Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, September 30, 2015

KAMPUNI YA TIGO YAKABIDHI MSAADA WA DAWATI 700 MKOANI MBEYA

 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kndoro(kulia)na Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya Tigo Diego Gutierrez wakifurahi kwa kukalia moja ya dawati 700 zilizotolewa na kampuni hiyo kwaajili ya shule 32 za mkoani Mbeya.
 Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya Tigo Diego Gutierrez akizungumza lengo la msaada huo.




Monday, September 21, 2015

IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOF PANJA WA KANISA LA MORAVIAN

Maaskofu mbalimbali wakiwa mwombea kwa kumpa baraka Askofu wa kanisa la Moravian Jimbo la kusini mchungaji Kenan Panja kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu askofu huyo iliyofanyika jumapili mjini Tukuyu wilayani Rungwe.
 Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilali akisalimiana na maaskofu mara baada ya kuwasili uwanjani kwaajili ya ibada


Wachungaji mbalimbali wa kanisa la Moraviana wakiwa katika ibada





 Mwenyekiti wa kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji Samwel Kabigi akisoma risala ya kanisa mbele ya mgeni rasmi makamu wa Rais Dk.Bilali.
 Kwaya ya  Shalom ikitumbuiza katika ibada hiyo maalumu mbelea ya makamu wa Rais Dk.Bilali.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akitoa salamu za mkoa kabla ya kumkaribisha makamu wa Rais Dk.Bilali
 Makamu wa rais Dk.Mohamed Gharib Bilali akimpongeza askofu Panja kwa kufikia daraja hilo la kiroho.Numa ya askofu na mkewe mama Panja.
 Makamu wa Rais Dk.Bilali akihutubia waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria ibada hiyo ya kuwekwa wakfu kwa askofu Panja.
  Askofu Panja akitoa neno la Shukrani mara baada ya kuwekwa wakfu.



Friday, September 18, 2015

UZINDUZI WA UTALII WA NDANI KATIKA JIWE IGEREKE IRINGA

Mgeni rasmi Afisa Utalii Tanapa Nyanda za juu kusini Risala Kabongo(katikati) akiwa na wanachama wa kikundi cha uhifadhi wa Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI) kwenye uzinduzi wa utalii wa ndani uliofanyika kwenye jiwe Igereke mkoani Iringa

Jiwe Igereke liko katika Mtaa wa Kihesa Kilolo manispaa ya Iringa mkoani Iringa.Eneo hilo linasimamiwa na kikundi cha uhifadhi wa Mazingira Kihesa Kilolo( KIUMAKI).Lengo la uzinduzi wa utalii huu wa ndani ni kuwahimiza wananchi wa Iringa  kutembelea vivutio vyao.

Maafisa wa Tanapa wakiwa na wanakikundi chini ya jiwe Igereke.


Katika jiwe hili kuna michoro ya kale kama ile ya Kondoa.Inasemekana ilichorwa na binadamu wa kale.
 

 



 
Katika uzinduzi huo pia Tanapa walikabidhi mipira kwaajili ya mchezo wa mpiara wa miguu kwa wanakikundi ili kuimarisha michezo na pia ushirikiano.

Monday, September 14, 2015

UKIRITIMBA WAKWAMISHA HALMASHAURI RUNGWE

KUTOFANYA kazi kwa umoja kwa watendaji katika halmashauri ya wilaya ya Rungwe kumetajwa kuwa chanzo cha kudorola kwa utendaji kazi ndani ya halmashauri hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alisema jana kuwa taarifa alizonazo ni kuwa watendaji ndani ya halmashauri hiyo hawana ushirikiano hata kidogo na badala yake kila mmoja anatekeleza majukumu yake kivyake.

Hali hiyo ilijidhihirisha wazi pale watendaji walipotakiwa kujibu maswali yaliyohojiwa na mkuuu wa mkoa yaliyotokana na hoja za mkaguzi na ndipo kila afisa akaonekana kuwa na majibu yake na kuleta mkinzano ndani ya kikao.

“Inaonekana hamfanyi kazi kama timu.Ninazo habari kuwa hakuna umoja kati yenu.Kila mmoja anafanya mambo yake ajuavyo yeye.” Alisema Kandoro kwenye kikao cha kupitia taarifa ya Mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG) katika mwaka wa fedha 2013/2014.

Kandoro alisema hali hiyo ndiyo inayochangia kwa kiasi kikubwa kukwama kwa shughuli za kimaendeleo na kuzalisha hoja nyingi za kiukaguzi zisizo za msingi ndani ya halmashauri hiyo.

Aliwataka watendaji wa halmashauri hiyo kutambua kuwa kufanya kazi kama timu ndiyo silaha pekee inayoweza kumwezesha kila mmoja wao kuonekana anawajibika katika nafasi yake na hivyo maendeleo ya wananchi kupatikana kwa urahisi.

Alisema anahitaji kuona wanafanya kazi kama timu kuanzia ngazi ya mkurugenzi mtendaji,menejimenti,watendaji na mpaka kwenye kata na vijiji huku wakitambua kuwa kilichowakutanisha ni kuwatumikia wananchi wa Rungwe.

