Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, November 30, 2012

TBL,WANAHABARI TULIPOAMUA KUPIMA HIV KATIKA ZOEZI MAALUMU LA KUPIMA AFYA ZA WAFANYAKAZI KATIKA KIWANDA TBL MBEYA

 Alianza Meneja wa kiwanda hicho Nicholaus Kanyamala kama anavyoonekana hapa

 Akafuata mfanyakazi mmoja baada ya mwingine.Huyu ni Stela Alexanda

 Wakafuata wafanyakazi wengine pamoja na wakazi wa kata jirani na kiwanda yaani Sisitila na Ikuti

 Kama ilivyo kawaida katika kupima HIV kila mmoja katika foleni ya kuingia kwa mnasibu/mshauri nasaha alikuwa akijiuliza majibu yatakuwaje.Kijasho chembamba kikawa kinamtoka kila mmoja.

Baada ya kupima na kupokea majibu Meneja wa kiwanda akaona umuhimu wa kuzungumza na wawakilishi wa vyombo vya habari

 Mazungumzo ya Meneja yakamvuta mwakilishi wa kituo cha Luninga cha STAR TV Husna Mlanzi na kuamua kupima pia kama alivyoamua Hosea Cheyo wa TBC ambaye hayupo pichani.
 Hakupenda kwa wakati huo apokee simu yoyote ile.Akaamua kuizima simu yake kabisaaaa.
 Kupima si tatizo sana,kungoja majibu ndiyo kazi.Husna akaanza kuwaza damu tayari imechukuliwa je majibu yangu yatakuwaje?
Hamasa ya kupima ikamkuna mmiliki wa blogu ya Lyamba Lya Mfipa.Akaamua kuingia ulingoni.Ni baada ya kujiuliza iwapo watu wote wamepima ninachoogopa ninini.Na kama ni majibu si yatakuwa mali yangu bila kujalisha ni mazuri au mabaya.

 Swali la kujiuliza ni je wewe unasubiri nini kuijua afya yako?Tambua Tanzania bila maambukizi mapya inawezekana!Hongera TBL Mbeya
Shughuli ikafungwa rasmi ambapo zaidi ya watu 190 wamepima ikiwa ni mpango wa kiwanda cha bia cha TBL mkoani Mbeya kama maandalizi ya siku ya ukimwi duniani ambayo kimkoa yatafanyika desemba mosi wilayani Mbozi.

BREAKING NEWZZZZZZZZ

ASKARI WA JWTZ WANNE KATI YA 10 WALIOKAMATWA KWA MAUAJI YA KIJANA MBALIZI LEO WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI

Wednesday, November 28, 2012


ASKARI Polisi wilayani Momba mkoani Mbeya wamefanikiwa kumnusuru Mkuu wa wilaya hiyo Abiud Saudea na jopo lake baada ya kuzingilwa na wananchi wa Kijiji cha Kamsamba.
Hali hiyo ilijitokeza kuazia majira ya saa Nane mchana leo baada ya Mkuu hyo wa wilaya kufika kijijini hapo na kuanza kuhutubia huku viongozi hao wa wilaya wakikusudia kumrejesha madarakani Mwenyekiti wa Kijiji hicho Vitus Sauzen aliyetimuliwa kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha.
Hali hiyo iliwakera wananchi na kuanza kuzomea jambo ambalo lilizusha vurugu mbele ya Mkuu huyo wa wilaya, kamanda wa polisi wa wilaya hiyo (OCD) na viongozi wengine.
Kutokana na fujo hizo, askari polisi waliingilia kati na kuwatawanya wnanchi na mabomu ya machozi hali ambayo haikufua dafu na kuamua kutumia risasi za moto ambazo zimejeruhi watu watatu ambao wamekimbizwa Hospitali ya wilaya ya Mbozi mkoani hapa.
Mbali na hao watu wanne wamekamatwa kwa kuhusika na uratibu wa fujo hizo wakiwemo viongozi wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika kata na kijiji hicho cha Kamsamba.
Waliokamatwa na Polisi ni pamoja na Richard Nyoni, Michael Simfukwe ambao ni viongozi wa Chadema. Wengine ni Jofrey Dismas na Sabati Kigaya.

