WATU watatu wameuawa kwa kunyongwa na kisha miili
yao kuchomwa moto katika Nyumba ya kulala wageni iitwayo Mexico Guest House
iliyopo wilayani Kyela mkoani Mbeya walikokuwa wamepanga vyumba vitatu tofauti.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ahmed
Msangi waliouawa wametambuliwa kwa majina waliyoandika katika kitabu cha
Mapokezi aliowataja kuwa ni wafanyabiashara Mariam Hassan aliyepanga chumba
namba 15 na Abbas Yasini aliyepanga chumba namba 14 na mkulima Tatizo Adam
aliyepanga chumba namba 103.
Kamanda Msangi amesema mnamo Machi 19 saa 10 jioni
walifika wageni wane katika Guest hiyo kati yao watatu wakiwa wanaume na
mwanamke mmoja ambapo walikodi vyumba vitatu na Marium aliingia katika chumba namba
15 akiwa na mwanaume mmoja ambaye hakuandika taarifa zake kwenye kitabu cha
orodha ya wageni.
Amesema majira ya saa moja jioni watu hao ambao wote
walisema wanatokea Songea mkoani Ruvuma walionekana wakitoka na baadaye waliporejea
wakaingia na kukaa chumbani kwa Marium na kufanya maongezi huku wakinywa
vinywaji.
Mnamo Machi 20 saa 1:30 asubuhi mtu mmoja aishiye
jirani na nyumba hiyo aliona moshi ukitokea kwenye chumba namba 15 alichopanga
Mariam na ndipo akawajulisha wahudumu wa gesti hiyo ambao baada ya kwenda
kukagua walikuta miili ya watu watatu ikiwa imenyongwa na kasha kuchomwa moto.
Amesema hata hivyo inadaiwa kuwa mapema siku hiyo
mwanaume aliyelala chumba namba 15 pamoja na marehemu Mariam ambaye hakuandika
taarifa zake kwenye kitabu aliondoka gesti hapo akiwa amebeba ndoo ndogo na
begi dogo ambapo aliaga kuwa yeye anasafiri lakini wenzake amewaacha
wanaendelea kupumzika.
Kamanda Msangi alisema chanzo cha mauaji hayo bado
hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi huku mmiliki wa gesti hiyo
Sprian Mtengela anashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano huku akisema miili ya
marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya Kyela kwaajili ya utambuzi.
No comments:
Post a Comment