Monday, April 29, 2013
MEMBE ACHANGIA MILIONI 10 HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE NA UKUMBI WA KANISA
WAZIRI wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa Bernad Membe jana aliongoza harambee ya kuchangia fedha kwaajili ya ujenzi wa shule ya sekondari na ukumbi wa mikutano wa kanisa la Baptist jijini Mbeya.
Katika harambee hiyo ambayo zaidi ya milioni 60 zilikusanywa Membe alitoa fedha taslimu shilingi milioni 10 na kuahidi kugharamia michoro ya ramani za majengo hayo.
Waziri wa afrika mashariki Samuel Sitta alichangia shilingi milioni mbili sawa na waziri wa usafirishaji Harisoni Mwakyembe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment