Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, April 29, 2013

MEMBE ACHANGIA MILIONI 10 HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE NA UKUMBI WA KANISA

WAZIRI wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa Bernad Membe jana aliongoza harambee ya kuchangia fedha kwaajili ya ujenzi wa shule ya sekondari na ukumbi wa mikutano wa kanisa la Baptist jijini Mbeya. Katika harambee hiyo ambayo zaidi ya milioni 60 zilikusanywa Membe alitoa fedha taslimu shilingi milioni 10 na kuahidi kugharamia michoro ya ramani za majengo hayo. Waziri wa afrika mashariki Samuel Sitta alichangia shilingi milioni mbili sawa na waziri wa usafirishaji Harisoni Mwakyembe.

TUCTA YALALAMIKIA KATIBA YA SASA

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi(TUCTA) mkoani Mbeya limesema kauli mbiu ya siku ya wafanyakazi mwaka huu ya Katiba izingatie usawa na haki za wafanyakazi inatokana na mapungufu lukuki yaliyopo kwenye katiba ya sasa. Mwenyekiti wa (TUCTA) mkoani hapa Alinanuswe Mwakapala aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye kikao kilichofanyika katika chuo cha wafanyakazi kilichopo Mwanjelwa jijini hapa. Mwakapala alisema zipo changamoto nyingi zinazomkabili mfanyakazi kutokana na mapungufu yaliyopo kwenye katiba na ndiyo sababu ya kuitumia kaulimbiu hiyo ili iweze kuleta msukumo kwa taifa katika maandalizi ya katiba mpya. Kutothaminiwa kwa wafanyakazi kulitajwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa na inayowafifisha moyo wananchi kuendelea kulitumikia taifa lao. Alisema kwa sasa wafanyabiashara wanaonekana kuwa na nguvu kwa serikali tofauti na wafanyakazi na ndiyo sababu wameendelea kuwa watu wa chini wanaonyonywa na wafanyabiashara. Mwakapala pia alisema kupitia sherehe za mei mosi wanataraji kufikisha kilio cha kuomba kupunguzwa kwa kiwango cha kodi kwa mfanyakazi kutoka asilimia 14 ya sasa hadi asilimia tano ya mshahara. Alisema pia watawasilisha ombi la kuomba kupandishwa kwa kiwango cha kima cha chini cha mshahara walau kufikia shilingi laki tano. Mwenyekiti huyo alisema mamombi hayo yanatokana na kupanda kwa gharama za maisha hususani nauli ambapo asilimia kubwa ya mshahara wa mfanyakazi kwa sasa unaishia kwa kugharamia nauli za kwenda na kutoka kazini hivyo kuishi maisha ya kuganga njaa.

Wednesday, April 24, 2013

MAUAJI TENA

MAUAJI yatokanayo na imani za kishirikina yamezidi kuugubika mkoa wa Mbeya na sasa hali inatisha na kuhitaji uwepo wa mikakati ya ziada kupambana na hali hiyo. Siku chache baada ya watu watatu kuuawa kwa imani za kishirikina akiwemo mfanyakazi wa reli ya Tanzania na Zambia(TAZARA) Ambrose Lucas aliyedhaniwa kuwa na lengo la kuiba watoto mtu mwingine pia ameuawa akituhumiwa kuwa mchawi. Aliyeuawa safari hii amefahamika kwa jina la Laison Mjaha(78) mkulima na mkazi wa kijiji cha Mawelo wilayani Chunya mkoani hapa. Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Barakael Masaki amesema kifo cha Laison kilibainika jana saa 4:00 asubuhi baada ya kukutwa akiwa ameuawa kwa kupigwa na sululu kwenye paji la uso wake nyumbani kwake. Alisema mbinu iliyotumika ni wauaji ambao hadi sasa hawajafahamika kumvamia mkazi huyo alipokuwa amelala nyumbani kwake na kasha kumtendea unyama huo kwa njia ya kujichukulia shetia mikononi. Masaki amesema mauaji hayoyanahusishwa na imani za kishirikina kwakuwa kwa muda mrefu marehemu alikuwa akituhumiwa kujihusisha na vitendo vya ushirikina kijijini hapo.
WARUNDI 18 MBARONI.WAKAMATWA NA POLISI WAKIWA WAMEJIFICHA VICHAKANI WILAYANI KYELA BAADA YA KUTIMULIWA KATIKA KAMBI YA WAKIMBIZI NCHINI MALAWI.WAMO WATOTO TISA NA WATU WAZIMA TISA.WANAUME NI 13 NA WANAWAKE WAATANO

