazingira pamoja na kutambuliwa na shahidi wa kwanza ambaye pia ndiye aliyekuwepo eneo la tukio unathibitisha pasipo shaka kutenda tukio hilo kutokana na kufanya tukio hilo majira ya jioni wakati kuna mwanga hivyo ilikuwa rahisi kutambuliwa.
Thursday, November 20, 2014
ASKARI ALIYEMUUA MWANAFUNZI HUYU AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA
Haya ni baadhi ya majeraha aliyojeruhiwa askari alipokutwa Univesal Pub siku ya Valentine akiwa na mwanamke aliyesadikiwa kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na askari Maduhu
Mwili wa mwanafunzi huyo kabla ya kuzikwa mara baada ya kuagwa na ndugu,jamaa na marafiki.Jeshi la polisi liligharamia shughuli za maziko ya mwanafunzi huyo na hapo ndipo shitaka likaanza kuunguruma mahakamani.
HABARI KAMILI
MAHAKAMA
Kuu kanda ya Mbeya imemhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa askari wa jeshi la
polisi F 5842 DC Maduhu aliyekuwa akikabiliwa na shitaka la mauaji ya
mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji(TEKU) Daniel Mwakyusa.
Aidha
mahakama hiyo pia imewaaachia huru washitakiwa wengine wawili wa kesi hiyo F
7769 DC Shaban na WP 6545 DC Neema baada ya kuwakuta hawana hatia.
Hukumu
hiyo ya kesi namba 16 ya mwaka 2013 imetolewa leo(Nov 19) na jaji Rose Temba
baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili.
Awali
ilielezwa mahakamani hapo na mawakili wa serikali Archiles Mulisa akisaidiwa na
Catherine Paul kuwa washitakiwa walifanya mauaji ya kukusudia mnamo Februari 14
mwaka 2012 kinyume cha kifungu namba 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama
ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.
Kwa
mujibu wa Wakili Mulisa washitakiwa hao kwa pamoja walihusika na mauaji ya
Daniel Mwakyusa baada ya kumpiga marehemu huyo kwa kutumia silaha inayodhaniwa
kuwa ni bunduki nje ya ukumbi wa starehe ujulikanao Univesal uliopo Uyole
jijini Mbeya.
Akitoa
hukumu ya kesi hiyo,jaji Temba amesema mshitakiwa namba moja DC Maduhu
anahusika moja kwa moja na mauaji hayo kutokana na ushahidi wa kimazingira
ikiwamo yeye kuwa mtu wa mwisho kuondoka na marehemu eneo la tukio na kumpeleka
kwenye gari,risasi tatu kupungua kwenye bunduki yake na pia kuwa mtu wa mwisho
kurejesha silaha kituoni.
Wednesday, November 19, 2014
BADO HAKUJACHANGANYA,TUNASUBIRI WATEJA WAMWAGIKE
Baadhi
ya vibanda vilivyojengwa na wafanyabiashara wadogo(Wamachinga) baada ya
halmashauri ya jiji la Mbeya pembezoni mwa Bustani ya jiji vikionekana
havijaanza kutumika.
Licha ya mamlaka husika kupeleka magari madogo ya abiria maarufu kama daladala katika barabara za eneo hilo bado baadhi ya wamachinga wanasema biashara haijawa nzuri kama maeneo waliyokuwa wakifanyia shughuli zao awali
Licha ya mamlaka husika kupeleka magari madogo ya abiria maarufu kama daladala katika barabara za eneo hilo bado baadhi ya wamachinga wanasema biashara haijawa nzuri kama maeneo waliyokuwa wakifanyia shughuli zao awali
Tuesday, November 18, 2014
Saturday, November 15, 2014
MAHAFALI YA KOZI YA NNE YA ASKARI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI YALIVYOFANA
Wahitimu wa mafunzo ya awali wakipita mbele ya mgeni rasmi kwa ukakamavu kwenye mahafali yaliyofanyika katika chuo cha Magereza Kiwira kilichopo wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
Mgeni Rasmi Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Pereira Ame Silima akikagua gwaride la wahitimu
Naibu waziri akikabidhi vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri kwenye mafunzo yao
Kikosi cha kujihami kikiwa uwanjani tayari kuonesha namna askari wa Zimamoto na Uokoaji anavyoweza kupambana na adui pasipo kutumia silaha za moto
Askari wa kike akionesha umahiri wa kuvuka kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kupita juu ya kamba
Mgeni Rasmi Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Pereira Ame Silima akikagua gwaride la wahitimu
Naibu waziri akikabidhi vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri kwenye mafunzo yao
Kikosi cha kujihami kikiwa uwanjani tayari kuonesha namna askari wa Zimamoto na Uokoaji anavyoweza kupambana na adui pasipo kutumia silaha za moto
Askari wa kike akionesha umahiri wa kuvuka kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kupita juu ya kamba
Subscribe to:
Posts (Atom)