Akizungumzia suala la udhibiti wa mapato ya ndani,Kandoro alisema bado inaonekana kuwepo kwa mianya ya upotevu wa fedha hivyo si kiasi chote kinachokusanywa na halmashauri kinakwenda sehemu sahihi na kuitaka ofisi ya katibu tawala mkoa kulifanyia kazi suala hilo.

Mkuu huyo wa mkoa pia aliagiza kutafutwa kwa ufumbuzi wa haraka juu ya malalamiko yaliyofikishwa kwake na watumishi wa halmashauri hiyo wakiwemo wa idara ya afya wanaolalamikia kukatwa mishahara yao pasipo sababu za msingi.

Alisema hali hiyo inakwamisha utendaji kazi wa watumishi na menejimenti kubaki ikitoa visingizio visivyo vya msingi pale inapobainika wananchi kutopata huduma kikamilifu kwenye idara husika.

TBL YAALIKA WAFANYABIASHARA KUNUFAIKA NA KIWANDA MBEYA

WAFANYABIASHARA mkoani Mbeya wamehimizwa kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda cha bia cha TBL mkoani kwao kwa kujihusisha na biashara zenye mahusiano na kiwanda hicho ili waweze kunufaika na uwepo wake.



Miongoni mwa fursa zilizopo ni pamoja na kuanzisha viwanda kwaajili ya kusaga unga wa mahindi utumikao katika kutengenezea bia.

Meneja wa kiwanda cha TBL Mbeya Waziri Jemedari alitoa hamasa hiyo alipozungumza na wanahabari mkoani hapa kwenye shindano la kuonja na kutambua ladha ya bia lililofanyika kiwandani na kuwashirikisha wanahabari kutoka vyombo mbalimbali.



Jemedari alisema bado wafannya biashara na wakulima mkoani Mbeya hawajaitumia vyema fursa ya uwepo wa kiwanda hicho hatua inayopelekea wenzao kutoka maeneo ya mbali kunufaika na fursa hiyo.



Alisema licha ya mkoa wa Mbeya kuwa miongoni mwa mikoa inayozalisha kwa wingi mahindi,bado kiwanda hicho kinalazimika kuagiza unga kutoka Arusha,Iringa,Kibaigwa na Dar es salaam.



“Wafanyabiashara wa Mbeya bado wamejikita katika biashara nyingine ikiwemo ya kununua nafaka kutoka kwa wakulima na kuziuza tena pasipo kuziongezea thamani.Hii inatulazimu kuagiza unga wa mahindi wa dona kutoka mbali wakati hapa mahindi yanalimwa kwa wingi.”



“Nadhani hawajatambua uwepo wa kiwanda hiki unavyoweza kuwanufaisha.Hatuwezi kufungua viwanda vya kusaga unga wa dona kwakuwa tutakuwa tunawanytima wengine fursa.Sisi tunatengeneza bia,tunahitaji wadau wengine wa kutuzalishia malighafi za kulisha kiwanda chetu” alisisitiza.



Alisema kwa sasa mahitaji ya unga wa mahindi wa dona kiwandani hapo ni mkubwa ambapo jumla ya tani 30 hutumika kwa kila juma moja hivyo ni fursa nzuri kwa watakaopenda kuwekeza kwenye uzalishaji wa malighafi hiyo.



Alisema TBL iko tayari kukutana na mfanyabiashara yeyote atakayeonesha nia ya kuwekeza katika biashara hiyo na itahakikisha inampa mwongozo juu ya namna gani malighafi inayohitajika na kiwanda inavyopaswa kutengenezwa.



Aliitaja fursa ya kilimo cha Shayiri kuwa faida nyingine ambayo wakazi wa Mbeya hawajawekeza ipasavyo kwani hadi sasa kwa mkoani hapa ni wakulima wa wilaya ya Mbozi pekee wanaozalisha huku kiwanda kikilazimika kununua bidhaa hiyo kutoka maeneo mengine ikiwepo Sumbawanga mkoani Rukwa.



Alisema licha yak ampuni kutoa fursa ya kuwawezesha wakulima katika shughuli mbalimbali za uzalishaji wa zao hilo,bado mwitikio wa wakulima mkoani hapa ni mdogo mno katika kilimo cha zao la Shayiri wakati soko ni la uhakika.

Katika shindano la kuonja bia,mtangazaji wa Mbeya FM David Nyembe anayekabidhiwa katoni ya bia aina ya Kilimanjaro Twist pichani aliibuka mshindi akifuatiwa na mwakilishi wa ITV mkoani hapa Emmanuel Lengwa aliyeshika nafasi ya pili.


