Friday, January 31, 2014
CBE WAELEZA MIKAKATI YAO BAADA YA KUFUNGUA TAWI MBEYA
Mkuu wa vyuo vya Elimu ya Biashara nchini(CBE) Profesa Emanuel Mjema akifafanua jambo katika kikao chake na waandishi wa habari juu ya ujio wa CBE mkoani hapa ambapo tayari wanapokea maombi ya wanaotaka kujiunga na chuo hicho mwaka huu wa masomo.
Profesa Mjema anasema Tanzania ina uhaba mkubwa wa wataalamu wa elimu ya biashara hali inayopelekea hata masomo ya biashara mashuleni kukosa walimu napia watanzania kuendelea kufanya biashara zao bila elimu hiyo hali aliyosema inawaathiri kiutendaji
CBE TAWI LA MBEYA WAKO KATIKA JENGO LA OPEN UNIVERCITY KARIBU NA MZUMBE
Wednesday, January 29, 2014
OPARESHENI YA KUKAMATA NGUO ZA NDANI ZA MTUMBA JIJINI MBEYA
Afisa viwango na mkaguzi wa TBS Paul Manyirifa akizungumza na waandishi wa habari juu ya oparesheni hiyo iliyomalizika kwa kumkamata mtu mmoja pekee aliyekuwa akiuza soksi za mtumba katika soko la Mbalizi
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi akielezea namna jeshi la polisi litakavyoendelea na oparesheni ya kukamata nguo za ndani za mtumba
Oparesheni ilimalizika kwa kuteketeza bidhaa zilizokamatwa nje ya jengo la ofisi ya kamanda wa polisi mkoani Mbeya.
Subscribe to:
Posts (Atom)