OFISI ya Katibu Tawala mkoani Rukwa imefikishwa katika mahakama kuu ya kazi kanda ya nyanda za juu kusini iliyopo jijini Mbeya kwa kukiuka makubaliano ya kumlipa mtumishi madai ya malipo ya uhamisho yaliyowekwa chini ya Tume ya usuluhishi na maamuzi.

KIFO CHA MTANGAZAJI CLEMENCE MPEPO


TASINIA ya habari mkoani Mbeya imepata pigo kufuatia kifo cha mtangazaji Clemence Mpepo(Mzee wa Makabila) wa kituo cha redio cha Bomba FM cha jijini Mbeya.

Mpepo alifariki usiku wa kuamkia Novemba 28 mwaka katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alikokuwa amelazwa akiendelea kupata matibabu kufuatia maradhi ya mapafu yaliyokuwa yakimsumbua.

Enzi za uhai wake mtangazaji huyo alijipatia umaarufu mkubwa kwa mashabiki mkoani hapa na maeneo ya jirani kufuatia umahiri wake wa kutangaza kipindi cha nyimbo za asili ambapo alikuwa mtaalamu wa lugha za makabila mbalimbali hali iliyokuwa ikiwavutia wasikilizaji wengi wa kipindi hicho kilichokuwa kikirushwa kila siku ya jumamosi.

Akizungumzia kifo hicho Meneja wa redio Bomba Fredy Helbert alisema ofisi imepokea kifo hicho kwa masikitiko makubwa kutokana na ushirikiano mkubwa aliokuwa nao Mpepo mpaka anaanza kusumbuliwa na maradhi.

Alisema marehemu alianza kuugua siku chache baada ya kufunga ndoa hivi karibuni akiwa bado katika likizo ya ndoa na baadaye hali ilizidi kuwa mbaya na kulazwa katika hospitali ya Mkoa na hatimaye Rufaa Mbeya kabla ya kupelekwa Muhimbili.

“Alikuwa bado katika likizo ya ndoa hivyo hata kazini alikuwa hajaanza kuingia ndipo maradhi yalipoanza kumsumbua.Jambo lililokuwa likitupa matumaini kuwa mpaka anaondoka na mkewe kwenda Dar es salaam alikuwa na unafuu mkubwa.Alikuwa akizungumza vizuri na kucheka nasi kama tulivyokuwa tumemzoea.Ghafla tukapata taarifa hali imebadilika na leo tunazungumza msiba”.

“Ni masikitiko makubwa kwetu kama wafanyakazi wenzake.Hakuwa mtu wa kukorofishana na mtu.Mcheshi wakati wote Lakini kikazi pia japo siku hizi watu wanasema pengo linazibika kwa Mpembo kwakweli ni vigumu maana utangazaji wake ulikuwa si wa kipindi kimoja.Kila kipindi tulichompa kilipata wasikilizaji wengi” alisema.

Kwa mujibu wa meneja huyo Mpepo atazikwa siku ya jumamosi Kinyelezi jijini Dar es salaama kutokana na maamuzi ya wazazi wake.

MTANGAZAJI WA REDIO BOMBA FM CLEMENCE MPEPO AFARIKI DUNIA

TANGAZO: KWA MASIKITIKO MAKUBWA UONGOZI WA REDIO BOMBA FM, TUNATANGAZA KIFO CHA MFANYAKAZI WETU CLEMENCE MPEPO "MZEE WA MAKABILA" ALIYEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI. KWA TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWAFAHAMISHA JUU YA UTARATIBU WA MAZISHI NA PIA ENDELEA KUSIKILIZA REDIO
 
 
.
 
 
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
PRESS RELEASE” TAREHE 28/11/2012.


