Na Joachim Nyambo.
BIASHARA ya vileo inazidi kushamiri siku hadi siku
mkoani Mbeya kama ilivyo kwa maeneo mengine nchini.Kushamiri kwa biashara hii
kunakoendana na kupanuka kwake kunasababisha wafanyabiashara kubuni mbinu mpya
kila kukicha.Lengo la ubunifu huu ni kuvutia wateja.
Mkoani hapa mji ulio na bishara kubwa ya vileo ni
jiji la Mbeya.Maeneo kama ya Mwanjelwa,Kabwe,Soweto,Ilomba na Sae yaliyopo
pembezoni mwa barabara kuu yanaonekana kuwa na baa nyingi ikilinganishwa na
maeneo ya pembezoni mwa jiji hilo.
Ingawa mkoa wa Mbeya unanafasi kubwa ya kuongoza kwa
kuwa na makanisa mengi nchini,uwingi wa nyumba hizo za ibada bado haujafikiaa
maeneo yanayouza vilevi.Yawezekana unapovuka kanisa moja kabla ya kulikuta
jingine utakutana na baa,au Grocery zaidi ya tano mpaka sita.
Uwepo wa maeneo mengi ya kuuza mvinyo unatokana na
jiji hili kuwaa moja ya maeneo nchini yenye kupata wageni wengi achilia mbali
kipato kizuri cha wakazi wake.Wapo wageni ambao huingia jijini hapa kutoka
mikoa mbalimbali nchini kila siku.Wapo pia wageni ambao huingia wakitokea nchi
mbalimbali za jirani zikiwemo Zambia,Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo(DRC).
Wengi wa wageni hawa ni wafanyabiashara ambao ama
huingiza bidhaa kutoka makwao au kuja kuchukua zile zinazozalishwa mkoani hapa
yakiwemo mazao ya chakula na biashara.Mazao hayo ni pamoja na
Ndizi,Mahindi,Kokoa,Mpunga na Kahawa.
Wataalamu wa masuala ya kiuchumi wanabainisha kuwa
Uwepo wa maeneo mengi ya starehe ni dalili za kukua kwa uchumi wa eneo
husika.Hivyo kwa Mbeya kushamiri kwa biashara ya vilevi pia ni kiashiria cha
kuwepo kwa uchumi imara na wenye kukua kila kunapokucha.
Lakini biashara ni matangazo!Hapo ndipo wamiliki wa
baa,grosery na maeneo mengine ya starehe jijini hapa wamekuwa wakukuna vichwa
kila mmoja akitafuta ubunifu utakaowezesha wateja wengi kukimbilia kwake.
Kuweka wahudumu wengi na walio warembo ni moja kati
ya ubunifu ulioibuka katika siku za hivi karibuni jijini hapa.Wafanyabiashara
za mvinyo wanasema njiaa hii inarahisisha zaidi kuwapata wateja kwakuwa
hushawishika na uwepo wa warembo.
“Usione watu wanajaa namna hii ukajiuliza maswali
mengi.Ni kweli wengine wanaweza kusema umetumia kizizi na wengine wakasema
umeboresha mazingira yako vizuri.Lakini ukweli ni kwamba siku mabinti hawa
wakipungua na mauzo yanapungua pia” alisema mmoja wa wafanyabiashara ya mvinyo
katika maeneo ya Mwanjelwa aliyeomba kutotaja jina lake wala jila la eneo lake
la biashara.
Mmiliki mwingine alisema kutokana na ushindani
uliopo wanalazimika kuwafuata mabinti mbali kwakuwa wanaotoka jirani ni
wasumbufu ahasa wanapopewa majukumu na mabosi wao.Hivyo inawalazima ama kutuma
gari au nauli ili kuwafuata wahudumu.Hasara hutokea pale wanapofika na kulizoea
jiji kwani huanza kurubuniwa na wenyeji na kuhamia sehemu nyingine.
Uchunguzi umebaini kuwa kivutio cha wahudumu hawa
kwa wateja sit u kuwahudumia vinywaji.Ipo biashara ya ngono pia inayoendelea
baina ya pande hizi mbili.Hiki ndicho hasa huwavuta wateja wengi kwenye baa
hizi zilizo na warembo wengi.
Unyonge utokanao na kutofahamu haki zao kisheria unatajwa
kuwa chanzo cha wahudumu hawa wa kike katika baa nyingi mkoani hapa kugeuzwa
watumwa wa biashara ya Ngono.
Shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Community
Media Organization(Tacomo),linasema limefanya uchunguzi na kubaini hali mbaya
kwa wahudumu wa kike katika biashara ya ngono.
Mkurugenzi wa Tacomo, Gordon Kalulunga, anasema
kumekuwepo na tatizo kubwa la wasichana wanaofanya kazi kwenye baa kukatiliwa
kingono huku msingi mkubwa wa ukatili huo ukijengwa na waajiri wao.Hali hiyo
imezidi kuwa mbaya na hatari kwa wafanyakazi hao lakini wamekuwa wakishindwa
kutoa taarifa kwa hofu ya kufukuzwa kazi na usalama wa maisha yao.
"Waajiri wakiwemo wamiliki wa baa na mameneja wamekuwa wakiwalazimisha wahudumu kufanya nao ngono kabla ya kuwapa ajira hizo.Lakini hata mara baada ya kuwaajiri huwalazimisha kufanya ngono na wateja wa baa hizo kwa makubaliano ya wateja hao kulipia kati ya shilingi elfu tano hadi elfu kumi kwa siku fedha iliyopewa jina maarufu la malipo ya kaunta.Malipo haya hayamhusishi binti anayekwenda kutumikishwa katika ngono bali itategemeana huruma ya mtu aliyekwenda naye akiamua kumlipa sawa na asipotaka pia haya” alisema Kalulunga.
"Waajiri wakiwemo wamiliki wa baa na mameneja wamekuwa wakiwalazimisha wahudumu kufanya nao ngono kabla ya kuwapa ajira hizo.Lakini hata mara baada ya kuwaajiri huwalazimisha kufanya ngono na wateja wa baa hizo kwa makubaliano ya wateja hao kulipia kati ya shilingi elfu tano hadi elfu kumi kwa siku fedha iliyopewa jina maarufu la malipo ya kaunta.Malipo haya hayamhusishi binti anayekwenda kutumikishwa katika ngono bali itategemeana huruma ya mtu aliyekwenda naye akiamua kumlipa sawa na asipotaka pia haya” alisema Kalulunga.
“Kibaya zaidi ni kwamba tumebaini uwepo wa biashara
ya binadamu ambapo kuna wahudumu wamekuwa mawakala wa kuwanunua wenzao mikoani
kwa kuwalaghai kuwa waje Mbeya kufanya kazi za Hoteli na kulipwa fedha nyingi,
ahadi ambayo haitimii kwani wakifika hapa wanaishia kutumikishwa kingono kwenye
baa wanazoajiriwa" aliongeza Kalulunga.
Mkurugenzi huyo aliitaja mikoa ambayo wasichana wengi wanatolewa huko na kuletwa bmkoani Mbeya kutumikishwa kingono kuwa ni pamoja Singida, Iringa, Njombe na Ruvuma.
Mkurugenzi huyo aliitaja mikoa ambayo wasichana wengi wanatolewa huko na kuletwa bmkoani Mbeya kutumikishwa kingono kuwa ni pamoja Singida, Iringa, Njombe na Ruvuma.
“Mkoa wa Singida unaongoza katika jambo
hili.Tulichobaini ni kuwa wengi wanadanganywa kwa kuahidiwa mambo makubwa
wakiwa makwao.Ndiyo sababu utakutana na mabinti wadogo wanaotoka kwenye mkoa
huo wakifanya kazi za uhudumu katika baa za hapa mjini.Wapo pia wanaokuwa
wametoroka mashuleni na kuja hapa”
“Ukweli wanapofika hawakutani nay ale walioahidiwa
wakiwa nyumbani.Hujikuta wametumbukia kwenye hatari ya ulevi na ukahaba kwa
kulazimishwa na waajiri wao”
“Wanajikuta kuhiari utumwa wa kuuzwa kwakuwa
wanapofika hupewa chumba kimoja kwaajili ya kulala na kuhifadhi vitu vyao kama
nguo.Haijalishi wako wengi kiasi gani.Wengine hupewa godoro na kitanda kimoja
ili walale hapo.Wao huviita vyumba hivi Gheto.Siku pekee ambayo binti anaona
analala vizuri ni pale anapobebwa na mwanaume kwenda kufanya naye ngono.Kwakuwa
watalala wawili tofauti na Gheto anajiona mwenye bahati.Huenda pia akala
chakula kizuri zaidi ya wanachokula wenzie Gheto” anasema Kalulunga.