Tuesday, April 23, 2013

WAWILI WAUAWA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA MBEYA

WATU wawili wamefariki dunia katika matukio ya mauaji tofauti yaliyotokea mkoani Mbeya kutokana na imani za kishirikina. Tukio la kwanza la mauaji lilitokea juzi majira ya saa 3:00 usiku katika kitongoji cha Katumba kijijini Ndala kata ya Kandete wilayani Rungwe ambapo mkazi wa kijiji cha Lusasi kata ya Mpombo Lufingano Nsinge(32) aliuawa na wananchio walioamua kujichukulia sheria mkononi. Kwa mujibu wa kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa Barakael Masaki chanzho cha mauaji hayo ni wananchi hao kumtuhumu Lufingano kuwa mhusika wa mauaji ya watoto wadogo ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara kwenye maeneo hayo. Masaki alisema kabla ya kuuawa na wananchi,Lufingano alikutwa ndani ya nyumba ya mtu aliyefahamika kwa jina la John Mwasamaleba(53) mkazi wa kijiji cha Ndala ambako ilisaidikiwa aliingia ndani ya nyumba hiyo akiwa anamvizia mmoja wa watoto wa nyumba hiyo ili afanye mauaji. Baada ya wananchi kujikusanya walianza kumpiga mtu huyo kwa kutumia silaha za jadi yakiwemo mapanga,vipande vya kuni,shoka na mipini hadi alipopoteza uhai wake. Kaimu kamanda huyo alisema kufuatia tukio hilo jeshi la polisi linawashikilia watu watu wane akiwemo mwenye nyumba alimokutwa marehemu kabla ya kuuawa na wananchi. Wengine ni Angolisye Mwakalinga(30),Lucas Mwasamaleba(40) na Leah Ndemange ambaye hakufahamika umri wake mara moja lakini wote hao ni wakazi wa kijiji cha Ndala wilayani Rungwe. Katika tukio la pili lililotokea majira ya saa 7:00 ya usiku wa kuamkia jana(April 23) katika kijiji cha Chobwe wilayani Ileje,Anna Panja(60) aliuawa kwa kuchinjwa shingoni kwa kisu na watu wawili akiwemo mwanaye wa kumzaa. Kaimu kamanda Masaki alimtaja mtoto wa marehemu aliyehusika na mauaji ya mama yake kuwa ni Michael Panja ambaye akiwa na mwenzake asiyefahamika jina walimvamia mama yake aliyekuwa amelala na baba wa familia Basale Panja(76) na ndipo wakamuua kwa kumchinja shingo kwa kisu kabla ya kukimbilia kusikojulikana. Kwa muda mrefu Michael alikuwa akimtuhumu mama yake kuwa mchawi ambaye amekuwa akimloga mkwewe ambaye ni mke wa moto huyo.