WILAYA YA MBEYA VIJIJINI - AJALI YA GARI KUACHA NJIA KUPINDUKA NA KUSABABISHA VIFO NA MAJERUHI 

MNAMO TAREHE 27.11.2012 MAJIRA YA SAA 19:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA IGAWILO BARABARA YA MBEYA/TUKUYU WILAYA YA MBEYA VIJIJINI MKOA WA MBEYA . GARI T.597 BVZ SCANIA LORI LIKIENDESHWA NA DEREVA AMBAYE BADO HAJAFAHAMIKA LILIACHA NJIA NA KUPINDUKA KISHA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WAWILI  AMBAO BADO HAWAJAFAHAMIKA  MAJINA WALA MAKAZI  JINSIA KIUME UMRI KATI YA MIAKA 30-35  NA MAJERAHA KWA WATU WAWILI 1. DAVI S/O MIROYI, MIAKA 18 MKAZI WA DSM NA 2. MWANSU S/O ADAM, MIAKA 28, MMAKONDE MKAZI WA MTWARA    AMBAO WAMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA MATIBABU ZAIDI. DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA AJALI. MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA NA TAHADHARI YA MATUMIZI YA BARABARA KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI. AIDHA ANATOA WITO KWA WANANCHI KUFIKA HOSPITALINI HAPO ILI KUTAMBUA MIILI YA MAREHEMU HAO NA KWA MTU/WATU WENYE TAARIFA JUU YA ALPOKIMBILIA DEREVA HUYO AZITOE POLISI ILI AKAMATWE VINGINEVYO AJISALIMISHE MARA MOJA.
Signed By,
    [DIWANI ATHUMANI – ACP]
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

ASKARI POLISI AMBAYE HAKUFAHAMIKA JINA WALA NAMBA YAKE ALIPOKUTWA NA Lyamba Lya Mfipa JIRANI NA HOTELI YA MBEYA PEACK JIJINI MBEYA AKICHORA CHINI

 ALIANZA HIVI
 AKAENDELEA NAMNA HII
 HAKUISHIA HAPO AKAZIDI KUENDELEA
AKAMALIZA KAZI YAKE NA KISHA AKAONDOKA

Tuesday, November 27, 2012

MTOTO ALIYECHOMWA MKONO NA HATIMAE KUKATWA MKONO WAKE WA KUSHOTO ALETWA MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI

MTOTO ANETH KATIKATI NA MAMA YAKE KULIA WAKIINGIA ENEO LA MAHAKAMANI LEO

WILVINA MKANDALA ANAETUHUMIWA KWA KUMUUNGUZA NA KUSABABISHA KUKATWA KWA MKONO WA MTOTO ANETH AKIINGIZWA MAHAKAMANI HUKU AKIWA HATAKI KABISA KUPIGWA PICHA
WAKAZI WENGI WA JIJI LA MBEYA NA VITONGOJI VYAKE WAMEJITOKEZA KWA WINGI KUJA SIKILIZA KESI HIYO

MTOTO ANETH AKISALIMIANA NA MAMA ALIYEMUHUDUMIA HOSPITALINI KABLA YA MAMA YAKE MZAZI KUJA TOKA BUKOBA
MAMA ANETH AKIONDOKA NA MWANAE MARA BAADA YA HAKIMU KUMUONA MTOTO HUYO NA KUPATA MAELEZO MAFUPI TOKA KWA MTOTO ANETH AMBAE ALISHINDWA KABISA KUONGEA MARA TU ALIPO MUONA SHANGAZI YAKE HUYO ALIYEMCHOMA MOTO AKIINGIA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA KESI HIYO IMEAIRISHWA MPAKA TAREHE 6/12 / 2012
MTOTO ANETH MARA TU BAADA YA KUTOKA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA AKISUBIRI KURUDISHWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA KUENDELEA NA MATIBABU
HUKU AKINA MAMA WAKIWA NA JAZBA YA KUTAKA HAKIMU AWAACHIE KIDOGO JAPO KWA DAKIKA TANO WAMFUNZE ADABU MTUHUMIWA HUYO KWANI WANADAI AMEWADHALILISHA SANA KWA KITENDO HICHO CHA KUMTESA MTOTO ANETH
KWA HISANI YA BLOGU YA MBEYA YETU    

NEWZZZZZZZZZ

TUNAZIDI KUKULETEA HUDUMA KARIBU.SIKILIZA LIVE MATANGAZO YANAYORUSHWA KILA SIKU NA KITUO CHA REDIO CHA BOMBA FM CHA JIJINI MBEYA
NI WAKATI WAKO PIA KUTANGAZA NA LYAMBA LYA MFIPA SASA
BLOG YA LYAMBA LYA MFIPA INAWAPA POLE WALE WOTE WALIOFIKWA NA MSIBA WA MSANII WA BONGOFLEVA NA MUIGIZAJI SHAROMILIONEA.

MWENYEZIMUNGU AIWEKE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU.
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
PRESS RELEASE” TAREHE 27/11/2012.

WILAYA YA MBARALI - AJALI YA GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA KUSABABISHA KIFO 

MNAMO TAREHE 26.11.2012 MAJIRA YA 14:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA MLANGALI BARABARA YA MBEYA/IRINGA WILAYA YA MBARALI MKOA WA MBEYA. GARI DFP 7322 AINA YA NISSAN PATROL MALI YA BARAZA LA KILIMO DSM LIKIENDESHWA NA DEREVA JACKSON S/O PAUL LIKITOKEA MBEYA KUELEKEA IRINGA ILIMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU AMBAYE BADO HAJAFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE JINSIA YA KIUME MWENYE UMRI KATI YA MIAKA 25- 30 NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO . CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA MISSION CHIMALA. DEREVA AMEKAMATWA. TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA NA TAHADHARI YA MATUMIZI YA BARABARA KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI. AIDHA ANATOA WITO KWA WAKAZI WA ENEO HILO KUFIKA HOSPITALINI HAPO ILI KUUTAMBUA MWILI WA MAREHEMU.

WILAYA YA CHUNYA - KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] 

MNAMO TAREHE 25.11.2012 MAJIRA YA SAA 21:20HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA ITINDI – MALEZA WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA. POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA MWASHI D/O LUGWISHA,MIAKA 25, MSUKUMA,MKULIMA MKAZI WA SAZA AKIWA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 5 . MTUHUMIWA NI MUUZAJI NA MNYWAJI WA POMBE HIYO. TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUJIEPUSHA NA MATUMIZI YA POMBE HARAMU KWANI NI HATARI KWA AFYA YAO NA NI KINYUME CHA SHERIA. 

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] NA MTAMBO WA KUTENGENEZEA 

 MNAMO TAREHE 26.11.2012 MAJIRA YA SAA 17:20HRS HUKO MPINDO BULYAGA – TUKUYU   WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA. POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA WALLACE S/O MSAMATI ,MIAKA 60, MMAKUA ,MKULIMA MKAZI WA MPINDO BULYAGA  AKIWA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 1 NA MTAMBO WA KUTENGENEZEA POMBE  HIYO  . MTUHUMIWA NI MUUZAJI NA MNYWAJI WA POMBE. TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUJIEPUSHA NA MATUMIZI YA POMBE HARAMU KWANI NI HATARI KWA AFYA YAO NA NI KINYUME CHA SHERIA.

Signed By,
    [DIWANI ATHUMANI – ACP]
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Monday, November 26, 2012

MAZISHI YA MAMA ALIYEUAWA KWA KUPIGWA NA MWANAE

 Akina mama waombolezaji wakisawazisha kaburi la marehemu Sinjembele Julius(62) aliyeuawa kwa kupigwa na mwanae Ndele Julius(25)
 Baadhi ya waombolezaji wakishuhudia mazishi ya Sinjembele yaliyofanyika Nyumbani kwake katika kitongoji cha Igawilo kata ya Swaya Mbeya

 Kaburi baada ya kuzikwa marehemu

Sunday, November 25, 2012

MATUMIZI HARAMU YA CHANDARUA

Vijana wakazi wa kijiji cha Kirando wilayani Nkasi mkoani Rukwa wakivua samaki wadogo katika ziwa Tanganyika kwa kutumia Chandarua kama walivyokutwa na Lyamba Lya Mfipa hivi karibuni.Hapa Chandarua(Mosquito Net) kimebadilishwa matumizi badala ya kumkinga binadamu asing'atwe na mbu akiwa amelala kinatumika kama nyenzo ya uvuvi.
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
PRESS RELEASE” TAREHE 26/11/2012.