Mkurugenzi huyo anasema ili kukabiliana na hali
hiyo,Tacomo wameandaa mpango mkakati wa mafunzo kwa wahudumu kwa kushirikiana
na wadau wengine watakaoona kuna umuhimu wa jambo hili kufanyika, ili kuweza
kutoa elimu kwanza ya kujitambua wahudumu hao ili kuwaondolea woga wa kutoa
taarifa.
Aliwaomba wadau mbalimbali kuona umuhimu wa kushiriki katika mpango huo huku akivitaja vyombo vya habari kuwa mhimili muhimu utakaowezesha kuikomboa jamii ya wahudumu wa baa.
Aliwaomba wadau mbalimbali kuona umuhimu wa kushiriki katika mpango huo huku akivitaja vyombo vya habari kuwa mhimili muhimu utakaowezesha kuikomboa jamii ya wahudumu wa baa.
Kadhalika aliwataka wahudumu wa kike kwenye baa
mkoani hapa,kujitokeza kwenye vyombo vya habari na sheria, kutoa malalamiko ya ukatili
wa kijinsia hasa rushwa za ngono wanazofanyiwa.
Uchunguzi pia uliofanywa na mwandishi wa makala haya
umebaini uwepo wa uwezekano mkubwa wa wahudumu hawa kuambukizwa maaradhi kwa
njia ya ngono.Wateja wengi huwanunuliwa pombe wahudumu wanaolenga kuondoka nao
siku husika.Mara nyingi wawili wote hulewa na wanapofikia uamuzi wa kwenda
kufanya ngono uhakika wa ngono salama unakuwa mdogo.
“Kama tunajikuta tumebeba mimba kutokana na wanaume
hao hao tunaolewa nao iweje kwa magonjwa.Ni kweli upo uwezekano mkubwa wa
kupata pia maambukizi kwakuwa wakati mwingine tunakosa namna ya kujitetea hasa
pale mwanaume anapokuwa amekulipia kaunta na umekunywa bia zake” alisema
mhudumu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Jasmini japo alisema hilo ni
jinalake la mjini tu.
“Inafikia wakati Yule anayepata wanaume wengi
anaonekana mwenye bahati zaidi ya ninyi wengine.Atakula vizuri,atavaa
vizuri,atasuka vizuri na atapendeza zaidi hata tunapokuwa tumeingia
kazini.Anakuwa amejitengenezea mtaji mzuri wa kupata mwanaume mwingine aliye na
fedha nyingi.Hivyo unapoanza shughuli hii kwa kumpata mwanaume mwenye nazo
unakuwa umejipatia mtaji mzuri sana.”alisema dada huyo.
Histori pia inaonesha kuwa mabinti wengi huanza
kutumia vilevi wanapowasili jijini hapa na kuanza kazi ya uhudumu.Wakiwa kwao
hawatumii na hata ukiwauliza wanakwambia hawakuwahi kutumia kilevi chochote
tangu kuzaliwa kwao.
Hatua hii inazua hofu ya kusafirishwa kwa magonjwa
ya zinaa kutoka jijini hapa na kuyapeleka katika jamii wanazotoka mara
wanapokwenda kwenye mapumziko.Wazazi wengi wa mabinti hawa sambamba na jamii
zinazowazunguka wanaamini kuwa ni wafanyakazi katika mahoteli makubwa.Hii ni
kwakuwa wengi wa wazazi hawa hawajafika jijini hapa kuona nini watoto wao
wanafanya.
Uchunguzi unaonesha waahudumu hawa kulipwa mishahara
midogo kutokana na uwingi wao.Anaebaki kutegemea mshahara ni wazi atabakia
kuishi maisha magumu na kuwa ombaomba kwa wenzie.Wapo pia wahudumu ambao
huwaomba mameneja kuwaruhusu wafanye kazi pasipo kuwalipa.Malipo yao hujilipa
wenyewe kutokana na ubunifu wao.Mara nyingi hawa ni wakongwe kwenye biashara
hii na wanaona kulipwa ujira kunasababisha waajiri kuwabana.
Halii hii ni changamoto kwa jamii,sit u wanakotoka
mabinti hawa.Bali pia maeneo wanayofanyia shughuli zao.Ni wakati kwa mamlaka
husika pia kulivalia njuga suala hili na kulitafutia ufumbuzi ili kuokoa kizazi
hiki na kijacho.Nasema nihatari kwakuwa biashara hii inaendelea kukua kila
siku.
No comments:
Post a Comment