TBC YAAHIDI UELEDI KATIKA UTENDAJIKAZI WAKE

SHIRIKA la Utangazani la TBC limeahidi kuendelea kuwatumikia watanzania kwa kuwapa habari zilizoandaliwa kwa umakini na weledi wa hali ya juu. Mkurugenzi wa Habari na Matukio wa TBC Mbwilo Kitugine alitoa ahadi hiyo katikaa semina ya wadau wa uandaaji wa vipindi vya shirika hilo iliyofanyika jijini Mbeya. Kitugine alisema ni wajibu wa TBC kuwatumikia wananchi ambao ndiyo walingwa hasa wa kuanzishwa kwa shirika hilo tangu awali. “Tuna tambua kuwa taifa linategemea sana shirika letu.Ndiyo sababu wakati wote tunafanya kadiri tuwezavyo ili tuweze kuwatumikia watanzania kwa kuwahabarisha juu ya mambo mbalimbali yanayotokea na kuendelea nchini.Kama ilivyo kwa vyombo vya habari vingine TBC ina wajibu wa kufanya shughuli zake kwa umakini mkubwa hasa kwa kutambua kuwa inabeba sura ya taifa.Ni kwa kulitambua hilo kila mara tunawasisitiza waandishi wetu wa habari kujikita katika uibuaji wa changamoto na pia maoni yenye kuleta suluhu kutoka kwa wadau”. Alisema Hata hivyo Kitugine alisema zipo changamoto mbalimbali zinazoukabili utendaji kazi wa TBC ikiwemo uhaba wa vifaa na pia bajeti finyu isiyotosheleza mahitaji ya uendeshaji wa shirika hilo. Lakini alisema changamoto hizo haziwavunji moyo wa kuendelea kuwatumikia watanzania kwa kuwahabarisha,kuwaelimisha na kuwaburudishaa kupitia vipindi mbalimbali vya vituo vya redio na televisheni vinavyomilikiwa na shirika hilo la kiserikali. Akifunga semina hiyo mkurugenzi wa kitengo cha usalama wa chakula kutoka mamlaka ya usimamizi wa ubora wa Chakula na Dawa nchini(TFDA) Raymond Wigenge aliwataka waandishi wa habari wa TBC kujikita kwenye uandaaji wa vipindi vya kijamii vilivyo bora ili kupambana na adui ujinga,maradhi na umasikini. Alisema kwa kuwa na vipindi vya kupambana na maadui hao tasnia ya habari nchini itakuwa yenye manufaa kwa umma tofauti na vipindi vya uchonganishi vinavyoibua chuki ndani ya jamii na kuwa kikwazo cha maendeleo. Wadau waliohudhuria semina hiyo ni pamoja na maafisa kutoka TBC,TFDA na taasisi za elimu ya juu nchini.

Sunday, April 21, 2013

SERIKALI MKOANI MBEYA KUPITIA OFISI YA OFISA HABARI WA MKOA IKO MBIONI KUANZISHA BLOGU YAKE ITAKAYOTUMIKA KUUJUZA UMMA JUU YA MATUKIO MBALIMBALI YATAKAYOKUWA YAKIFANYWA NA IDARA MBALIMBALI ZILIZOPO CHINI YA OFISI HIYO.HUENDA BLOGU HIYO IKAITWA MBEYA KWANZA.
MKAZI wa kijiji cha Magamba wilayani Mbozi Elisha Zambi(27) anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Mbeya akikabiliwa na tuhuma za unyang’anyi wa kutumia nguvu. Kijana Elisha anadaiwa kutumia nguvu kunyang’anya pikipiki aina ya T.Better yenye namba T 606 CCS yenye thamani ya shilingi milioni 1.7. Kwa mujibu wa kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya Barakael Masaki pikipiki hiyo ilikuwa mali ya Mbungu Kabeja(39) mkazi wa kijiji cha Lwati aliyekuwa akiitumia kusafirisha abiria maarufu kama bodaboda. Kaimu kamanda Masaki alisema jana majira ya saa tisa alasiri mtuhumiwa akiwa na mwenzake ambaye hakufahamika jina wala makazi yake walikodi bodaboda hiyo wakimtaka Kabeja kuwatoa kijijini Lwati na kuwapeleka kijiji cha Mlowo walikodai walitaka kwenda kupata matibabu hospitali. Kinyume na makubaliano wakiwa njiani wateja hao waliobebwa kwa mtindo maarufu wa Mshikaki uliopigwa marufuku na jeshi la polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani walimtaka dereva kusimama na kumtaka awaachie pikipiki yake. Mhanga wa tukio hilo alijitahidi kupambana na wanyang’anyi hao wawili kwa kupigana nao na ndipo alipofanikiwa kumdhibiti kijana Elisha lakini kwa bahati mbaya mtuhumiwa wa pili akafanikiwa ktoroka na pikipiki hiyo. Masaki alisema mtuhumiwa yuko mahabusu wakati uchunguzi wa kumtafuta mtuhumiwa aliyekimbia na pikipiki ukiendelea na kuhakikisha kuwa wakati wowote watuhumiwa wa tukio hilo watafikishwa mahakamani. Alitoa wito kwa raia wema walio na taarifa juu ya uwepo wa mtuhumiwa wa pili ama pikipiki inayosadikiwa kuwa ya wizi kutoa taarifa katika chombo chochote cha sheria kilichopo jirani huku akionya pia watu kutonunua pikipiki yoyote isiyo na vielelezo vya umiliki halali toka kwa muuzaji. Aliwataka pia madereva wa boda boda kutambua kuwa sheria ya kuzuia ubebaji wa abiria zaidi ya mmoja katika pikipiki moja inalenga kuwaweka salama wao hivyo wanapaswa kuizingatia.

Saturday, April 6, 2013

WATANZANIA WATAKIWA KUJIVUNIA KUMILIKI ZIWA NYASA

TANZANIA huchangia asilimia 59 ya maji ya ziwa Nyasa kupitia mito yake kiasi ambacho ni kikubwa ikilingaanishwa maji kutoka nchi za Malawi na Msumbiji. Hayo yalibainishwa na Ofisa wa maji Bonde la ziwa Nyasa Witgal Nkondola alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake. Nkondola amesema nchi jirani ya Malawi inachangia asilimia 33 ya maji ya ziwa hilo huku asilimia nane zinazosalia zikichangiwa na mito iliyopo nchini Msumbiji. Hata hivyo ofisa huyo amesema ni watanzania wachache wanaotambua kuwa mitoaa yao inachangia kwa kiasi kikubwa maji ya ziwa hilo hivyo wanapaswa kujisikia fahari kuwa sehemu ya wamiliki wa ziwa hilo. Almeitaja mito ya Songwe,Kiwira na Lufilyo iliyopo mkoani Mbeya kuwa miongoni mwa mito inayoingiza maji kwa wingi katika ziwa hilo. Amekiri pia vivutio vya utalii vilivyopo kwenye ziwa hilo na eneo zima la Bonde la Maji la Ziwa Nyasa kutotangazwa ipasavyo yakiwemo maziwa madogo ya asili 11 yaliyopo wilayani Rungwe.

Wednesday, April 3, 2013

VURUGU ZA TUNDUMA 40 MBARONI

MJI mdogo wa Tunduma wilayani Momba jana haukuwa shwari kufuatia vurugu zilizoanzishwa na kikundi cha baadhi ya wakazi huku zikihusishwa na itikadi za kidini katika suala zima la uchinjaji. Vurugu hizo zilizuka majira ya saa 2:30 asubuhi baada ya waanzilishi wa vurugu hizo kuingia katika barabara kuu na kuanza kuchoma magurudumua ya magari huku pia wakiweka mawe makubwa barabarani. Hata hivyo chanzo cha vurugu hizo kilionekana kupokelewa kwa mitazamo tofauti ambapo wapo baadhi walionekana kupinga kuwa zinahusisha masuala ya kidini kwakuwa walioonekana kushiriki ni vijana wapiga debe walioonekana kuchanganyikana na vibaka. Vurugu hizo zilisababisha kufungwa kwa muda mpaka kati ya Tanzania na nchi jirani ya Zambia kwa hofu ya usalama,shugjhuli za kibiashara zilisimama huku pia mabasi ya abiria kutoka Sumbawanga mkoani Rukwa yakizuia kuendelea na safari hadi alipofika kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Diwani Athuman. Akizungumzia tukio hilo kamanda Athuman alisema wni vigumu kusema moja kwa moja vurugu hizo zina msukumo wa itikadi za kidini ama la kwakuwa washiriki ni watu wanaonekana kupenda kutumia vurugu kujinufaisha kwa kuiba. “Tunduma kuna watu wamejenga mazoea ya wao kuonekana kama ndiyo wapenda vurugu.Wao bila kuwepo kwa vurugu hawasikii raha.Lakini pia wanaonekana kuwa na maslahi kupitia migogoro hiyo na ndiyo sababu wamekuwa wakianzisha chokochoko za kuchafua amani kila wakati”. “Leo makundi ya waharifu wameingia barabarani na wakiwa pia wanarusha mawe hovyo kwa askari waliokuwa wamejipanga kukabiliana na hali hiyo hivyo ikalazimu askari kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya wahalifu hao” Kamanda huyo alisema athari zilizotokana na vurugu hizo ni pamoja na kujeruhiwa kwa askari mmoja wa jeshi hilo baada ya wafanya vurugu kurusha mawe na kuvunja kioo cha gari ya polisi aliyokuwa akiendesha. Alisema pia kutokana na kurusha mawe hovyo wafanya vurugu walimjeruhi mwenzao mmoja ambaye alikimbizwa hospitali na kuanza kupata majeruhi. Athari ni nyingine ni kuvunja msikiti mmoja kuvunjwa na wavunjaji kutaka kuondoka na madirisha ya jingo hilo lakini wakakimbia na kuyaacha baada ya polisi kufika eneo hilo. Kamanda Athuman alisema pia nyumba ya askari mmoja ilivamiwa na kuvunjwa dirisha moja lakini kutokana na eneo hilo kuwa na mbwa wengi walifunguliwa na kuwakurupusha. Kwa mujibu wa kamanda huyo zaidi ya watu 40 walikamatwa na jeshi hilo kwaajili ya kuhojiwa juu ya tukio hilo huku pia akisisitiza hatua za kisheria kuchukuliwa kwa mtu yeyote atakayekuwa amehusika pasipo kujali ni katika itikadi ya kidini au siasa. Aliwataka wakazi katika mji wa Tunduma na mkoa wa Mbeya kwa ujumla kutokubaliana na watu wachache wanaopenda kuvuruga amani kwa lengo la wao kujinufaisha.