WILAYA YA MBEYA MJINI - MAUAJI
MNAMO TAREHE 25/11/2012 MAJIRA YA SAA 14:00HRS HUKO SWAYA JIJI NA MKOA WA MBEYA. SINJEMBELE  W/O JULIUS, MSAFWA, 62YRS, MKULIMA NA MKAZI WA SWAYA ALIFARIKI DUNIA NYUMBANI KWAKE BAADA YA KUSHAMBULIWA KWA MATEKE NA NGUMI SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI WAKE NA MTOTO WAKE  AITWAYE NDELE S/O JULIUS. MBINU ILIYOTUMIKA NI KUMSHAMBULIWA KWA MATEKE NA NGUMI NA KUPELEKEA MAUMIVU MAKALI YALIYOSABABISHA KIFO CHAKE. CHANZO NI UGOMVI ULIOKUWEPO BAINA YA MTUHUMIWA NA KIJANA MWENZAKE NA NDIPO MAMA ALIPOKWENDA KUAMULIA NA MTUHUMIWA KUMGEUKIA MAMA YAKE. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. MTUHUMIWA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO HILO. JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUEPUKA TABIA YA KURUHUSU HASIRA ZIWATAWALE NA KUFANYA MAAMUZI YANAYOWEZA KUSABABISHA MADHARA MAKUBWA BADALA YAKE BUSARA ITUMIKE. AIDHA ANATOA WITO KWA MTU/WATU WENYE TAARIFA JUU YA MAHALI ALIKO MTUHUMIWA WAZITOE ILI AKAMATWE VINGINEVYO AJISALIMISHE MARA MOJA KWENYE MAMLAKA HUSIKA ILI SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.

Signed By
    [DIWANI ATHUMANI – ACP]
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Saturday, November 24, 2012

NYUMBA ZA WALIMU KYELA HOIIII

Moja ya nyumba za walimu katika shule ya msingi Ipyana wilayani Kyela mkoani MbeyaHali ya nyumba za walimu katika shule hiyo ni mbaya kama inavyoonekana hapa
 Chini ni dirisha la nyumba hiyo likiwa limefunguliwa

VODACOM WAPATA AJALI MBEYA

Ajali hii imetokea usiku wa kuamkia leo maeneo ya barabara ya mbalizi kuelekea mabatini Gari hiyo mali ya kampuni ya simu vodacom iliporamia nguzo ya taa za barabarani  na dereva wake amejulikana kwa jina moja tu Karinga ambae ameumia kidogo chanzo cha ajali mpaka sasa hakijajulikana





Kwa hisani ya Blogu ya Mbeya Yetu

Thursday, November 22, 2012

MATUKIO KATIKA PICHA

 Mkuu wa wilaya ya Mbeya Norman Sigala akiwasaidia mafundi wanaojenga daraja la Itiji jijini Mbeya kupika
 Mmiliki wa blogu ya Lyamba Lya Mfipa akifanyiwa vipimo
Mbele ni baadhi ya wabunge wa mkoani Mbeya wakiwa katika moja ya
mikutano mikubwa mkoani hapa.Kutoka kulia ni Aliko Kibona(Ileje),Mary
Mwanjelwa(Viti maalumu CCM),Mchnungaji Luckson Mwanjala(Mbeya V) na
Godfray Zambi(Mbozi Mashariki).

Wednesday, November 21, 2012

JWTZ 10 MBARONI KWA MAUAJI


WATU 14 wakiwemo askari 10 wa jeshi la wananchi(JWTZ) wa kikosi cha 44KJ kambi yaa Mbalizi wilayani Mbeya wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani hapa kwa tuhuma za mauaji.


Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwani Athuman amesema leo kuwa kushikiliwa kwa askari hao kunatokana na mauaji ya kijana  Petro Sanga(25)  yaliyotokea novemba 18 mwaka huu akiwa katika baa ya Power Pub ambapo askari hao wanatuhumiwa kuhusika

Tuesday, November 20, 2012

LIGI YA MWENYEKITI YAMALIZIKA


MICHUANO ya ligi ya Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya imemalizika kwa timu ya kata ya Halungu kunyakua ubingwa baada ya kuifunga timu ya kataa ya Ndalambo goli 2-1.

Halungu iliibuka bingwa wa mashindano hayo na kuzawadiwa kombe la fedha taslimu shilingi laki tatu katika mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa Vwawa ambapo hadi dakika 90 za mwanzo zinamalizika timu hizo zilikuwa sare ya goli 1-1.

RUNGWE WAJIPANGA KWA USAFI WA MAZINGIRA


SERIKALI wilayani Rungwe mkoani Mbeya imesema imejipanga kuhakikisha hali ya usafi wa mazingira inazingatia katika maeneo yote wa wilaya hiyo kwa kuanza kuwawajibisha wasiofuata utaratibu uliopo.

Mkuu wa wilaya hiyo Chrispin Meela aliyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani yaliyofanyika kitaifa juzi katika mji mdogo wa Tukuyu wilayani hapa.