Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, March 22, 2016

ZOLA D APONDA WATUNISHA MISULI WENZAKE



Image result for Zola  DMSANII wa Muziki wa hip hop laini nchini David Michael Mlope maarufu kama Zola D ameibuka na kuwaponda vijana wanaofanya mazoezi ya kutunisha misuli akisema wanahatarisha afya zao kutokana na dawa wanazotumia.

Zola D ambaye pia ni mmoja wa mabondia nchini alibainisha hayo alipozungumkza na waandishi wa habari alipokuwa mkoani Mbeya ambapo alisema tabia ya Mapenzi ya jinsia moja ni miongoni mwa matokeo ya Dawa wanazotumia watunisha misuli ili kutanua misuli yao kwa haraka.


“Vijana wengi hivi sasa  wanatumia kwa wingi dawa za kutunisha misuli maarufu kama ‘doping’ ili waweze kutanua misuli yao kwa haraka pale wanapohitaji.Kwa sababu zinazotajwa kuwa ni kutafuta ajira kama vile ulinzi kwenye kumbi za starehe, ulinzi wa watu maarufu(bodyguard) na wengine mashindano ya kunyanyua vitu vizito au wakiutafuta utanashati wanatumia dawa hizi bila kujua madhara yake baadaye” alifafanua Zola D.


Alisema dawa hizo maarufu kwa jina la Anabolic Steroids husaidia kutunisha misuli ndani ya muda mfupi lakini madhara yake ni makubwa ambapo mtumiaji huweza kupata magonjwa ya kansa, kupanuka kwa moyo na kupasua mishipa ya damu inayopelekea kupoteza maisha.

Alisema mbali na madhara hayo pia vijana wengi hupoteza uwezo wa kufanya mapenzi jambo linalowapelekea kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja kutokana na kupoteza nguvu za viungo vya uzazi inayosababishwa na matumizi ya madawa hayo.

Alibainisha kuwa kutokana na madhara hayo kwa vijana kupitia kampuni ya Tanzania Streetsworkout ameanzisha aina ya mazoezi ambayo hayahusiani na kwenda gymu wala kunyenyua vitu vizito mazoezi ambayo yanamlenga kila mtu bila kujali umri wala jinsia


Alisema mazoezi ni tiba ya magonjwa mengi hivyo ni muhimu kila mtu akaona umuhimu wa kufanya mazoezi ambayo sio lazima kunyenyua vitu vizito ilikuwa na misuli mikubwa bali ni kujenga utimamu wa mwili ili kujiepusha na magonjwa.
Image result for Zola  D
Aliongeza kuwa aina hiyo ya mazoezi wanayofundisha wao ni yale ambayo hufanywa nyumbani, chumbani, ofisini na hata barabarani ambapo kila mtu anaweza kufanya mazoezi kwa dakika tatu na kuendelea kadri atakavyojipangia lakini matokeo yake ni makubwa kutokana na mabadiliko anayoyapata.

Alisema kwa sasa kupitia kampuni hiyo,wanazunguka nchi nzima lengo likiwa ni kuhamasisha vijana,wazee na watoto kuacha kutumia dawa za kutunisha misuli na badala yake wajikite kwenye mazoezi ya kawaida ili kujenga afya zao na hatimaye kujikita katika uzalishaji mali.Image result for Zola  D

No comments:

Post a Comment