HATARIIIIIIIIIII

USIPENDE KUKABIDHI KAZI BILA MAELEKEZO FASAHA

Tuesday, April 2, 2013

HABARI PICHA NA Lyamba Lya Mfipa

MTOTO DEBORA ALIYEZIKWA HAI NA BABA YAKE BWANA MWANGONGA SEBULENI NYUMBANI KWAKE.1.DEBORA ENZI ZA UHAI WAKE 2.MWILI WA DEBORA BAADA YA KUFUKULIWA NA POLISI 3.KULIA NI BABA WA DEBORA ANAYETUHUMIWA KUMZIKA AKIWA HAI MWISHONI MWA MWAKA 2012 ALIPOKAMATWA JUZI

MWILI WA MTOTO DEBORAH BAADA YA KUFUKULIWA
Mwanamke mmoja anashikiliwa na polisi mkoani Mbeya kwa tuhuma za kumuuza mtoto wa kaka yake ili aweze kupata fedha kwaajili ya kusaidia katika kesi ya kaka yake. Mwanamke huyo amefahamika kwa jina la Tabu Mwashipete(40) mkulima na mkazi katika kijiji cha Mpemba wilayani Momba mkoani hapa. Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwan Athuman alisema mwanamke huyo alikamatwa juzi(Aprili mosi) majira ya saa 2:00 usiku na kumtaja mtoto aliyekuwa akiuzwa kuwa ni Hosea Mwashipete(5). Kamanda Athumani alisema mwanamke huyo alikuwa akimuuza mtoto Hosea kwa mkazi mwenzake wa kijiji cha Mpemba John Sinyinza(64) kwa gharama ya shilingi 1,000,000. Alisema sababu ya kuuzwa kwa mtoto huyo ni kutafuta fedha kwaajili ya kusaidia katika kesi inayomkabili baba wa mtoto huyo aliyetajwa kwa jina la Simon Mwashipete anayekabiliwa na kesi ya mauaji nchini Malawi. Kamanda huyo amemtaja mteja wa biashara hiyo ndiye aliyewezesha kukamatwa kwa mtuhumiwa kwani akiwa amemlipa fedha ya awali kiasi cha shilingi 100,000 alitoa taarifa polisi na kisha kuweka mtego uliowezesha kumkamata mwanamke huyo wakati wakiendelea kufanya mazunguzo ya lini atamalizia kiasi cha shilingi 900,000. Kwa mujibu wa Athuman mama wa mtoto huyo alikwisha fariki dunia hivyo Hosea amekuwa akiishi nyumbani kwa shangazi yake aliyeamua kumuuza ili kupata kiasi hicho cha fedha.

UJIO WA ATCL SONGWE ENTERNATIONAL AIRPOT MBEYA