Tuesday, September 1, 2015

TANGAZO TANGAZO TANGAZO



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA


 
RPC.                                                                                              Ofisi ya Kamanda wa Polisi,                                                                                                                                                                                                                                                                                                   Mkoa  wa  Mbeya,                                                                                    
Namba ya simu 2502572                                                                                              S. L. P. 260,
Fax - +255252503734                                                                                            MBEYA.             
              tanpol.mbeya@gmail.com
                
TANGAZO KWA UMMA.
JESHI LA POLISI TANZANIA LINAWAITA KWENYE USAILI WAHITIMU WALIOORODHESHWA WA SHAHADA, STASHAHADA NA ASTASHAHADA. USAILI UTAFANYIKA KUANZIA TAREHE 03.09.2015 HADI TAREHE 04.09.2015 KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI HADI SAA KUMI JIONI KATIKA MAENEO YAFUATAYO:-
·         FANI YA UTAWALA, UCHUMI, USIMAMIZI WA SHERIA NA UTEKELEZAJI [BALE], UALIMU, UANDISHI HABARI, UHANDISI MADINI [MINING ENGINEERING], UGAVI, LUGHA, USHAURI NASIHI, KATIBU MUKTASI, LAND SURVEY CATHOGRAPHER NA GEOMATICS WATAFANYA USAILI KATIKA CHUO CHA TAALUMA YA POLISI DAR ES SALAAM [DPA] KILICHOPO KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI JIJINI DAR ES SALAAM.

·         MAFUNDI MAGARI, MATENGENEZO YA PIKIPIKI, MAFUNDI MATENGENEZO YA UMEME WA MAGARI [AUTO ELECTRICAL], MAFUNDI RANGI ZA MAGARI, MAFUNDI MAGARI, MAFUNDI USHONAJI,MAFUNDI BODY ZA MAGARI NA MADEREVA. USAILI WA KADA HIZI UTAFANYIKA KIKOSI CHA POLISI UFUNDI KILICHOPO KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI DAR ES SALAAM.


·         MATENGENEZO YA KOMPYUTA, FAX & PHOTOCOPY MACHINES NA MAWASILIANO YA REDIO [DIPLOMA IN RADIO COMMUNICATION], USAILI WAO UTAFANYIKA NYUMA YA KIKOSI CHA UFUNDI YAANI TEHAMA KEKO CHINI.

·         WAKEMIA, BAILOJIA [MOLECULAR BIOLOGY] USAILI UTAFANYIKA MAKAO MAKUU YA POLISI YALIYOPO MAKUTANO YA BARABARA YA OHIO NA GHANA JENGO LINALOTAZAMANA NA POSTA HOUSE.


·         KADA ZA AFYA USAILI WAO UTAFANYIKA KATIKA KIKOSI CHA AFYA KILICHOPO KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI DAR ES SALAAM.

·         MANAHODHA NA MAFUNDI MITAMBO WA MELI, USAILI WAO UTAFANYIKA KATIKA KIKOSI CHA WANAMAJI KILICHOPO KARIBU NA JENGO LA MAHAKAMA YA RUFAA.

·         DAKTARI WA WANYAMA, USAILI WAO UTAFANYIKA KATIKA KIKOSI CHA MBWA NA FARASI KILICHOPO KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI DAR ES SALAAM.

·         MAFUNDI AC ZA MAJUMBANI, ARCHITECTURE DRAFTMAN, QUANTITY SURVEYORS, CIVIL ENGINEER, WELDING & FABRICATION, UMEME WA MAJUMBANI, PAINTING, ALUMINIUM & GLASS WORK, PLUMBING, MOSONRY, MOTOR REWINDING, HYDRO GEOLOGY DRILLING WELL, REFRIGERATION & AIR CONDITIONING. USAILI WA KADA HIZI UTAFANYIKA KIKOSI CHA POLISI UJENZI NDANI YA KAMBI YA POLISI BARRACKS KURASINI KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI DAR ES SALAAM.

·         FANI ZA BENDI, BRASS BENDI, WOODWIND, STRING JAZZ NA PERCUSSIVE, USAILI WAO UTAFANYIKA KIKOSI CHA BENDI KILICHOPO KANDO KANDO YA BARABARA YA KILWA KURASINI DAR ES SALAAM.

·         FANI YA URUBANI,USAILI  UTAFANYIKA  KIKOSI CHA ANGA KILICHOPO UWANJA WA NDEGE NDOGO WA ZAMANI WA J.K.NYERERE DSM.
MUHIMU:
1.      MWOMBAJI AFIKE KWENYE USAILI AKIWA NA NAKALA HALISI YA VYETI VYOTE VYA MASOMO/TAALUMA [ACADEMIC TRANSCRIPT (S)/CERTIFICATE (S) YAANI KIDATO CHA NNE, SITA, CHUO NA CHETI CHA KUZALIWA. KIAPO CHA KUZALIWA HAITAKUBALIWA.
2.      MWOMBAJI ALIYEITWA KWENYE USAILI ATALIPIA GHARAMA ZA UPIMAJI AFYA SHILINGI ELFU KUMI (10,000/=), USAFIRI, CHAKULA NA MALAZI KWA MUDA WOTE WA ZOEZI LA USAILI.
3.      AMBAYE HATAHUDHURIA USAILI KUANZIA SIKU YA KWANZA HATAPOKELEWA.
ILI KUPATA/KUONA ORODHA YA MAJINA, TEMBELEA www.policeforce.go.tz
Imetolewa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.