Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, November 8, 2014

RUNGWE WAPIGWA JEKI KUKAMILISHA UJENZI WA MAABARA

 Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela (Kushoto)akipokea msaada wa saruji kutoka kwa mkurugenzi wa mradi wa kampuni ya State Grid mhandisi Andrew Mwaipaja


 Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela (Kushoto)akipokea msaada wa saruji kutoka kwa Mkurugenzi wa fedha wa TOL Gases Evarist Telafu 




MSAADA wa Saruji na Sealingboard wenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 4.7 umetolewa kwa wilaya ya Rungwe mkoani hapa ili kuiwezesha wilaya hiyo kukamilisha ujenzi wa maabara kwa wakati.

Kampuni ya State Grid inayosambaza umeme vijijini kupitia wakala wa umeme vijijini(REA) imetoa mifuko 100 ya saruji na sealing board 80 vyote vikiwa na jumla ya thamani ya shilingi milioni tatu na Kampuni inayojishughulisha na uzalishaji na uchakataji hewa mkaa ya TOL Gases imekabidhi mifuko 100 ya Saruji yenye thamani ya shilingi milioni 1.7.

Wakikabidhi msaada huo mkurugenzi wa miradi wa kampuni ya State Grid mhandisi Andrew Mwaipaja na Mkurugenzi wa fedha wa TOL Gases Evarist Telafu wamesema kampuni hizo zimechukua uamuzi wa kusaidia ujenzi wa maabara za shule za sekondari baada ya kuguswa na mikakati ya ujenzi huo.


Akipokea msaada huo,Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispini Meela amesema kampuni hizo mbili ambazo shughuli zake ni za kisayansi zimeonesha mfano mzuri wa wadau wa masuala ya sayansi kutowaachia wazazi pekee kutekeleza agizo la rais.


Mkuu huyo wa wilaya amesema licha ya kuwepo kwa changamoto za baadhi ya wananchi kutoona umuhimu wa kuchangia upo uhakika wa kutosha kuwa maabara katika shule za sekondari wilayani hapa zitakamilika kabla ya Novemba 15 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment